Watanzania tuwe makini na vyombo vya habari vya Kibeberu. CNN wazusha kukamatwa kwa Freeman Mbowe ni amri ya Rais Samia!

Yaani hayo maswali yanaonesha upeo wako wote.
 
Wee mzee sometimes tunakutetea huku ila sometimes unayakoroga mwenyewe,

Hii ni hesabu ya chekechea

1. Jeshi la polisi limemkamata Mbowe kwa tuhuma ambazo mpaka sasa hawajamfikisha mahakamani kujua ana hatia au la.

2. Raisi Samia ndie amiri jeshi mkuu.

Nani alaumiwe ?
 
Mimi nimeyasikiliza hayo mahojiano..Kama wewe ni mwanahabari kweli na a just person, sema Prof Cheeseman ameongea kitu gani kibaya au cha uongo kwenye hayo mazungumzo?..mpaka useme sijui wamebagaza, sijui ni chombo Cha mabeberu.. nitajie neno moja tu ambalo sio kweli. Nasubiri majibu yako

Your browser is not able to display this video.
 
Well said comrade.......

Paschal Mayalla ameshawahi KUSHAURI hayo na kuweka BANDIKO humu ndani.....

Katika Zama Kama hizi za "kuchafuka kwa bahari" kwa kweli TUNAYUMBA....TUNAYUMBA MNO....

Ninaamini tuna watu wenye WELEDI mkubwa tu.....

Ni muda mwafaka kwa SERIKALI YA AWAMU YA 6 KUCHUKUA HATUA STAHIKI Kwani tuendako CHANGAMOTO kubwa zitatukabili....
 
🤣🤣🤣🤣 I always like your writing skills sir ...
 
Hawawezi kuwa wa wazi !!. Kwa sababu wanajaribu kuuiga u communist ktk dunia ya leo. Na katika u communist hakuna uwazi , bali kumtukuza mtawala .
 
Jumbe Brown:Mimi Mimi ni mwana CCM Toka mwaka 1989 nimeshika nyadhifa mbalimbaliza chama na serikali kwa hiyo nchi hii naijua kwa kiasi chake ,Sasa Nakupa mfano ebu cheki uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2019 na uchuguzi mkuu 2020 vipi kama Taifa tupo sahihi?Vipi hujui chaguzi za Namana hii ndo huingiza nchi kwenye machafuko?

Sasa Leo anatokea kiongozi kama Mbowe anadai tupate katiba mpya ili tuwe na Taifa lenye haki anabambikizwa kesi eti ni gaidi .Sasa kati ya Mbowe na sisi nani ni mzalendo.Tuache unafiki tuipende nchi yetu kwa kupenda ukweli hata kama unatuumiza.
 
Hivi unaposema wanaandika pasipo vyanzo vya kuaminika,naomba nikuulize hivyo vyombo vya kuaminika unavyotaka wewe ni vipi??
Polisi walisema wamemshitaki kwa makosa ya ugaidi,sote tunajua mfumo wa Tanzania ulivyo hata polisi waliomkamata walisema wamepokea maelekezo maana yake ni kuwa RPC alipkea maelekezo kutoka kwa IGP na IGP anayatoa kwa RAIS sasawewe kwa akili yako tueleze kama kuna MTU anayeweza MPA maelekezo IGP tofauti na Rais??
 
Wakati mwingine naona katika maraisi nchi ambao ni bora kabisa kwa dhana ya uhuru wa habari na kujieleza Kikwete Jakaya anabaki kuwa bora kabisa. Alishawahi kuwambia CCM wenzie kuwa hoja ujibiwa kwa hoja sio kwa kutumia polisi na vyombo vya usalama.Ndio maana wakati wa utawala wake watu walikua huru kutoa maoni hata ikapelekea kuibuliwa madudu mengi ikiwemo suala la ufisadi na pia akaasisi mchakato wa katiba mpya Sasa kwanini ccm wanaogopa katiba mpya?
 
Mwenyewe nawashangaa hawa wana CCM wenzangu hivi mwanaume kabisa unakuwaje MTU wa kila kitu ndio pasipo hata kutumia ubongo.
Kupitia Mwenyekiti wetu Magufuli tumepata somo kubwa sana,na hilo somo ni umuhimu wa Katiba Mpya.halafu huwa namshangaa mwana CCM anayebisha kuwa hakuna umuhimu wa Katiba mpya unabaki unajiuliza hivi huyu na Nyerere aliyeanzisha Chama na kusema mapungufu ya Katiba hii nani hiyo sahihi??
 
Pasikali aisee unawafundisha CNN jinsi ya kuripoti habari?!

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo lingine hata kama mama hakutoa maelezo hayo ni kuwa kila askari anaenda kumkamata mtuhimiwa huyu askari anajitoa ufahamu anasema "sio mimi nimepewa maelekezo ya kukukamata kutoka juu"sasa kauli ya askari kama hii tayari mojakwa moja mlengwa analenga kuwa ni Rais maana huku juu maelezo yanakotoka hawamalizii kusema ni juu kwa nani.
Hili nalo linachangia mama kuhusishwa
 
Wewe nawe mjinga mbowe kakamatwa kwa amri toka juu sababu CCM hawataki katiba mpya, hawataka siasa za ushindani na wao ndio wanaowatumia vyombo vya usalama kwa maslahi yao je mwenyekiti wao ni nani kama sio raisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…