Watanzania tuige mfano wa Ujerumani, tunapaswa kumsahau Magufuli na kuweka bidii kusonga mbele

Watanzania tuige mfano wa Ujerumani, tunapaswa kumsahau Magufuli na kuweka bidii kusonga mbele

Mkuu, Hitler aliwawinda sana wakosoaji, na kuwaua! Sasa hatutaacha kumlinganisha Magufuli na Hitler kwa sababu Magufuli hakuanzisha vita ya dunia. Ndio maana nimesema kwamba ulinganifu wa Magufuli na Hitler ni katika philosophy zao, mentality, sio katika matukio kama kuanzisha vita ya dunia.
Magufuli alikua na philosophy gani?
 
Sidhani kama kuna Mtanzania ambae hajui mazuri ya Magufuli akiwa raisi wa Tanzania, atapinga kwamba Magufuli hakuwa na roho ya uzalendo kwa Tanzania, alichukia ufisadi, alichukia watu ambao anawaona walikwamisha bidii zake za kuindeleza Tanzania. Hakuna Mtazania atakaepinga kwamba Magufuli alikuwa mchapa kazi kweli kweli, mwenye kupenda nchi yake na raia wa Tanzania, mzalendo namba moja.

Lakini hilo linakukumbusha nini?

Linatukumbusha kiongozi aliewahi kuwa na hulka ya Magufuli pale Germany, Adolf Hitler. Hitler alikuwa mzalendo kweli kweli. Alisimamia Germany na kuifanya Germany kuwa taifa lenye uchumi wenye nguvu kuliko mataifa yote. Alipenda uzalendo, alichukia ufisadi na usaliti dhidi ya nchi yake. Hitler alikuwa muasisi wa gari za VW, Volks Wagen (People's Car) ili kila raia wa Germany aweze kumudu kuwa na gari. Hakuna kiongozi katika Germany anaeweza kusemwa alileta maendeleo kwa nchi yake kama alivyofanya Hitler, mzalendo namba moja wa nchi yake.

Lakini sasa, nani leo unamsikia akimsifia Hitler kwa makubwa aliyoifanyia Germany? Hakuna, kwa sababu hakuna mtu aliyesahau machungu yaliyosababishwa na Hitler.

Hakuna mtu hapa Tanzania asiyejua machungu yaliyoletwa na Magufuli katika azma yake ya kuiendeleza Tanzania, machungu ambayo hayana utetezi hata uyaangalie kwa mtazamo upi. Hayana justification.

Hata hivyo, kwa tulio hai, kuwachukia Hitler au Magufuli, ambao tayari wamekufa, ni dalili kwamba tuna matatizo ya afya ya akili, tunahitaji psychiatric help. Kuwasifia pia ni tatizo, kwa sababu tunaumiza wale walioumizwa nao, ambao bado wapo hai pamoja nasi. Tutapanda gari za VW za Hitler, tutapita kwenye flyover za Magufuli, lakini hatutaimba sifa zao.

Kama Germany ilivyoamua kumsahau Hitler pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yake, Tanzania tunapaswa kumsahau Magufuli pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yetu.

Tuangalie mbele sasa. Tusahau yaliyopita, tuachane na kulinganisha uongozi wa sasa na uliopita. Tuvunje magenge. Tuanze upya.

The world and your country need YOU now, not Hitler, not Magufuli.
Mkuu kwani hilter hakumbukwi mpaka Leo?
 
Adolf Hitler alivyowaswaga wajerumani kwa vitisho, kulazimisha kuunga juhudi na kutishia kuanika siri za faragha za wanaompinga zilifanana na za mtawala John Pombe Magufuli ..

