Watanzania wanaosoma Urusi huwa wanachezewa akili na Warusi?

Watanzania wanaosoma Urusi huwa wanachezewa akili na Warusi?

Nazungumzia watanzania waliosoma Urusi kwakuwa ni hao ambao ninawafahamu vizuri pengine na wa nchi nyingine wapo hivyo pia lakini sifahamu.

Kikubwa ni kwamba wasomi wengi waliosoma nchini Urusi wakirudi na wakarudi nchini wengi wao huwa wanakuwa hawana akili nzuri, nimefatilia hilo kwa kipindi kirefu sana.

Nina baba yangu mdogo alisoma Urusi kwa kipindi cha kipindi cha miaka saba aliporudi nchini amekuwa mlevi wa kupindukia haeleweki kabisa mambo anayoyafanya wakati alipokuwa akiondoka alishakuwa daktari mzuri tu.

Mwingine ni mjomba wa rafiki yangu wa karibu, yeye siku ambayo mjomba wake anafika airport walimshangaa kwakuwa jinsi walivyomkuta hawakutegemea kabisa alikuwa kama chizi chizi tu na muda huu ninapoandika thread hii mjomba wa rafiki yangu huyu ni kichaa kabisa.

Ni wengi sana ninaowafahamu walienda kusoma Urusi wakiwa na akili nzuri tu na waliporudi wamerudi wakiwa hawana akili timamu kabisa yaani wanakuwa hawaeleweki eleweki kabisa.

Nikawa nafikiria pengine wakifika nchi za watu wanaiga sana tabia ya kunywa pombe kwakuwa wenzetu wa Urusi wanakunywa sana pombe hivyo pombe hizo zinawaathiri nikagundua kuwa sikweli kwakuwa hata Ujerumani ni wanywaji wazuri sana wa pombe lakini watanzania wanaosoma huko hawapo kama ndugu zetu (wengi) walisoma Urusi.

Je? Warusi huwa wanachezea akili za Watanzania? hili tatizo lipo kwa watanzania tu?

ni kweli kabisa nina mifano hai km 3 hv tena ni waalimu wa chuo cha must mbeya,wameenda urus wamerudi hajielewi kabisaaa!!!cjui huwa wanawapa nini??
 
Mimi Nafikiria ni Tatizo la Mtu mwenyewe na Sio warusi. Mimi nawaelewa wengi waliosoma na Hivi sasa wanamafanikio ya kutosha nakutajiaa.
1. Kuna Daktari wa Wanawake yuko Mnazi mmoja Zanzibar anaitwa Dr. Juma ambaye hata Muhimbili wanamtumia yeye wiki mara mo anakwenda Muhimbili.
2. Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar vile vile Kasoma Urusi Jina Dr. Garu
3. Dr. Talib Ali yeye kamaliza Urusi, kafanya kazi Muhimbili miaka miwili, baadaye kaenda Amerika kasoma na hivi sasa kaanzisha Detal clinik ya kwake mwenyewe karibu na washington nenda inaitwa AVATAR Dental clinic
Na wengi ninawaelewa
4. Mimi mwenyewe nimesoma Urusi, Baadaye nimefanya kazi Tanzania miaka 5, na Hivi sas niko Ujarumani na nafanya kazi kwenye Consulting Company kwa miaka 10 hivi sasa kama Structural Engineer

Tatizo liko kwo wenyewe

Mkuu Mtambwe,
Nakubaliana na wewe kuwa tabia ya mtu inategemeana na mtu mwenyewe.Mtu kuwa 'CHAPOMBE' au 'CHIZI' inachangiwa na mambo mengi ikiwepo background history na msongo wa mawazo
Mimi mwenyewe ni mmoja wa watu waliosoma Urusi na kama ni pombe nilikua nakunywa tena sana.
Hii thread imejaribu kuangalia watu waliosoma Urusi na kwa kuwa hakuna utafiti wowote uliofanyika watu wameweka taarifa za watu wanaowazunguka(Naogopa kusema hao mliowaona au kuwajua ni sehemu ndogo sana ya watu waliosoma Urusi).Ni bahati mbaya kwamba wanafahamiana na watu ambao labda kutokana na ugumu wa maisha na msongo wa mawazo waliona njia mbadala ni kuishi maisha waliyoishi na matokeo yake wamepata madhara kwenye hilo.
Ili tuweze kukubakliana na mtoa mada inabidi atupe statistics za watu waliosoma Urusi katika kipindi fulani na atuambie katika hao ni wangapi wanaonekana kama anvyoita 'Machizi'.
Wakati mimi naenda Urusi nilienda na wenzangu watano.Wote tumerudi salama na kila mmoja anashughulika na maisha yake ya kila siku.Pamoja na hayo tuliweza kufahamiana na Watanzania wengine waliokua mbele yetu au waliokuja nyuma na kwa kuwa bado tunawasiliana wote wapo vizuri na maisha yanaenda.
Kuonekana chizi sio lazima uwe umesoma Urusi wapo wasomi wengi wanaonekana akili hazijakaa sawa kwasababu mbalimbali nyingi zikiwa ni kutokuweza kutawala msongo wa mawazo.
 
