Watanzania tujiulize: Ikiwa sisi ndiyo wenye mali, nini kinatukimbiza nje kutafuta wa kuja kuzila (eti kuwekeza)?

Watanzania tujiulize: Ikiwa sisi ndiyo wenye mali, nini kinatukimbiza nje kutafuta wa kuja kuzila (eti kuwekeza)?

Kididimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2016
Posts
4,153
Reaction score
3,800
Watanzania wenzangu, kuna kitu hakiko sawa!

Tutachanganyiwa lugha zote kuwa tunafungua nchi kumbe kuna hila ndani yake.

Sikubaliani kabisa viongozi kuzunguka dunia nzima kuomba pesa na uwekezaji.
Tunajidhalilisha!

Tuna bunge, Mawaziri, Wasomi, Wanasiasa, Wafanyabiashara maarufu nk, tumeshindwa kutulia na kukipanga hata iwe miaka 100 ijayo tukaijenga nchi yetu wenyewe? Hiyo haraka ni ya nini?

Wazee wetu kina Warioba, Msekwa, Malecela, Msuya nk niwaulize, mmekubali wajukuu zenu na elimu zao kuwa manamba wa Wazungu? Ndivyo hivyo Mwl. Nyerere aliwausia? Vijana,wajukuu zenu serikali iliwasomesha hadi vyuo vikuu ili wawe ombaomba duniani? Au waendesha bodaboda tuu na siyo kusimamia rasilimali zetu?

Ni kwa nini kila Rais aingiapo tunaruhusu alete mambo yake mapya na siyo kuendeleza ya mtangulizi au yaliyoasisiwa na nyie wazee wetu?

Mwl. Nyerere alituachia rasilimali tuzitumie kujiletea maendeleo au kuzinadia duniani?

Tujitizame.
 
Pimia hapo Chididimo tu mkuu nyinyi ni matajiri wa ng'ombe lakini bila kutoka hapo mkaenda hata ZUZU tu hamta kunywa chai wala hamta vaa.kwani vitu hivyo na zaidi vinapatikana Kuanzia Zuzu, majengo. au One way.
 
Muulize yeye kazalisha nini na kaweza kukiuza hata kwenye soko moja la kimataifa? Alilipa kodi shs ngapi na ameajiri watu wangapi?

Akikujibu nitagg
Huyu jamaa sijui kawaza nini, azalishe nini mkuu kazi kushindana kuongeza matembe na kutazama mikia ya ng'ombe tu
 
Tunakimbizana na maisha bwashee. Inawezekana we umesukumwa na ubinafsi tu kuandika haya lakini kumbuka watanzania Ni wengi maskini wanatafuta ajira. Laiti ajira au serikali ingekuwa na uwezo wa ku accommodate watanzani wote hakuna haja ya uwekezaji kutoka nje lakini ujue hata marekani ndani kwao Kuna wawekezaji wengi kutoka china, urusi n.k. Hivyo siku nyingine ficha ujinga wako
 
Tunakimbizana na maisha bwashee. Inawezekana we umesukumwa na ubinafsi tu kuandika haya lakini kumbuka watanzania Ni wengi maskini wanatafuta ajira. Laiti ajira au serikali ingekuwa na uwezo wa ku accommodate watanzani wote hakuna haja ya uwekezaji kutoka nje lakini ujue hata marekani ndani kwao Kuna wawekezaji wengi kutoka china, urusi n.k. Hivyo siku nyingine ficha ujinga wako
Nini maana ya "Ajira". Tueleze tafadhali.
 
Kwanza Tanzania hatuna rasilimali za thamani kama tunavyoaminishana utasikia eti tuna mito, mabwawa, ardhi, madini, wanyama pori, maziwa ni rasilimali sawa ila hazina thamani kama tunavyoaminishana.
 
Hebu na wewe jiulize jambo moja tu:-

Assume leo hii dunia YOTE inasusia Dhahabu na Tanzanite kutoka Tanzania na bidhaa zake. Pamoja na hayo, wewe ndo unakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Je, kama taifa, dhahabu na tanzanite yetu tutaitumia kwa matumizi yapi?
 
Hata we tofautisha kuzila na kuwekza. Wakiwekeza we ndo unakula na wao pia. Na inafanyika hivyo kwa sababu huna uwezo wa kuwekeza. Mpaka hapo ulipo sidhani hata laki Kama unayo
Tumezuia "Vipaji" tunaenda kuvitafuta nje, hivyo siyo vyetu!!!! Tusijidanganye. Viongozi wanaokotezana kindugu wanadanganyana kutafuta" mjomba feki" kuwa atawasaidia, huyo mjomba ni mjinga? Hatusomi Historia? China,Vietnam,Indonesia,Malaysia,Brazil kwa uchache waliwezaje? Vijana wenye uelewa wapo, tujenge maono ya mbele tuwawezeshe kwanza Hawa. " The time is coming when all stupid minds will be uprooted,and the facts open " Haiwezekani Wazazi wetu watuachie mali tutapanye kwa kukosa maarifa! Hilo nalikataa.
 
Kujisahihisha ni muhimu la sivyo ni kusubili aibu. CCM inafanya makosa makubwa sana kwa kuendeshwa na serikali na kufanya kazi ya chama kuonekana rahisi sana. Serikalini watumishi hawaaminiki maana na wenyewe wamekandamizwa na mfuma mbovu pamoja na masilahi kiduchu.

Tanzania ina kila kitu ikiwemo mitaji ya kutosha tatizo viongozi wakuu hawajaamua au hawajui la kufanya. Muda ni sasa visingizio hatutaki amkeni tuanze kijenga nchi aibu ya umaskini jamani inatosha.
 
Back
Top Bottom