MUSIBA AFUNGUKA MAOVU YA MAKAMBA,KINANA NA NAPE / WANATAKA KUNIUA/KUNA GARI INANIFUATA


View: https://m.youtube.com/watch?v=UFMnxRfH2D0
Kikaragosi cha propaganda kilichotumika 2015 - 2021 mzalendo uchwara Cyprian Musiba na wawezeshaji wake kutoka Ikulu walikopi njia zote za propaganda za muovu Adolf Hilter wa Ujerumani kuteka media, magazeti, sera ya 'maendeleo ya Vitu', kubinya sauti

Adolf Hitler na CCM Mpya ilidhibiti Kuanzia redio na filamu hadi magazeti na uchapishaji, utawala wa Nazi ulidhibiti kila nyanja ya utamaduni wa Ujerumani kuanzia 1933-1945. Kupitia Wizara ya Uelimishaji na Uenezi ya Umma ya Josef Goebbels, serikali ya Ujerumani ilidhibiti kwa uthabiti ujumbe wa kisiasa, ikikuza uungu wa kiongozi huyo-Führerprinzip-na kueneza pepo kwa "adui wa rangi" anayeenea kila mahali na potovu. Maonyesho mapya katika Jumba la Makumbusho la Makumbusho ya Maangamizi ya Maangamizi ya Kiyahudi huko Washington, D.C., yanachunguza "jinsi Chama cha Nazi kilivyotumia mbinu za kisasa na vile vile teknolojia mpya na jumbe zilizoundwa kwa uangalifu ili kuwashawishi mamilioni kwa maono yake ya Ujerumani mpya." Michael C. Moynihan wa Reason.tv alitembelea pamoja na mwanahistoria na mtunza makumbusho Steve Luckert ili kujadili dhima na ufanisi wa propaganda katika kuongezeka kwa ufashisti na mafunzo gani yanaweza kutolewa kutoka kwa jaribio la Nazi la udanganyifu mkubwa

From radio and film to newspapers and publishing, the Nazi regime controlled every aspect of German culture from 1933-1945. Through Josef Goebbels' Ministry of Public Enlightenment and Propaganda, the German state tightly controlled political messaging, promoting deification of the leader—the Führerprinzip—and the demonization of the ubiquitous and duplicitious "racial enemy." A new exhibit at the United States Holocaust Memorial Museum in Washington, D.C., examines "how the Nazi Party used modern techniques as well as new technologies and carefully crafted messages to sway millions with its vision for a new Germany." Reason.tv's Michael C. Moynihan visited with museum historian and curator Steve Luckert to discuss the role and effectiveness of propaganda in the rise of fascism and what lessons can be drawn from the Nazi experiment in mass manipulation.

View: https://m.youtube.com/watch?v=Af44Slin7lg&pp=ygURTmF6aSBwcm9wYWdhbmRpc3Q%3D





Toka maktaba :
2015 5 February

Professor Nathan Stoltzfus on Hitler's Management of the Germans


View: https://m.youtube.com/watch?v=gvqKny2TQ64
On January 20, 2015 Nathan Stoltzfus delivered a lecture, "Hitler's Management of the Germans: Coercion, Compromise and the View from Washington" as part of "The U.S. in World Affairs: The Cold War and Beyond" lecture series. The lecture was followed by a discussion with Professors Konrad Jarausch and Gerhard Weinberg. The forum is organized by the Richard M. Krasno Distinguished Professorship in the Department of History and the College of Arts and Sciences, with support at UNC from the Curriculum in Peace, War and Defense, the Institute for the Arts and Humanities and UNC Global, as well as from the Triangle Institute for Security Studies and the West Triangle Chapter of the United Nations Association of the United States of America.
 
Magufuli alikua na philosophy gani?
Nitaleta maendeleo kwa Tanzania kwa njia yeyote ile, the end justifies the means, hata kama inabidi niue baadhi ya Watanzania ili kuiletea Tanzania mafanikio. Atakaetofautiana nami hayuko nasi. Na mimi ndio najua nchi yangu inahitaji nini na nani ili tuendelee. Na hata nikichukua hela za serikali, ni kwa nia nzuri kwa sababu mimi sio fisadi na sikusudii kuzitumia kifisadi. Na lazima kila mtu atii nitachosema. Usipotii wewe ni msaliti. Na wazungu wote ni maadui zetu. Matajiri wote ni mafisadi.