inashangaza sn.pia naishangaa s/kali ytu,kwa kua inapoteza pesa nyingi kuwasomesha watu wke
rkn mwosho wa cku hasara.aifanyi uchunguzi,aijiuri kwa nn hyu karudo yko so!ni ttzo kwakweli.roho inauma kupoteza maichinia,maprofesa nk.

Kati ya serikali ambayo haisomeshi wananchi wake nje ya kwanza ni Tanzania, usiisingizie kabisa, watu wote unaoona wanasoma scholarship nje jua wanalipiwa either na vyuo au serikali ya nchi hiyo waliopo ila sio serikali ya Tanzania, na Tanzania inabidi ianze kusomesha wataalam nje, its a very good thing nashangaa kwa nini uko against nacho
 
mimi ninachojua wengi wao wakirudi hawaamini uwepo wa mungu, kumbe na hili pia lipo

Mkuu inategemea na mtu mwenyewe.Kule kuna uhuru sana wa mtu kujiamulia style ya maisha aitakayo.Kama mtu akimkataa Mungu ujue hakua na msingi mzuri wa imani yake.
Bado nasisitiza tabia ni mtu mwenyewe wala sio Warusi.Ukiwaiga baadhi ya warusi utaishia kuishi maisha ya ajabu ajabu.
 
Dah ...hii ni kweli kabisa hata mimi kuna watu 3 nawafahamu...wamerudi na hali mbaya sana ..mmoja kati ya hawa ni kichaa...alikua anapanga mawe pale kwenye junction ya morogoro road na bibi titi, ana phd.

Huyo alikuwa anafanya utafiti!!! Sasa hivi yuko wapi?
 
Wapo wengi sana wazuri tu na hadi leo hii wanatumika sana maeneo mbalimbali.

Kaka yangu na rafiki yangu wamesoma na wamerudi wazima kabisa. Leo wote ni Wahandisi Tanzania.

Kuna wengine kweli ni wanywaji sana, kama huyu JEMBE aka Mbunge wa Geita, Max, kapiga sana kinyaji akiwa Mbunge.

1653.jpg
 
Kama vile kweli wengi huwaga hawaamino kama kuna mungu
 
Ni kweli hata my auncle naye alisoma huko Urusi mambo ya Engeneering miaka ya 70 kaja zake TZ kafanya kazi miaka kadhaa pale wizara ya Ardhi ila akafukuzwa kwa redundancy shauri ya pombe na anasa zake.
Mwaka 83 mara tu baada ya kufukuzwa kazi alichanganyikiwa na siku hz yupo kama ZEZETA.
 
Hii issue ina ukweli wake wakuu. Mimi nawafahamu wakaka wawili wa familia moja wote waliporudi walichanganyikiwa. Mmoja ndio akapotea kabusa mpaka leo hajulikani yuko wapi mpaka ndugu zake wanahisi alishakufa labda. Mwingine yupo ameshakuwa mtu mzima kzbisa lakini alichanganyikuwa kabisa yani hana mke, hana kazi na ni chizi
 
Dah ...hii ni kweli kabisa hata mimi kuna watu 3 nawafahamu...wamerudi na hali mbaya sana ..mmoja kati ya hawa ni kichaa...alikua anapanga mawe pale kwenye junction ya morogoro road na bibi titi, ana phd.
kwl kbsa kaka alikuwa ni lecture mzuri sana huyo jamaa pale DIT
 
we humuoni Lukuvi mana nae alienda huko miaka ya 1970s kwa course ya wiki moja kuchukua certificate ya political science...............VODKA inahusika hapa

Alipata matatizo na ukichaa baada ya kusoma course ambazo wanasoma warusi tu.
Ndipo aliporudi Bongo na kujitambua kwamba sio mzima, akaamua kwenda kwa babu wa Loliondo kipindi kile.
 
