Watanzania tujiulize: Ikiwa sisi ndiyo wenye mali, nini kinatukimbiza nje kutafuta wa kuja kuzila (eti kuwekeza)?

Watanzania tujiulize: Ikiwa sisi ndiyo wenye mali, nini kinatukimbiza nje kutafuta wa kuja kuzila (eti kuwekeza)?

Contents za subject matter unayojaribu kuadress ni bayana,lakini"Approach" yetu Ina kizungumkuti. Bado nasisitiza"Tujipime" tukae tupange tunachohitaji kama nchi,kabla ya"kufukuzia" kama ulivyosema fursa za wawekezaji na uwekezaji. Haraka ya nini? Tumepata Uhuru miaka 60 plus iliyopota,hatukujua population ya watu inaongezeka,leo tukurupuke hatuna madawati au madarasa? Na je,tutakopea vingapi endapo hata chaki ya mwalimu ni ya mkopo?
Juzi hapa,Mama yetu kaleta fedha za madarasa na madawati,umeona ilivyotumika nguvu kubwa kutetea hoja yake kwa wananchi! Wananchi wanasema nchi imejaa misitu kedekede ya kutengeneza madawati,leo wanaingizwa madeni kwa kofia ya Covid-19bila sababu za msingi!!!.
Unapomleta mwekezaji wa nje kwenye nchi,unatengeneza ajira 10,unavuruga 100 na za kudumu endapo kazi hiyo ingefanywa na sie wenyewe. Hilo liko wazi na mifano ipo!! Sera zetu za fedha hasa za mikopo ya nje haziko bayana!! Kila kiongozi anatumia "approach" tofauti hasa kujikwezea na kuunda"minorities" wa kumsemea , hapa Ina walakini. Mara nyingi imeonekana kwa nchi nyingi manufaa yake hayawezi kukuza uchumi ndani ya muda muafaka,pale mkopo unapolenga huduma za kijamii,. Kwani muda wa kurejeshwa tungeacha haraka,kwa nguvu za wananchi na "rasilimali "zilizopo hiyo kazi ingekuwa imeisha bila kuiminya jamii kufaidisha wageni.
Nina maono makubwa na Nchi yangu,tusijione wanyonge,na tusijidekeze,tunaweza. Kumchukua Mwarabu Oman kuja kuwekeza kilimo cha Zabibu ni fedheha kwa Taifa!
Nimetumia lugha nyepesi nieleweke.
Kumbe 'umezama' kidogo kuliko nilivyotegemea niliposoma mada yako huko ukurasa wa kwanza?

Heshima mkuu.

Lakini sidhani kwamba mkuu 'chige' ataweza kukuelewa kwa haya uliyoweka hapa. Huyu kapofushwa na usakaji wa u'oligarch'wa kiTanzania.
 
Hivi kweli kuna sababu yeyote ya Tanzania kuagiza mafuta ya kula na vyakula vya nafaka kama mchele au sukari? TBL na viwanda vingine vya bia nasikia wanatumia billions kuagiza ngano/shayiri za kutengeneza bia kila mwaka wakati tuna maelfu ya eka zilizojaa rutuba na vijana wasio na kazi? hii ni laana sio aibu tena
 
I wish jf wangeweka kitufe cha likes 1000

Jibu Bora zaidi kwa mtoa mada
Pole yako kama unafikiri hilo ndilo "Jibu Bora zaidi kwa mtoa mada".

Inaelekea huelewi alichoandika mleta mada. Lakini, hapana. Nakufahamu vyema kwa michango yako humu JF kuhusu mambo kama haya.

Totally brainwashed to the extent that the mind has no capacity to think of alternatives to what is programmed; more like a robot of sorts.
 
Hivi kweli kuna sababu yeyote ya Tanzania kuagiza mafuta ya kula na vyakula vya nafaka kama mchele au sukari? TBL na viwanda vingine vya bia nasikia wanatumia billions kuagiza ngano/shayiri za kutengeneza bia kila mwaka wakati tuna maelfu ya eka zilizojaa rutuba na vijana wasio na kazi? hii ni laana sio aibu tena
Muulize chige, au Lord maswali yako haya mazuri.