That was his philosophy.
 
Nakubaliana na wewe 100% kabisa. Na swali sasa ni kama Magufuli alikuwa mzalendo in the real meaning of uzalendo, au alikuwa a misconceived mzalendo ambae ali-justify yale yasiyofaa kwa kutumia excuse ya uzalendo
Magufuli alikuwa ni mlevi wa madaraka aliyejificha kwenye kichaka Cha uzalendo. Sehemu kubwa alitumia madaraka yake kukomoa wasiomsujudia. Alifanikiwa kuteka kundi kubwa la masikini waliokuwa wanapata faraja kwa kuona akiwakomoa matajari. Ogopa mzalendo anayeshurutusha kuonekana mzalendo.
 
Marehemu Mwinyi alikuwa na akili nyingi sana aliposema kila zama na kitabu chake

Wanasiasa wote wanatakiwa kujua hilo kuwa huwezi kuwa mwanasiasa wa zama zote utafika mahali hu fit zama zimebadilika ndio maana Nyerere aling'atuka baada ya kuona zama alizo haenei

Pilau ya Idd au Krisimasi iliyopita ya mwaka jana haiwezi kuwa tamu kama ya leo hata uihifadhi kwenye freezer lazima hiyo ya mwaka jana ikubali kuwa pilau mpya ni bora kuliko yenyewe iwe ilipikwa na Nyerere, Mwinyi,Kikwete au Magufuli ,babu au baba yako mzazi au Mama yako mzazi au marehemu waliotangulia au walio hai inatakiwa kusahaulika watu waangalie leo yaani present ili nchi,familia ,nk isonge mbele na maisha yasonge mbele.Maisha ni kwenda mbele kuanzia kifikra nk sio kila saa kukumbuka tu mavi ya kale ambayo hayanuki au pilau ya kale au masufuria ya Misri huko tulikokuwa watumwa wawe wa farad wakoloni nk
 
Nitaleta maendeleo kwa Tanzania kwa njia yeyote ile, the end justifies the means, hata kama inabidi niue baadhi ya Watanzania ili kuiletea Tanzania mafanikio. Atakaetofautiana nami hayuko nasi. Na mimi ndio najua nchi yangu inahitaji nini na nani ili tuendelee. Na hata nikichukua hela za serikali, ni kwa nia nzuri kwa sababu mimi sio fisadi na sikusudii kuzitumia kifisadi. Na lazima kila mtu atii nitachosema. Usipotii wewe ni msaliti. Na wazungu wote ni maadui zetu. Matajiri wote ni mafisadi.

That was his philosophy.
hayo ni maoni yako.

Hatahivyo haiondoi ukweli kwamba Wazungu ndio wachochezi wa Rushwa na Ufisadi Duniani.


Wawekezaji ni Wanyonyaji
 
Magufuli alikuwa ni mlevi wa madaraka aliyejificha kwenye kichaka Cha uzalendo. Sehemu kubwa alitumia madaraka yake kukomoa wasiomsujudia. Alifanikiwa kuteka kundi kubwa la masikini waliokuwa wanapata faraja kwa kuona akiwakomoa matajari. Ogopa mzalendo anayeshurutusha kuonekana mzalendo.
Usiwe mtumwa wa historia Kikwete aliongea mfano baba yako marehemu kama alikuwa hakujali aligoma hata kukusomesha wakati pesa alikuwa nazo mfano utamlaumu hadi lini .Pambana na hali yako wewe mtu mzima sasa achana na marehemu baba yako apambane na yeye na hali yake huko aliko
 
Your stupidity mleta mada is beyond comprehension.