Labda wanatumia vitu ambavyo hata wenyeji wenyewe wanaviogopa. Na mara nyingi sisi waTanzania ni wabishi sana, ukiambiwa hii acha mbaya wewe ndiyo unataka hiyo hiyo, madhara yake ndiyo kama hayo. Hata wazungu wanaokuja bongo na kufakamia gongo zilizotengenezwa kwa maji ya betri wengi wanaishia kuwa machizi.
 
Mkuu inategemea na mtu mwenyewe.Kule kuna uhuru sana wa mtu kujiamulia style ya maisha aitakayo.Kama mtu akimkataa Mungu ujue hakua na msingi mzuri wa imani yake.
Bado nasisitiza tabia ni mtu mwenyewe wala sio Warusi.Ukiwaiga baadhi ya warusi utaishia kuishi maisha ya ajabu ajabu.
wazazi wangu walinikatalia kuenda kusoma huko kwa sababu za kidini. na kuniruhusu kuenda uturuki
 
Baadhi ya sababu ni hizi
1. Maisha ya Russia yana stress nyingi sana, kumbuka kule kuna ubaguzi wa hali ya juu, lakini ni baadhi ya sehemu. Russia bado kuna makundi ya vijana wa kifashist ambao wakimuona mtu mweusi siyo tu kumtukana, lakini huwa wanatoa hadi vichapo.
2. Maisha ni magumu, Russia siyo kama nchi nyingi za Western Europe, kule life tilt na ngumu sana kuwa unafanya kazi na kuingiza kipato kingine nje ya boom. Vitu hasa vyakula vipo juu sana wanafunzi wanashindwa kumudu matokeo yake sasa watoto wa kike wanaishia kuwa machanguduo au kutafuta waarabu waweze kuwatunza, na wale wengine wanaishi kwa utapeli na kuiba vipodozi kwenye masupermarket. Vijana wa kiume huwa wanafanya mpango wa kuwa na wanawake wa kirusi wenye kazi nzuri au maisha mazuri ili waweze kukabiliana na maisha, haswa hapa ndipo tatizo linapoanzia manake mtoto wa kiume anajikuta hana kabisa uhuru wa kufanya lolote mbele ya mwanamama ukiangalia anapewa hela ya kula na kunywa.
3. Ingawa maisha ya Russia especially Moscow yapo juu sana, lakini anasa ni nyingi sana zikiwemo pombe na wanawake. Kwa ufupi Russia wanauza pombe na sigara kwa bei nafuu sana hii inasababisha hata kwa hela ndogo kabisa watu waweze kumudu. Kingine hapo ni hao wanawake, Russia imejaaliwa kuwa na wasichana wazuri na warembo haswa ukilinganisha na wazungu wengine, wasichana hawa wengi wao ni warahisi sana na unakuta wanapenda watu weusi, sasa hapo nipo kwenye tatizo, vijana wengi wanafanya umalaya wa kupitiliza hadi kusahau kabisa shule, au unakula mwanamke anamng'ang'ania ili abaki Russia masomo yake yatakapoisha. Sasa hii kitu huwa inawaconfuse sana vijana wetu kule.
4. Vijana wengi wa kiume huwa wanazaa na wanawake wa kirusi, lakini wanafanya hivyo bila ya kuwa na malengo maalumu angalau wapo wale wanaotaka passport(wachache sana). Sasa unakuta mtu anapomaliza anataka achukue mtoto wake na dada wa kirusi anagoma kwa hiyo unakuta mtu anachanganyikiwa kwa kuacha damu yake ughaibuni (hawa wapo wengi sana, nadhani ndiyo wanaongoza).
5. Angalau Russia kuna ubaguzi, lakini kwa upande fulani kuna ufree mkubwa sana kwa mtu kuamua aishi vipi, yaani mtu anaweza toka bongo ni ustaadhi au mlokole mzuri lakini akifika kule anakutana na ule ufree ambao bongo alikuwa haupati(kumbuka wengi wanaojifanya kushika sana dini kwa hapa kwetu tz ni kwa ajili tu ya mazingira na watu wanaomzunguka) sasa kwa Russia no one cares wewe fanya utakalo as long kwamba hauvunji sheria za nchi. Unaweza ukawa unakwenda club kila siku kuanzi j3, j4 hadi j3 nyingine, unaweza wewe ukawa unakunywa pombe kiasi utakacho, yaani hakuna atakayekufuatilia kabisa, that is your life.
6. Kingine ambacho nadhani ni kikubwa zaidi ni hizi Russian Vodka, hizi kitu aisee ni shida sana, ni pombe kali sana hakuna. Vijana wengi huwa wanazifakamia hizi kitu na hasa ukizingatia hata kama Tz zipo lakini siyo kali kama za Russia, zile za kule jamani ni balaa sana. Warusi wenyewe hasa wenye fezwa huwa wanakunywa sana Vodka, lakini wanakula matunda mengi na manyama nyama yao fulani ambayo yanasaidia sana kuua ukali wa pombe, sasa mwenzangu na mimi mwanafunzi wa kibongo na boom la dola 300 kwa mwezi hautoweza kumudu kununua hizi nyama na matunda, ni ngumu sana. (Hii ndiyo sababu kubwa zaidi kwa upeo wangu, Vodka ndizo zinawapa watu matatizo, narudia tena hii siyo kwa watanzania tu hata kwa warusi wenyewe hasa wale wa kipato cha chini huwa wanapata uchizi kutokana na hizi pombe kali za Vodka).
7. Winter, baridi la Russia ni baridi dume yaani usikae kabisa ukataka kulinganisha na kale kaupepo ka Makambako. Russia kuna winter la hatari, ila warusi wengi walio na kipato kizuri huwa wanaweza kujisitiri na hili baridi, lakini sasa wabongo inakuwa ngumu kwao kutokana na kipato hafifu walichonacho kuweza kununua nguo nzito kama vile sox za winter, viatu vya winter, makoti, sweaters, gloves, kofia nzito, blanket nzito za winter, kwa hiyo athari ya baridi huwa linawachukua taratibu sana mpaka ukifika muda wa miaka mitano mpaka kumi nipo unakuta mtu anaumwa sana tena magonjwa ya baridi ambayo kisayansi ungonjwa unaweza penya hadi kwenye ubongo na kumfanya mtu awe chizi.
8. Kingine angalau kinaweza kisichangie sana ni sigara, watu wengi wanaanza kujifinzia kuvuta sigara wakiwa kule, hii ni katika harakati za kupunguza baridi na stresses.
Ushauri: Serikali isiwe inawatelekeza hawa watoto na vijana wetu walio kule. Iwe inajaribu kufanya follow ups na kujua maendeleo yao academically. Elimu ya Russia ni nzuri sana, lakini kuna udanganyifu wa hali ya juu kwenye kupata marks na hatimaye cheti.
 
