Watanzania tuwe makini na vyombo vya habari vya Kibeberu. CNN wazusha kukamatwa kwa Freeman Mbowe ni amri ya Rais Samia!

Watanzania tuwe makini na vyombo vya habari vya Kibeberu. CNN wazusha kukamatwa kwa Freeman Mbowe ni amri ya Rais Samia!

Ewe Mgalatia mwenye akili nani amekuloga? Mbona ulianza kwa roho sasa unamalizia kwa mwili?

Ndugu yangu Mayala umelogwa na nani?mbona umekuwa empty kiasi hiki?

Ni sisi wapinzani wenyewe tutaweza kujitetea, kwa sasa ccm wamepoteza ushawishi kwa umma, hivyo wamejishika na vyombo vya dola ili kuendelea kututawala kwa shuruti. Namna pekee ni sisi wapinzani kugoma kushirikiana na wanaccm.

Hakuna kushiriki msiba wala sherehe ama hafla yoyote ya mwanaccm, hakuna kununua chochote kwenye biashara ya mwanaccm, ama hata kupakia vyombo vyao vya usafiri labda iwe lazima sana. Tusiogope kuhamashana kwenye hili. Kwa vyovyote mbinu hii itamgusa kila mtanzania. Kwenye nyumba za ibada hakuna kutoa sadaka, na kuwaambia viongozi wa dini wanakalia kimya uovu. Mbinu hii haitatuacha na vilema wala kubambikiwa kesi, kutekwa ama kuuwawa. Mbinu hii ilitumiwa Zanzibar na ilifanya kazi.

Madai ya katiba mpya ni ya halali, kwanini wezi wa kura wasio na ushawishi waendelee kututesa na kutuumiza kwa madai yetu halali? Ni juu yetu wapinzani kujiokoa.
 
Mwambieni mama yenu mwendazake alikuwa anabebwa na Vatican yeye Hana pa kushikia ooh ooh alafu awkward kuwa na female dictator..walikuwepo female dictators 1)Indira Gandhi (2)Jiang Qing (3)Imelda Marcos (4)Elena Ceaușescu..kwa hiyo siyo kitu kipya Kama mtangulizi wako au mumeo dictator lazima utakuwa female dictator..
One wonders who will be the next Indira Gandhi,Jiang Qing,Imelda Marcos or Elena Ceaușescu????????????
 
Wanabodi,

Wiki iliyopita nilialikwa TBC kwenye kipindi cha Mizani, kinachoendeshwa na Dr. Ayoub Rioba. Mada kwenye kipindi hicho ni "Dhima ya Vyombo vya Habari Kulinda Maslahi ya Taifa".

Kwenye mjadala kuliibuka hoja jinsi Vyombo vya habari vya nje vinavyoibagaza Africa katika ripoti zake. Kwao kuibagaza Africa ndio maslahi kwao kwa mataifa yao.

Juzi Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Mbowe amekatwa na Polisi na tuhuma za kijinai.

CNN wameripoti hivi:



Katika ripoti hiyo, kwanza CNN, hawakutafuta any authoritative source Kutoka nchini Tanzania, zaidi ya kuokoteza habari hiyo kama ilivyoripotiwa na media mbalimbali za ndani.

Kwa vile CNN ni chombo cha kibeberu, hivyo kina agenda ya kubagaza, CNN wakamtafuta Prof. Nic Cheeseman, ni Professor wa Democracy, University of Birmingham, kabla ya hapo, alikuwa Director wa African Studies Centre at Oxford University, ili kuichambua habari hiyo.

Prof. Huyo akatunga uongo wa wazi wa mchana kweupe kuwa Freeman Mbowe, amekamatwa kwa amri ya rais Samia ili ku divert attention ya vuguvugu la katiba na tozo kwenye miamala ya simu!.

Huu sio uongo wa mchana kweupe?. Yaani hata kwa akili ya kawaida tuu, yaani Rais wetu Samia atoe amri ya Kukamatwa kwa Mbowe, kisa ni vuguvugu la mjadala wa katiba mpya na tozo za miamala?!, Watanzania tusijue, aliyemkamata Mbowe, amezungumza na sababu ametoa, CNN badala ya kutafuta the reliable sources, wanatuletea wazushi na kutuletea uzushi!. Ukisikia Ajenda hasi ndio hizi!.

