Sasa ona unakorukia, ninavyokuona unaruka ruka tu bila kuwa objective. Baada ya kukuonesha kuwa OGP is just a project kwa manufaa ya mabwanyenye, umekuja na mada nyingie ya kulinganisha Botswana na Tanzania. Hii ndiyo tunaiita ni kukosa direction au kukosa kitu cha kuongelea. Umekuja unaimba OGP, OGP unaijua OGP wewe? OGP imeanzishwa juzi juzi tu September 20, 2011.
Sasa hivi tupo na kiongozi anaweka maslahi ya Taifa mbele. Hayo masuala ya OGP na TWAWEZA ni usanii mtupu. Yaani watu wamekaa kwenye ofisi zao Dar wanapiga simu kuwauliza watu 1000 kati ya watu Milioni 50 then unaweka conclusion!!? Huu ni usanii na upuuzi wa kujipatia kipato pasipo kufanya kazi.
Nimekueleza kwa mataifa yanayojielewa na yanayopiga hatua kwa haraka. Haya mambo ya OGP ni mpango wa Mataifa ya Magharibi kurudisha nyuma juhudi za maendeleo. Nchi za ASIA zenye competition kubwa kiuchumi kwenye nchi za magaribi hazimo kwenye OGP maana ni upuuzi tu. Hizo rafiki ni Drama kama drama za akina Tundu Lissu. Hao hao akina Zitto Kabwe wanaolilia OGP kwa sababu wanamanufaa ndani yake Halmashauri yake imepata hati chafu. Huku madiwani karibia wote ni wa chama chake.
Halafu unatakiwa utambue kila nchi ipo na sheria na utaratibu wake. Huwezi kulazimisha Tanzania ifanane na USA. USA waishi kwa maisha yao na sisi tunaishi kwa maisha yetu. Halafu utambue Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa mabunge ya jumuia ya madola. Fuatilia namna ya mabunge ya jumuia ya madola yanavyoongozwa.
Mmeomba muoneshwe mikataba wewe na nani? Unadhani kila kitu kinawekwa public? Kuna taratibu zipo kama unataka kuona mikataba yenye maslahi mapana na Taifa letu. Nimekueleza kija na unatakiwa kuwa objective.
Eti ujenzi wa SGR what? fuatilia utaratibu na utaweza kuiona mikata yote.
Ujenzi wa uwanja wa ndege Chato!? lengo lako ni kutaka kumchafua rais wetu tu. Nchi imejidhatiti kujenga viwanja vya ndege kila mkoa. Chato ipo katika mkoa wa Geita. Sasa unataka watu wa Geita wasiwe na kiwanja cha ndege.
Mbona huongelei ujenzi wa kiwanja cha ndege Simiyu? Mbona huongelei Kiwanja cha Ndege Songwe? Mbona huongelei kiwanja cha Ndege Mafia, Mbona huongelei kiwanja cha ndege Kigoma?
Tanzama hii ramani. Mkoa wa Geita hakuna kiwanja chochote cha Ndege. Sasa wakitaka kujenga nyie mnapiga makelele. Mbona kuna mikoa ipo na viwanja zaidi ya kimoja wanageita hawalalamiki? Acha chuki wewe
Vijana walioishiwa fikra wanaruka ruka tu bila kuwa objective. Si ndio nyie mliwahi kumwita JK kuwa dhaifu, ndio nyie mlimwita kuwa hawezi kukemea rushwa nk. Nimesema ninyi ni wazandiki, wanafiki msio na haya mmejaa chuki, haki ya nani mtahukumiwa kwa hayo. Taifa linahitaji maendeleo, linahitaji chakula, linahitaji Amani. Taifa halihitaji OGP tangu OGP iingie mimi sijawahi kuona mantiki yake. Kuna organazation zipo nyingi tu rafiki mfano
- Transparency International
- National Democratic Institute
- International Foundation for Electoral Systems
- International Institute for Democracy and Electoral Assistance
- Freedom House
- Human Rights Watch
- Amnesty International
Yapo mengi mengi mno.