Yaani Una mfananisha Magufuli na Hitler hivi una uelewa hata wa iota wa hizo Jews concentration camps ambapo kuna ushuhuda wa maandishi ya wasalia na vizazivyao.

Unamjua hata Henrich Himmler, una ujinga wa kiasi gani kufananisha shida walizopitia Jews through NAZi watu wamefungiwa na kunyimwa chakula kwa miezi na kuuliwa kama vile sisimizi na maiti kutupwq kwenye matanuru ya moto hadi kujaa mafuta ya binadamu.

Una akili timamu kweli kufananisha ukatili wa NAZI na nchi nyingine yoyote in the 20/21 century.

Unaweza kutaka kwa ushahidi hata mmoja alieuliwa kwa baraka za Magufuli; how stupid are you.
 
hayo ni maoni yako.

Hatahivyo haiondoi ukweli kwamba Wazungu ndio wachochezi wa Rushwa na Ufisadi Duniani.


Wawekezaji ni Wanyonyaji
Okay, umeniuliza swali kuhusu maoni yangu juu ya philosophy ya Magufuli halafu unaniambia hayo ni maoni yangu. Sasa ulitaka nikupe maoni ya nani? Kwani philosophy ya Hitler unafikiri ni Hitler aliitaja?

Labda niambie wewe basi, Magufuli alikuwa na philosophy gani?
 
Your stupidity mleta mada is beyond comprehension.

Yaani Una mfananisha Magufuli na Hitler hivi una uelewa hata wa iota wa hizo Jews concentration camps ambapo kuna ushuhuda wa maandishi ya wasalia na vizazivyao.

Unamjua hata Henrich Himmler, una ujinga wa kiasi gani kufananisha shida walizopitia Jews through NAZi watu wamefungiwa na kunyimwa chakula kwa miezi na kuuliwa kama vile sisimizi na maiti kutupwq kwenye matanuru ya moto hadi kujaa mafuta ya binadamu.

Una akili timamu kweli kufananisha ukatili wa NAZI na nchi nyingine yoyote in the 20/21 century.

Unaweza kutaka kwa ushahidi hata mmoja alieuliwa kwa baraka za Magufuli; how stupid are you.
Una kila dalili za mtu ambae hajasoma. Katika context, naweza kumlinganisha Messi na mtoto mcheza cha ndimu mtaani kwetu, lakini wewe hutaelewa hilo
 
Tunajua wengi wa wanaotaka Hayat Rais asahaulike, ni Wazungu, Waarabu na Wahindi....na vibaraka wa Mabeberu.

Leo Idd tunaona wamerudi ulingoni kuhamasisha Umma uwakumbatie Mafisadi ya Nchi hii.
 
Sidhani kama kuna Mtanzania ambae hajui mazuri ya Magufuli akiwa raisi wa Tanzania, atapinga kwamba Magufuli hakuwa na roho ya uzalendo kwa Tanzania, alichukia ufisadi, alichukia watu ambao anawaona walikwamisha bidii zake za kuindeleza Tanzania. Hakuna Mtazania atakaepinga kwamba Magufuli alikuwa mchapa kazi kweli kweli, mwenye kupenda nchi yake na raia wa Tanzania, mzalendo namba moja.

Lakini hilo linakukumbusha nini?

Linatukumbusha kiongozi aliewahi kuwa na hulka ya Magufuli pale Germany, Adolf Hitler. Hitler alikuwa mzalendo kweli kweli. Alisimamia Germany na kuifanya Germany kuwa taifa lenye uchumi wenye nguvu kuliko mataifa yote. Alipenda uzalendo, alichukia ufisadi na usaliti dhidi ya nchi yake. Hitler alikuwa muasisi wa gari za VW, Volks Wagen (People's Car) ili kila raia wa Germany aweze kumudu kuwa na gari. Hakuna kiongozi katika Germany anaeweza kusemwa alileta maendeleo kwa nchi yake kama alivyofanya Hitler, mzalendo namba moja wa nchi yake.