Kwa vile hii ni lugha ya watu, na pia naufahamu uwezo wa wengi wetu kwenye uelewa hizi lugha za watu, hivyo ili kuwasaidia wale wenzangu na mimi, sikiliza kwa makini jibu la swali la pili.
"it is a crackdown, she has launched or pretended to launch all along"

Watanzania Wazalendo lazima tuwe makini sana na Vyombo hivi, unaweza kujikuta unasambaza taarifa ya kuibagaza nchi yako, rais wako na watu wako bila kujijua.

Uzalendo wa kweli ni kutanguliza mbele maslahi ya nchi yako, maslahi ya taifa lako, maslahi ya watu wako.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali

Mh Rais ashauriwe kuepuka kutoa kauli tata zinazopelekea watu kuunganisha matukio&kauli zake.
Kauli za Rais zinatoa kiashiria cha;
1.Kuwapa go ahead wenye nia
ovu kufanya uovu,hata kama
hawajaagizwa.
2.Kuweka uhalali wa matukio kutokana na kauli za Rais.
Hata kama si maagizo yake.
KUMBUKA kauli za Hayati dhidi
ya Lissu,na tukio la Lissu
kushambuliwa.
Ni muhimu kama kiongozi achunge maneno.
Hata hivyo bado ana nafasi kubwa
ya kukitendea haki kiti chake.
 
Hizi akili za njaa ni tatizo sana kwa taifa hili.
Mzee kama wewe bado huishi kujikomba kupata ubwabwa.
 
CNN mambo ya Tanzania wao yanawahusu kitu gan??

Fake mainstream media hawawez kuingilia mambo yetu ya ndan,so chadema wanadhan hao CNN watawasaidia kitu gan
Mambo ya ndani ni uonevu dhidi ya wapinzani ?!. Sasa mbona mnawaachia hata bila kuwafungulia kesi ?! Mnasumbuliwa kasumba na ulimbukeni wa ki dictator na ukoloni . Hayo mambo yameshapitwa na wakati [emoji107]
 
Rubbish
Profesa Cheeseman ambae kiumri bado kijana sana (ana miaka 42) amewahi kuandikia Daily Nation la Kenya.

Alijiuzulu kuandikia gazeti hilo kwa kudai kuna censorship.

Kila nchi ina maamuzi katika kuangalia ufanisi wa waandishi wa habari kwamba hawaandai sumu ya kuwalisha wasomaji.

Sumu hizo ni uchochezi, fake news na habari zisizo na vyanzo vya kuaminika.

Hivyo tokea sakata la Daily Nation profesa Cheeseman hawezi kuwa na mtazamo chanya juu ya Afrika.

Moja ya nyenzo muhimu kabisa kwa mwandishi wa habari ni kuwa na "reliable sources", wengi hawana akiwemo profesa Cheeseman.

Huu ni wakati wa waandishi nguli kama wewe bwana Mayalla kuanza kupika waandishi wapya kabisa na walo na maono ya kitaifa na pia kujifunza kutoka propaganda za nje.

Waandishi wa habari wenye "critical thinking" hawapo Tanzania kwa sasa.
 
Kwa hiyo ungekuwa ndio wewe mwandishi wa habari....je tukupigie makofi kwa kunukuu taarifa nyeti kutoka kwa NON-AUTHORITATIVE SOURCE?
Na Mayala ni mwandishi au mwanaharakati? Kama ni mwandishi ningejiridhisha kwa tabia na kutokuwa na upande hasa kwa kuwabeza wapinzani, watanzania wote tunajukumu la kulea vyama vyote vya siasa, viwe bora ili baadae vikiweza kuchukuwa madaraka, pia viweze kuendesha Nchi kwa jinsi tunavyotarajia!
 
Mh Rais ashauriwe kuepuka kutoa kauli tata zinazopelekea watu kuunganisha matukio&kauli zake.
Kauli za Rais zinatoa kiashiria cha;
1.Kuwapa go ahead wenye nia
ovu kufanya uovu,hata kama
hawajaagizwa.
2.Kuweka uhalali wa matukio kutokana na kauli za Rais.
Hata kama si maagizo yake.
KUMBUKA kauli za Hayati dhidi
ya Lissu,na tukio la Lissu
kushambuliwa.
Ni muhimu kama kiongozi achunge maneno.
Hata hivyo bado ana nafasi kubwa
ya kukitendea haki kiti chake.
Huu ni ukweli wenyewe. Mkuu umemaliza. Wateule wa hovyo na wasaka vyeo, kutumia mianya kupitia kauli za Rais kutenda maovu . Rais achunge kauli zake. (Chokochoko)
 
Huyo mdada wa CNN anaijua vizuri katiba ya nchi yako na hali ya demokrasia Africa kwa sababu Ni msomi mwenye masters ya Uandishi, anasoma, anafuatilia, anauliza vyanzo makini kama mwandishi makini na serious anayeipenda kazi yake.

