WaTanzania wanahitaji Mageuzi Makubwa sana - Ni lazima CCM iondoke madarakani

WaTanzania wanahitaji Mageuzi Makubwa sana - Ni lazima CCM iondoke madarakani

Sisiemu itaondokaje wakati hakuna chama mbadala? Na hata kama vipo, vina watu wenye uweledi wa kuongoza serikali na nchi?
Unahoji kwamba hakuna wenye weledi huku wewe uko juu ya stuli ndefu kaunta unashushia balimi baridiii huku unasikiliza mziki wa Marioo wa "asikwambie mtuu bia tamuuu.."
 
Uhuru wa kutoa mawazo upo kama haupo.
Ukiilaumu serikali ukaigusa pabaya upo matatani !
Ukilaumu Bunge ukaligusa pabaya upo matatani !
Ukiilaumu polis ukaigusa pabaya ndio usiseme !
CCM imevikalia vyombo hivi na havipumui havina sehemu katika kufuata katiba,hii hii iliokuwepo ,hawawezi kutekeleza majukumu yao kwa kujiamini,wanahofu,wanaogopa kupoteza kazi.
Kusema hakuna Chama kingine hio sio kweli ni kuzidi kudumiza mawazo,Hakifuatwi Chama kunafuatwa Katiba ya Nchi ,vyombo husika ni lazima vifanye kazi zake kwa mujibu wa sheria,CCM imejipenyeza na imeviteka vyombo hivyo. Tunaona Chaguzi hazifuati sheria wala katiba yaani mambo mengi yanakiukwa mchana kweupe. Unapoenda kusema unakutana na wale wale waliojipenyeza.
Nchi inazidi kuvurugwa na wanaovuruga ni hawa CCM ,tukubali wameteka kila kitu.
 
Unahoji kwamba hakuna wenye weledi huku wewe uko juu ya stuli ndefu kaunta unashushia balimi baridiii huku unasikiliza mziki wa Marioo wa "asikwambie mtuu bia tamuuu.."
Dah! Si uongo Mkuu wewe ni bonge la mtabiri! Yaani umesema ukweli mtupu! Ebu nipe na mechi za kubetia leo nipate ya kuzimulia kesho!
 
Unataka mpinzani atokee nchi za nje?wapinzani watatoka ndani ya ccm na wengine kutoka kwa raia wema wa kitanzania ambao wanaifahamu demokrasia,Sasa ndugu yangu ulitaka wapinzani watokee wapi?
 
CCM na Chama cha Kikomunisti cha China ni kitu kimoja. Huu ni ukweli mchungu sana kwenu.

Kila mwanaccm anatamani iwe hivyo, au ionekane ni hivyo. Hata hivyo sio kila mtu anaona fahari mwenendo wa hicho chama cha kikomunisti cha China. Hivyo sio jambo linalotutia wivu sisi kuona nyie ccm mnanasibisha na chama cha kikomunisti cha China, yaani hatuoni wivu kabisa, na hata mkijisifia ufanano wenu na chama cha kikomunisti cha China, tunawaona ni majuha tu. Imeisha hiyo.
 
Back
Top Bottom