Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!

Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!

H

Hapo mwanaume "kichwa cha nchi" inategemea ni jamii gani - patrilineal au matrilinear . Ukienda kwenye matrilineal societies, hicho "kichwa cha nchi hakionekani". Nimekaa kwenye matrilinear society miaka 8, angalau nina uzoefu huo. Mwanaume, mfano, among the Chewa ni 'ceremonial' hana mamlaka kwa watoto, hata kwa mkewe. Hata mtoto akitaka kuolewa au kuoa si yeye anayetoa idhini. Na pia anayeamua nani atoke nyumbani akaishi anakotaka (kati ya mwanaume na mwanamke) ni mwanamke, na si mwanaume. In fact, mwanamke ndiye anayemfulumusha mwanaume kwa kumwambia "Toka hapa nyumbani, rudi kwenu" au "katafute sehemu nyingine ya kuishi. Sikutaki." Sasa hapo kichwa cha nchi ni nani, anayefulumushwa (asiye na mamlaka) au anayebaki nyumbani (mwenye mamlaka)?
Mkuu nchi yetu ya Tanzania ni Patrillineal, Mwanaume ni muamuzi namba moja katika nyanja zote/Top controller 😛
 
Toka aniondolee dhulma ya loan board na kunipandisha daraja akili inaniambia Mama anafaa..

Miaka mitano iliyopita sikuwa na uhakika na nyongeza ya mshahara. Naamini Mwakani mambo yatakuwa vizuri. Cha msingi tumuombee afya,uhai,busara,hekima,utu na uzima kwa YEYE Mwenye Uwezo wa yote.
You are selfish being
 
😀Umekaribia kuelewa sasa, utakapoacha ushabiki utarudi kwenye point....Mwanaume ndiye anapaswa kuwa dereva mkuu wa nchi, Msikiti, Kanisa, Familia n.k...😎
Not necesarily, kwenye dini yes but kungine kote anything a man do, woman can do, but not everything a woman can do, a man can do!。
P
 
Mkuu nchi yetu ya Tanzania ni Patrillineal, Mwanaume ni muamuzi namba moja katika nyanja zote/Top controller 😛
nchi yetu ni secular state, haina dini, hivyo hakuna cha matrilinier wala patriarch, any gender can be a president。
P
 
Katika nchi yako Tanzania hakuna matrireneal societies?
hakuna kabisa. Mwanamke katika presedential position "NO!"...tumejikwaa hatuwezi kuendelea kuhalalisha anguko letu 😎 , Mungu ametuvusha salama katika kipindi kizito tumshukuru aliyekuwa amewekwa ili kutupitisha hapo..tunamshukuru sana, ila sasa tumefika mwisho atupishe tuendelee na taratibu zetu za kila siku ili Mungu aendelee kutupa mema kupitia Mwanamume kwenye hiyo nafasi😛
 
ila kwenye urais, sio lazima ndio awe Mama Samia, anaweza kuwa yeye au mwanamke mwingine yoyote aliyepangiwa kwasababu mpangaji sio yeye, wala sio sisi, mpangaji ni YEYE. Hivyo ikitokea, YEYE amepanga rais wa Tanzania kwa mwaka 2025 awe ni mwanamke, then rais wa Tanzania kwa mwaka 2025 atakuwa ni mwanamke, ila mwanamke huyo atakuwa ni yule aliyepangiwa na YEYE, kuwa rais wetu 2025, kama aliyepangiwa na YEYE ni yeye Mama Samia, then who are we kusema no?
Hii inasisimua sana mkuu, kama kweli YEYE akifanya kuchagua vice versa, hakika waTanzania tutabaki midomo wazi.
 
Back
Top Bottom