Nyie endeleni kujaza waandishi uchwara, bongo movies na makanjanja wapiga makele kwenye media zenu ambao kazi yao ni kufukizia deal za matangazo na bahasha halafu mbaki mnalia haiwezekani na huo utopolo mwingine wa CIA.
Katika hili nakuunga mkono,nchi hii inafuatiliwa sana,kiukweli utawala uliopita ulileta doa kubwa huku nchi ikifuatiliwa kwa karibu kuwa na element za udikteta.Haiwezekani mdada wa CNN aielewa vyema katiba ya nchi hii,anamuuliza mchambuzi wa masuala ya kidemokrasia kwa nchi za Africa hadi nikashaangaa.CNN ni tawi la CIA na FBI.Itakuwa tunawachunguzi humuhumu wa mabeberu.Wanasiasa waliopo ughaibun nao wanaichafua nchi hii,hawezekani Lissu anasema hatutawadhamin huku akitaka waachiwe bila masharti yeyote na imekuwa hivyo,kwanini anajiamini hivi.Wanasiasa wa upinzan warudi nchini baada ya maridhiano,kuna mpasuko nchi hii.
 
Wanabodi,

Wiki iliyopita nilialikwa TBC kwenye kipindi cha Mizani, kinachoendeshwa na Dr. Ayoub Rioba. Mada kwenye kipindi hicho ni "Dhima ya Vyombo vya Habari Kulinda Maslahi ya Taifa".

Kwenye mjadala kuliibuka hoja jinsi Vyombo vya habari vya nje vinavyoibagaza Africa katika ripoti zake. Kwao kuibagaza Africa ndio maslahi kwao kwa mataifa yao.

Juzi Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Mbowe amekatwa na Polisi na tuhuma za kijinai.

CNN wameripoti hivi:



Katika ripoti hiyo, kwanza CNN, hawakutafuta any authoritative source Kutoka nchini Tanzania, zaidi ya kuokoteza habari hiyo kama ilivyoripotiwa na media mbalimbali za ndani.

Kwa vile CNN ni chombo cha kibeberu, hivyo kina agenda ya kubagaza, CNN wakamtafuta Prof. Nic Cheeseman, ni Professor wa Democracy, University of Birmingham, kabla ya hapo, alikuwa Director wa African Studies Centre at Oxford University, ili kuichambua habari hiyo.

Prof. Huyo akatunga uongo wa wazi wa mchana kweupe kuwa Freeman Mbowe, amekamatwa kwa amri ya rais Samia ili ku divert attention ya vuguvugu la katiba na tozo kwenye miamala ya simu!.

Huu sio uongo wa mchana kweupe?. Yaani hata kwa akili ya kawaida tuu, yaani Rais wetu Samia atoe amri ya Kukamatwa kwa Mbowe, kisa ni vuguvugu la mjadala wa katiba mpya na tozo za miamala?!, Watanzania tusijue, aliyemkamata Mbowe, amezungumza na sababu ametoa, CNN badala ya kutafuta the reliable sources, wanatuletea wazushi na kutuletea uzushi!. Ukisikia Ajenda hasi ndio hizi!.

Kwa vile hii ni lugha ya watu, na pia naufahamu uwezo wa wengi wetu kwenye uelewa hizi lugha za watu, hivyo ili kuwasaidia wale wenzangu na mimi, sikiliza kwa makini jibu la swali la pili.
"it is a crackdown, she has launched or pretended to launch all along"

Watanzania Wazalendo lazima tuwe makini sana na Vyombo hivi, unaweza kujikuta unasambaza taarifa ya kuibagaza nchi yako, rais wako na watu wako bila kujijua.

Uzalendo wa kweli ni kutanguliza mbele maslahi ya nchi yako, maslahi ya taifa lako, maslahi ya watu wako.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali

Mateso ya Erick Kabendera na kifo cha mama yake vitakuandama mpaka mwisho.
 
Punguza kelele wamwachie...

Tumechoshwa na kelele zenu, mmekamata hamtosheki mnakuja kufungua fungua nyuzi kila baada ya sekunde kama mna uhalo mkavu
 
Back
Top Bottom