adriz
JF-Expert Member
- Sep 2, 2017
- 12,207
- 26,521
Kwa masikitiko makubwa niende moja kwa moja.
Watanzania wengi hatuelewi na hatujapata bado ufafanuzi sababu zinazopelekea Vifurushi vya Internet kupanda mara kwa mara tena kwa ghafla miezi michache tokea Rais Samia achukie madaraka.
Alianza kuupiga mwingi hadi tukawa tunajifia mitandao kwa kuongoza kwa unafuu wa gharama za internet kipindi Gb1 unapata kwa Tsh1,000/= lakini ghalfa zikaanza kupanda kwa awamu hatimaye leo awamu ya tatu kupanda tokea awe madarakani(kama sikosei) nimekuta Tsh3,000/= mtu unapata Gb 1.5 na mitandao yote vifurushi viko bei ghali kuliko vilivyokuwa ghali awali.
Athari nilizoziona kutokana tokea hali hii ilivyoanza miezi iliyopita na kuongezeka sasa;
1. Kuongezeka wimbi la watu wanaotumia njia haramu za kupata bando za bure mfano Free VPN.
Huko Telegram nimechunguza nimekuta magroup maalumu kwa akji ya watu kupeana hayo maujanja ili kuendana na ukali wa hali hata mitaani na hapa Jf ukiwa na connection ya VpN ya free data watu kibao wanakufuata Pm na wengine wapo radhi kukuchangia chochote kitu hivyo inachangia mapato ya serikali kupotea kwa asilimia kubwa.
2. Kupungua Idadi ya views youtube kwa asilimia kubwa na watu kukosa mapato.Hata wasanii wamepigwa za uso miezi hii na haijawahi kutokea kuwa na idadi ndogo namna hiyo kwa fanbase yao
3. Kupunguza motisha ya watu kusaka maarifa mtandaoni. Mimi nilikuwa ninachanel zangu maalumu za kufuatilia makala maalumu na mada za kisanyansi, kihistoria nk huko YouTube lakini nina miezi YouTube naiogopa kwenye simu yangu na naipitia ili nibaki kuperuzi angalau JF.
4. Ongezeeni wana JF....
#UziTayari
Watanzania wengi hatuelewi na hatujapata bado ufafanuzi sababu zinazopelekea Vifurushi vya Internet kupanda mara kwa mara tena kwa ghafla miezi michache tokea Rais Samia achukie madaraka.
Alianza kuupiga mwingi hadi tukawa tunajifia mitandao kwa kuongoza kwa unafuu wa gharama za internet kipindi Gb1 unapata kwa Tsh1,000/= lakini ghalfa zikaanza kupanda kwa awamu hatimaye leo awamu ya tatu kupanda tokea awe madarakani(kama sikosei) nimekuta Tsh3,000/= mtu unapata Gb 1.5 na mitandao yote vifurushi viko bei ghali kuliko vilivyokuwa ghali awali.
Athari nilizoziona kutokana tokea hali hii ilivyoanza miezi iliyopita na kuongezeka sasa;
1. Kuongezeka wimbi la watu wanaotumia njia haramu za kupata bando za bure mfano Free VPN.
Huko Telegram nimechunguza nimekuta magroup maalumu kwa akji ya watu kupeana hayo maujanja ili kuendana na ukali wa hali hata mitaani na hapa Jf ukiwa na connection ya VpN ya free data watu kibao wanakufuata Pm na wengine wapo radhi kukuchangia chochote kitu hivyo inachangia mapato ya serikali kupotea kwa asilimia kubwa.
2. Kupungua Idadi ya views youtube kwa asilimia kubwa na watu kukosa mapato.Hata wasanii wamepigwa za uso miezi hii na haijawahi kutokea kuwa na idadi ndogo namna hiyo kwa fanbase yao
3. Kupunguza motisha ya watu kusaka maarifa mtandaoni. Mimi nilikuwa ninachanel zangu maalumu za kufuatilia makala maalumu na mada za kisanyansi, kihistoria nk huko YouTube lakini nina miezi YouTube naiogopa kwenye simu yangu na naipitia ili nibaki kuperuzi angalau JF.
4. Ongezeeni wana JF....
#UziTayari