Wao wanachojuwa ni kwamba lazima uwekezaji wa mabilioni kwenye magesi na mafuta, na hata kilimo cha aina hiyo ndivyo vitakavyowezesha Tanzania kuendelea; na kwa vile hakuna mwenye uwezo wa mabilioni Tanzania, ni lazima uwekezaji utoke nje ya nchi. Vinginevyo, tusahau kabisa kuwa Tanzania itaendelea!

Mawazo ya ajabu kabisa haya!
 
Mtaji hamnao, mlichonacho ni maneno na blaa blaa tu
Hakuna mfanya biashara mwenye mtaji; mitaji hutolewa na mabenki. Kwa nini tusitumie mabenki kupata mitaji hiyo? Tatizo letu ni ujinga wa kutokujua la kufanya, tunategemea wengine ndio watufanyie tupate vya ulaini. Wakati Botswana wanabadilisha maisha yao kwa kutumia raslimali zao hawakuwa na mitaji, bali ni sera zao tu ndio ziliwabadilisha.

Nyuma kidogo wakati wa utawala wa Mkapa na Kikwete kuna mhindi mmoja alitukana watanzania kuwa ni wajinga, Akadai kuwa yeye alikuja Tanzania bila hela ila alikuwa na akili na ndiyo maana akawa tajiri kwa muda mfupi sana. Nadhani mhindi huyo alifukuzwa lakini alitupa za usoni mwetu. Kila mara tunatafuta visababu vya kuhalalisha kushindwa kwetu.
 
Watanzania wenzangu, kuna kitu hakiko sawa!

Tutachanganyiwa lugha zote kuwa tunafungua nchi kumbe kuna hila ndani yake.

Sikubaliani kabisa viongozi kuzunguka dunia nzima kuomba pesa na uwekezaji.
Tunajidhalilisha!

Tuna bunge, Mawaziri, Wasomi, Wanasiasa, Wafanyabiashara maarufu nk, tumeshindwa kutulia na kukipanga hata iwe miaka 100 ijayo tukaijenga nchi yetu wenyewe? Hiyo haraka ni ya nini?

Wazee wetu kina Warioba, Msekwa, Malecela, Msuya nk niwaulize, mmekubali wajukuu zenu na elimu zao kuwa manamba wa Wazungu? Ndivyo hivyo Mwl. Nyerere aliwausia? Vijana,wajukuu zenu serikali iliwasomesha hadi vyuo vikuu ili wawe ombaomba duniani? Au waendesha bodaboda tuu na siyo kusimamia rasilimali zetu?

Ni kwa nini kila Rais aingiapo tunaruhusu alete mambo yake mapya na siyo kuendeleza ya mtangulizi au yaliyoasisiwa na nyie wazee wetu?

Mwl. Nyerere alituachia rasilimali tuzitumie kujiletea maendeleo au kuzinadia duniani?

Tujitizame.
Kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza!!
 
Hakuna mfanya biashara mwenye mtaji; mitaji hutolewa na mabenki. Kwa nini tusitumie mabenki kupata mitaji hiyo? Tatizo letu ni ujinga wa kutokujua la kufanya, tunategemea wengine ndio watufanyie tupate vya ulaini. Wakati Botswana wanabadilisha maisha yao kwa kutumia raslimali zao hawakuwa na mitaji, bali ni sera zao tu ndio ziliwabadilisha.

Nyuma kidogo wakati wa utawala wa Mkapa na Kikwete kuna mhindi mmoja alitukana watanzania kuwa ni wajinga, Akadai kuwa yeye alikuja Tanzania bila hela ila alikuwa na akili na ndiyo maana akawa tajiri kwa muda mfupi sana. Nadhani mhindi huyo alifukuzwa lakini alitupa za usoni mwetu. Kila mara tunatafuta visababu vya kuhalalisha kushindwa kwetu.
Na maandishi rahisi kama haya bado baadhi ya watu hawawezi au hawataki kuyaelewa.

