Watanzania tunazikuza sana timu za Kiarabu, hazina ubora wa kutisha kama tunavyoziongelea

Mashabiki wazuri ni wa Ihefu au sio?Mbarali mbali.
 
Uwekezaji nao ni muhimu, Imagine unachukua Striker kutoka Dortmund mshahara wa miezi sita tu unapata hela za usajili za timu za Kariakoo, kila mwaka tutakuwa tunasema tumewakosakosa lakn wenyewewanajua wanachokifanya. BTW mpira wa Tz umekuwa sana tofaut na miaka ya nyuma.
 
Ukweli mtupu.
 
Mkuu
mimi mpira sina taaluma nao sana, ila kwa takwimu kadhaa hii hoja yako nimeshaiongea sana kwa baadhi ya mashabiki wa timu zote!

Tangu simba itolewe na wydad kwa penati nikaona hawa waarabu wako overrated! Mwarabu anatakiwa awe kama raja anakupiga nje/ndani sio chini ya goli3, sasa skuizi hata tukimenyana nao tunawafunga ama draw hapo utasema ni bora sana? Tukifungwa na waarabu sasa hivi ni uzembe tuna kiwango/uthubutu/experience kuwasifu na kuwaabudu ni ujinga wa kiwango kikubwa sana!
 
Wanafungika vizuri sana
 

Alahaly unaipaje ujiko ambao haina team tumeikuta inabeba makombe huku sisi tunajikongoja… tunatamani tuwe kama wao team bora africa na duniani
 
Waarabu wanabebwa sana hawana maajab
 
Bila ushahidi ni porojo kama porojo zingine tu...
Weka vikombe vya hizo timu za tanzania na hizo za waarab kuthibitisha kuwa ziko levo moja...
Kwenye facilities huko usiingie, na kwenye bajeti usiguse kabisa... ongelea tu mafanikio ya uwanjani... unalingana nao kwa kigezo kipi mfano al ahly? Yeye kukutoa kwa jasho sio kigezo cha kusema unalingana nae, hata ktk ligi bora ulaya timu za mwisho ktk msimamo zaweza sumbua anayeongoza...
Usipotoshe watu, weka ushahidi tu bila porojo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…