Watanzania tuwe makini na vyombo vya habari vya Kibeberu. CNN wazusha kukamatwa kwa Freeman Mbowe ni amri ya Rais Samia!

Wewe paskali ndio mzushi lakini Cnn inasikika dunia nzima. Hata ukipindisha na kuweka nakshi kilichosemwa cnn ndio uhalisia wa mambo. Tujisahihishe hizi sinema zina negative impact kwetu kama tunategemea utalii, FDI, mikopo na chanjo za msaada.
 
Bado haujakata tamaa na kujipendekeza? Hata ukipata kwa umri wako inabidi uanzie angau ukuu wa mkoa.
 
Unapoteza muda wakokumwelewesha. Mayala inaonekana ni low IQ, hafundishiki.
 
Nyinyi mnanufaika na huu mfumo kandamizi huku mmejificha kwenye koti la uzalendo. Ipo siku yenu tu ngoja Watanzania waamke kutoka usingizini
Wala hakuna cha kunufaika na mfumo, sisi ni watu wazima wenye akili timamu na uwezo mzuri wa kujua nini kinachoendelea. Sisi siyo nyumbu wa kwenda tu na mob psychology!
 
... Lakini ufahamu kwamba kuunga mkono mtawala wa kiimla sio uzalendo ila kumpinga ndio uzalendo.

Siku hizi kufuatia hali ngumu ya maisha kumezuka mtindo wa baadhi ya watu kushabikia vitendo vya kibabe na kihuni wanavyofanyiwa wapinzani wakifikiri kwamba kwa kufanya hivyo watakumbukwa katika teuzi mbalimbali zinazofanywa na mtawala.
 
Huyo profesa ni mjinga mno....

Nchi ina vyombo vya ulinzi na usalama ,yeye alipata habari za ushahidi kutoka wapi kuwa amri hiyo imetoka kwa mh.Rais wetu?!!!

Si kila wanachokiongea kina ukweli....
Kuna possibility ya 200% wewe ndiye uliye mjinga na siyo huyo Profesa...

Kama wewe huwezi kupata habari (inside Infos) usifikiri kuwa wengine hawawezi pia...!

Unadhani wote serikalini wanapenda ujinga huu Wa kuonea na kubambikizia makosa na kesi watu unaoendelea...?

Unadhani hakuna insiders wa ndani serikali wanaoweza kununulika na kuvujisha inside infos kama hizi..?

Kama serikali inaweza kununua wanasiasa wa upinzani kwa pesa, basi hata yenyewe inaweza kununuliwa pia...!
 
Kumtiii rais ndio uzalendo [emoji1]

Hata Kama rais analeta taharuki.

Hapa bongo raisi MUNGU-mtu.

Uzalendo Ni kumpinga hata rais alieye madaraka Kama amri zake zinaleta mpasuko na taharuki kwenye jamii .

Uzalendo Ni kupigania nchi na nchi sio rais Bali wananchi.

Uzalendo sio kuimba wimbo wa Taifa ukiwa umepiga saluti huu sio uzalendo.

Uzalendo Ni kupambana na maadui wa ndani na nje hata Kama wamekalia kiti Cha uongozi ikiwa wanatoka nje ya msingi ya utawala Bora na kushindwa kupigania maslahinya Taifa .

Bongo uzalendo Ni kutii amri bila shuruti[emoji1]hata Kama amri hi ni batili inatoka kinywani mwa dhalimu.

Hii nchi sometime inachosha kwa kweli

Sent from my kombola using ramli JamiiForums mobile app
 
Ni sisi wapinzani wenyewe tutaweza kujitetea, kwa sasa ccm wamepoteza ushawishi kwa umma, hivyo wamejihika na vyombo vya dola ili kuendelea kututawala kwa shuruti. Namna pekee ni sisi wapinzani kugoma kushirikiana na wanaccm.

Hakina kushiriki msiba wala sherehe ama hafla yoyote ya mwanaccm, hakuna kununua chochote kwenye biashara ya mwanaccm ama hata kupakia vyombo vyao vya usafiri labda iwe lazima sana. Tusiogope kuhamashana kwenye hili. Kwa vyovyote mbinu hii itamgusa kila mtanzania. Kwenye nyumba za ibada hakuna kutoa sadaka, na kuwaambia viongozi wa dini wanakalia kimya uovu. Mbinu hii haitatuacha na vilema wala kubambikiwa kesi, kutekwa ama kuuwawa. Mbinu hii ilitumiwa Zanzibar na ilifanya kazi. Madai ya katiba mpya ni ya halali, kwani wezi wa kura wasio na ushawishi waendelee kututesa na kutimiza kwa madai yetu halali. Ni juu yetu wapinzani kujiokoa.
 
Wewe Hupati TEUZI unahangaika Miaka yote

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Marehemu Magufuli, aliposema Mayala ni neno la kisukuma lenye maana ya njaa,toka kipindi icho nilikuelewa kuwa unasumbuliwa na mayala.
 
Ewe Mgalatia mwenye akili nani amekuloga? Mbona ulianza kwa roho sasa unamalizia kwa mwili?

Ndugu yangu Mayala umelogwa na nani?mbona umekuwa empty kiasi hiki?
 
Paskali hebu ongelea hili la katiba tulilorithi toka kwa mkoloni kuwa na "IMPERIAL PRESIDENCY" yaani raisi alpha na omega kila kitu kinaanzia kwake na kuishia kwake. Hata bunge letu halina mamlaka juu ya analoliamua raisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…