Lakini sasa, nani leo unamsikia akimsifia Hitler kwa makubwa aliyoifanyia Germany? Hakuna, kwa sababu hakuna mtu aliyesahau machungu yaliyosababishwa na Hitler.

Hakuna mtu hapa Tanzania asiyejua machungu yaliyoletwa na Magufuli katika azma yake ya kuiendeleza Tanzania, machungu ambayo hayana utetezi hata uyaangalie kwa mtazamo upi. Hayana justification.

Hata hivyo, kwa tulio hai, kuwachukia Hitler au Magufuli, ambao tayari wamekufa, ni dalili kwamba tuna matatizo ya afya ya akili, tunahitaji psychiatric help. Kuwasifia pia ni tatizo, kwa sababu tunaumiza wale walioumizwa nao, ambao bado wapo hai pamoja nasi. Tutapanda gari za VW za Hitler, tutapita kwenye flyover za Magufuli, lakini hatutaimba sifa zao.

Kama Germany ilivyoamua kumsahau Hitler pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yake, Tanzania tunapaswa kumsahau Magufuli pamoja na mazuri aliyoifanyia nchi yetu.

Tuangalie mbele sasa. Tusahau yaliyopita, tuachane na kulinganisha uongozi wa sasa na uliopita. Tuvunje magenge. Tuanze upya.

The world and your country need YOU now, not Hitler, not Magufuli.
Human being don't understand logic, reasons, mouth narration but how you touch them instinctively and our own intuition make us to understand what are you doing to us.
Don't try to control nature my friend.
Kwani wakiwa wanamsifia wanakuja kukuambia ama kila wanaloongea wajerumani hata saivi mtu yupo ndani na beibi wake wanakulana wanaongea about their hero basi unanasa sauti zao .
Pia miaka mingapi imepita tokea Hitler afariki.

Kama kuua mbona Kama mafisadi ndio wanaoua kuliko anayeua anayemuingilia anayejenga Taifa lake.
Ama nikuambie mafisadi wanavyoua na Tena wanaua wengi taratibu mno na kwa muda mrefu sema ni indirect huwezi ona na ndio Mana huko china mla rushwa bro anauliwa na sahihi kabisa auliwe yaani angekuwa anakatwa kwanza kiungo kimoja kimoja mpaka afe.
Sema Sheria za nchi hii kama Kuna mtu mmoja anaamua kuwa ziwe anavyopenda anavyoona kuwa zitambeba. Hivi tukisema kila mwenye Mali aonyeshe alivyozipata na alilipia wapi mapato na kipato chake aliwezaje kuwekeza Mali ikakua ndio ujue watu wanakula jasho la watu na wao wanakufa ama wanauliwa wanaporwa jasho lako.

Mafisadi na viongozi wote Wanaojua kuwa wameuza Mali za watanzania kwa manufaa yao Bali sio Tanzania wanawauaje watanzania zaidi kuliko ambao wameuliwa na jpm ama Hitler.

1- Tafuta data za wamama wajazito waliojifungua huko vijijini wakakosa dawa, huduma nzuri ya dawa na kidaktari Mana dawa zinapigwa/hazinunuliwi na madaktari hawawekewi mazingira rafiki wao wakae huko ili wawahudumie walipa Kodi. Tafuta vijiji vyote Tanzania ujue ni wangapi wanaofariki wakati wa kujifungua ndio uje kuongea ujanja wako hapa

2- Tafuta ni akina mama wangapi wanaofariki njiani wakipelekwa hospital kubwa Ila hakuna ambulance, zinaharibika njiani kisa roads mbaya. Tafuta ujue data zao na sio kuleta mambo Kama ushabiki tu ama huna kazi sema hujui tu Hawa mafisadi na baadhi ya vizee vilivyotuuzia nchi yetu.

