Watanzania, tuuchukie ufisadi kama tunavyochukia matukio mengine. Mafisadi hawajawahi kuwa Marafiki wa Tanzania

Nehemia Kilave

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2022
Posts
1,414
Reaction score
3,118
Hisia ,chuki na mihemko vikitawala mambo mengi sana huwa hayaendi sawa.

Ripoti za CAG zinatolewa, madudu mengi yanaonekana, pesa nyingi zinaliwa na kupotea.

Kwa sasa hali ilivyo utapiga mtoto wako au ukifanya tukio ambalo ndilo linavuta hisia za wajinga wengi na welevu wachache hapo haki itatendeka huku fisadi akiachwa anadunda mitaani.

Ufisadi hauna tofauti na uuaji, unyanyasaji na ulawiti.

Watu wanakufa sababu ya mpumbavu mmoja asiyejali maisha ya watu na kuwa na utu kakwapua ma bilioni.

Fisadi inatakiwa aimbwe kila sehemu, meme kila sehemu na achukiwe popote atakapo onekana.

CHADEMA ya Slaa walikuja na list of SHAME pale Mwembeyanga ndivyo inavyotakiwa .​
 
ilisaidia nini hiyo list of shame, na hiyo chuki kwa mafisadi itasaidia nini wananchi, bila kuja na mawazo mapya na fikra mbdala kuukomesha huo ufisadi πŸ’
 
Mafisadi ndiyo wameshika usukani wa nyanja zote zauongozi wa nchi, labda useme tuikatae CCM maana ndiyo inawafuga mafisadi.
 
CAG alitoa ripoti ya ufisadi wizara nyingi TU! Maza akaishia kusema stupid! Ikaisha hivyo! Hii nchi ni ya hovyo sana!
 
aulizwe makamu mwenyekiti taifa Chadema, wakati fulani alipiga mayowe ya nguvu mno haijulikani aliona nini kule ndrani ndrani kabisaa Chadema πŸ’
Au Yale majizi mapapa yenye rangi ya majani mabichi ,,yanaweyo weka fedha nje ya nchi ,Yale yanayotuma watot wao kua wageni rasmi na kutoa michango ya Malaki ya ela wakat ni watot wadogo wanao soma
 
Au Yale majizi mapapa yenye rangi ya majani mabichi ,,yanaweyo weka fedha nje ya nchi ,Yale yanayotuma watot wao kua wageni rasmi na kutoa michango ya Malaki ya ela wakat ni watot wadogo wanao soma
si wanefundishwa ukarimu na kujitolea.

ubahili haujawahi kumsaidia mchoyo kwa chachote πŸ’
 
Mleta mada;
Umewahi kusikia kiongozi yeyote ndani ya CCM ya sasa akikemea Ufisadi?
Umewahi kusikia kuna yeyoyote mla rushwa/ fisadi kapelekwa mahakamani?
Umewahi kusikia zile reports za CAG kama kuna yeyote aliyechukuliwa hatua?
Sasa hapo ujue kinachoendelea ktk nchi yako
 
Ilisadia lowassa-RIP kutoingia madarakani
kwahivyo waliotajwa kwenye list of shame hawako madarakani na wala hayati EGLowasa hakuwako madarakani right?

Gentleman,
hiyo list of shame ilitajwa mwaka gani, ili kuweka kumbukumbi sawa kwa faida ya wadau?πŸ’
 
Hata kusumbua waomba kazi kuja mpaka Geita pale Wajja Hospital kwa Interview feki wakati tayari mna mtu wenu mdada ambaye mlimwambia aje saa 6 mchana wakati wengine mliwaambia waje saa 2 asubuhi nao ni UFISADI na UTAPELI kama huo mwingine tu,shame on you all Wajja Hospital
 
ilisaidia nini hiyo list of shame, na hiyo chuki kwa mafisadi itasaidia nini wananchi, bila kuja na mawazo mapya na fikra mbdala kuukomesha huo ufisadi πŸ’
Ningeshangaa Sana Fisadi Sr usitokee kupambania squad yakoπŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…