mimi nafikiria ni tatizo la mtu mwenyewe na sio warusi. Mimi nawaelewa wengi waliosoma na hivi sasa wanamafanikio ya kutosha nakutajiaa.
1. Kuna daktari wa wanawake yuko mnazi mmoja zanzibar anaitwa dr. Juma ambaye hata muhimbili wanamtumia yeye wiki mara mo anakwenda muhimbili.
2. Mkurugenzi wa mamlaka ya maji zanzibar vile vile kasoma urusi jina dr. Garu
3. Dr. Talib ali yeye kamaliza urusi, kafanya kazi muhimbili miaka miwili, baadaye kaenda amerika kasoma na hivi sasa kaanzisha detal clinik ya kwake mwenyewe karibu na washington nenda inaitwa avatar dental clinic
na wengi ninawaelewa
4. Mimi mwenyewe nimesoma urusi, baadaye nimefanya kazi tanzania miaka 5, na hivi sas niko ujarumani na nafanya kazi kwenye consulting company kwa miaka 10 hivi sasa kama structural engineer

tatizo liko kwo wenyewe


subiri pm kutoka kwa dada zetu humu...

We subiri tu zinakuja
 
Hivi mtu ukiwa unapiga mitungi daily wewe ni chizi? Mbona wavuta sigara daily maofisini hamuwaiti machizi? Acha tupige mitungi hadi kuchee,

Ndio Nyie mnaozungumziwa na Mtoa mada.... Machizi...

Mfano uliotoa ni chizi peke yake anayeweza toa mfano usioendana na akili timamu... IQ Ndogo mno... utakuwa Umesomea Urusi wewe kama sikosei...
 
Back
Top Bottom