3- Tafuta walimu wa physics and mathematics ratio to students iko ngapi kwa shule nzima Tanzania. Watoto wapo alfu mbili mwalimu mmoja wa maths na physics hakuna na hili suala ni la mzungu ama tubinafsishe.
Watoto wanaofeli kisa hakuna walimu wazuri baadaye Hawa watt wanaishia kuwa wadangaji, Malaya, vibaka, vibarua, Wala dawa za kulevya ili kupunguza machungu ya maisha yao, watt wanapata magonjwa na mimba Mana maisha hata ya kusoma sio rafiki kwao wangesoma angalau akapambana akawa nesi, mwalimu, nk.
Tafuta ujue haya madhara mpaka kifo vijana wanaanza kuwa vibaka Mana maisha ni makali shule hakuna , vibarua hakuna shule wanafeli Mana walimu hawapo , vitabu na mazingira mazuri ya masomo ya maabara .

3-Tafuta namba ujue ni watu wangapi vifaa ama Mali zao ama biashara zao zinaharibika kisa Kuna umeme wa kifurushi. Vijana wanashindwa kujiajiri huko vijijini kisa umeme wa uhakika na ndio Mana jpm aka African Hitler alitaka umeme wa uhakika saivi bwawa limewashinda maji yamefunguliwa yameua watu 35 huko rufiji haya sio mauaji ya binadamu Kama huyo mmewe aliyeuwa. Nikuulize ivi kweli jpm angekuwepo haya mauaji yangetokea huko rufiji. Uelewe watu wameshapiga zao mradi sio Kama enzi za marehemu. Unajua ni kiasi gani dizaini imechenji hata kwa sgr mahala palipotakiwa pawekwe nguzo kisa Kuna mkondo mkubwa wa maji saivi wanajaza kifusi mlima na huku ilitakiwa nguzo za zege train ipite juu.

4- Unajua ni vijana wangapi hawapati ajira kisa tu hawana mtu kwenye system wa wakulima wanabakia wengine kubeba unga ama kuwa wadangaji na kufanya kazi ambazo ni risk kwao unajua ni wangapi hapa wanaokufa.

5- Unajua wakulima wangapi wanashindwa kusafirisha mazao yao kisa tu barabara mbovu yanaozea shambani.
Naweza nikaendelea na list ni ndefu

Ngoja kwanza nisaini hapa mktaba wa bilioni 75 tukodi software ya kunijuza umeme Kama umekatika kutoka India. Yaani hii Ni hela tu ya kukodi software huko tanesco waza ni wanafunzi wangapi wanakaa chini na wapo madarasa ya udongo ambao wanaweza wakaangukiwa .
Kuna shule hapa hapa mwanza mjini watoto wanakaa chini, hakuna Hitler wa kuweza kutoa sauti kuwa watoto wasikae chinim darasa moja watoto Mia moja unaona haya ndio Yana akili.

Haya bana ulitaka demokrasia umeipata Mana Simba wa yuda hayupo saivi hakuna uwoga. Hamjamaliza kusafisha mitambo Mana ilikuwa inawaka ikiwa mibovu watu waliogopa kutumbuliwa.

Ngoja nipige tour kucheki mito ikoje na kina chake na helicopter baadaye nijiandikie pdm na hela ya kukodi helicopter ni ndefu Bora ingenunua dawa.

Sawa mvua zimesnyesha zimeharibu mitambo.
Treni ya moro to dar sgr inasubiria Nini ama tuna refurbish vichwa ili tupige Cha juu. Kumpa mtu uongozi mwenye kuwaza chakula na ni masikini Ni sawa na kumpa Bora mzungu na Ni Bora apewe masikini ambaye ana Nia ya kuinyanyua nchi like sokoine, NYERERE ama Mandela. Unadhani hao akina NYERERE angekuwa Kama huyo mjanja wenu unadhani mngekuwaje
 
Back
Top Bottom