Wahindi toka India waliletwa Afrika Mashariki na Waingereza kujenga reli. Walipokuja hawakuwa na mtaji wowote, lakini Upanga yote ile na hata Mzizima kwenyewe ndio wakawa wa kujenga maghorofa, kwa mikopo ya benki.

Haya, tukubali kwa wakati ule elimu ya watu wetu ilikuwa chini sana kuweza kusimamia mikopo ya aina ile,... lakini tukubali kuwa hata baada ya miaka 60 ya uhuru bado hatuna watu wanaoweza kukopesheka na kuitumia mikopo hiyo kuijenga Tanzania?

Mwalimu Nyerere alipokuwa akisema maendeleo yanahitaji "WATU, ARDHI na UONGOZI BORA", hatukuweza kuelewa maana yake ni nini?
 
Na maandishi rahisi kama haya bado baadhi ya watu hawawezi au hawataki kuyaelewa.

Wahindi toka India waliletwa Afrika Mashariki na Waingereza kujenga reli. Walipokuja hawakuwa na mtaji wowote, lakini Upanga yote ile na hata Mzizima kwenyewe ndio wakawa wa kujenga maghorofa, kwa mikopo ya benki.

Haya, tukubali kwa wakati ule elimu ya watu wetu ilikuwa chini sana kuweza kusimamia mikopo ya aina ile,... lakini tukubali kuwa hata baada ya miaka 60 ya uhuru bado hatuna watu wanaoweza kukopesheka na kuitumia mikopo hiyo kuijenga Tanzania?

Mwalimu Nyerere alipokuwa akisema maendeleo yanahitaji "WATU, ARDHI na UONGOZI BORA", hatukuweza kuelewa maana yake ni nini?
Mbona huyo Nyerere alishindwa kuleta maendeleo miaka yote aliyokuwa madarakani? Kang'atuka kaicha nchi hoi. Kuhusu Wahindi na mafanikio yao, msikilize huyu hapa wa Uganda lakini alichoongea kinahusu hata Tanzania

 
Mtaji hamnao, mlichonacho ni maneno na blaa blaa tu
Tatizo sio mitaji,maana kama ingekuwa ni hizo mitaji hizo trillion tunazokopa zingetoshea kuanzia. Tatizo kubwa la viongozi wetu lipo kwenye FIKRA. Wengi wao ni vipofu, maana fursa au pesa huonwa kwa macho ya fikra.
 
Mbona huyo Nyerere alishindwa kuleta maendeleo miaka yote aliyokuwa madarakani? Kang'atuka kaicha nchi hoi. Kuhusu Wahindi na mafanikio yao, msikilize huyu hapa wa Uganda lakini alichoongea kinahusu hata Tanzania


Ulitaka alete 'internet' ndipo ujue kwamba nchi inaendelea? Au ulitaka aache mabilionea kumi na makabwera milioni 20 ndipo ujue kwamba nchi inaendelea?
Hukuona shule na huduma za afya zilivyopanuka. Hukuona hali ya maisha ya watu ilivyokuwa inabadilika toka ilivyokuwa enzi za ukoloni?

Wewe hata kuelewa 'concept' ya nchi kuendelea huijui?
 
Ulitaka alete 'internet' ndipo ujue kwamba nchi inaendelea? Au ulitaka aache mabilionea kumi na makabwera milioni 20 ndipo ujue kwamba nchi inaendelea?
Hukuona shule na huduma za afya zilivyopanuka. Hukuona hali ya maisha ya watu ilivyokuwa inabadilika toka ilivyokuwa enzi za ukoloni?

Wewe hata kuelewa 'concept' ya nchi kuendelea huijui?
Yaani shule na hospitali tulizoachiwa na wakoloni au zilizojengwa na makanisa unataka kumpa sifa Nyerere kama kazileta yeye? Huyo Nyerere mwenyewe alisomeshwa na mkoloni. Halafu nchi kuwa na mabilionea siyo dhambi kama wameipata hela yao kwa nguvu na jasho lao. Mabilionea wanatoa ajira, wanawekeza, na wakiweka hela zao kwenye mabenki yetu zitazunguka ndani ya uchumi wetu. Makabwera walikuwepo hata enzi za Nyerere tena walichoka sana.
 
Back
Top Bottom