Watanzania wanashangaza Sana; hawataki kujiingiza kwenye Siasa halafu wanalaumu Wanasiasa!

Watanzania wanashangaza Sana; hawataki kujiingiza kwenye Siasa halafu wanalaumu Wanasiasa!

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Napenda Siasa Kwa sababu ni mchezo wa wenye wajanja. Napenda Biashara Kwa sababu ni mchezo wa wenye bahati, napenda Fasihi na Falsafa Kwa sababu ni uwanja wa Akili na hekima.
Napenda sheria Kwa sababu ni mto ubebao Haki na Dhulma. Itoshe!

Watanzania wengi ni watu wa ajabu Sana, ukienda vijiweni ukaanzisha Mada ya Siasa hutapata wachangiaji wengi, na wengi watakuambia hawapendi kujadili wala kujiingiza kwenye Siasa. Hilo sio tatizo kwani kila mtu anamaamuzi na Uhuru wake, lakini tatizo ni pale mtu asiyejihusisha na Siasa halafu muda huohuo utamkuta ananilaumu serikali au kuwasema viongozi. Huo Kama sio wendawazimu ni nini!

Siasa ni mchezo wa maslahi, vita ya kupata kikubwa, silaha ya kuitafuta kesho iliyobora kabisa.

Huwezi kuwa Mfanyabiashara mkubwa bila kuwa mwanasiasa, huwezi kuwa mtu Mkubwa bila kuwa mwanasiasa, huwezi kuwa Sheikhe, Imamu au Mchungaji au Askofu bila kuwa Mwanasiasa.
Huwezi kuwa Mwandishi, Mwanamuziki mkubwa bila kuwa mwanasiasa,

Kujitenga na wanasiasa kunamaanisha Jambo moja tuu, kutafuta kuwa mnyonge, mtu asiye na maslahi.
Msindikizaji,

Kama kuna Jambo ambalo watoto wangu nitawaambia wasije kujitenga nalo basi ni Siasa. Kujitenga na Siasa ni kutaka kutawaliwa, kukaliwa kooni, kuwa tabaka la chini.

Watu wote wakubwa katika sekta zote wanajihusisha na Siasa iwe Direct au indirect.

Kujiingiza kwenye Siasa Kwa watu wote ndio huitwa Demokrasia, yaani kila mmoja kuyapigania maslahi yake kivyovyote, Kwa Amani au kwa vita, Kwa mazungumzo au Kwa silaha.
Kugawana na sio kugawiwa.
Kupeana na wala sio kupewa.

Wanasiasa wote Duniani wanatabia zinazofanana, Hawana tungo isemayo; Kesho yangu ni bora kuliko leo.
Wao wananeno moja tuu, nalo ni; Leo ni leo asemaye kesho muongo.
Wanasiasa wanamsimamo wa tumalizane leoleo, kila mtu achukue chake leo, mambo ya kesho yatajijua yenyewe.

Wakiwa mbele za watu watasema, Mradi au mpango huu utaleta tija miaka kumi ijayo" ilhali wao wananufaika na mpango huo Leo hii,

Ni Kama Siasa za wachungaji na waganga wajanja, atakuambia Akuombee na mwaka ujao utafanikiwa tuu! Lakini wao watakuambia uwape pesa Leo hiyohiyo. Hiyo ni Siasa, janja janja na utapeli uliohalalishwa.

Watanzania wenzangu sijui nilikuwa nazungumzia nini, hapa nimeshajichanganya.
Ila niseme tuu; Kujitenga na Siasa ni kujitenga na maisha mazuri ya Dunia.
Kukimbia maslahi yako na familia yako.

Nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
 
Kwema Wakuu!

Napenda Siasa Kwa sababu ni mchezo wa wenye wajanja. Napenda Biashara Kwa sababu ni mchezo wa wenye bahati, napenda Fasihi na Falsafa Kwa sababu ni uwanja wa Akili na hekima.
Napenda sheria Kwa sababu ni mto ubebao Haki na Dhulma. Itoshe!

Watanzania wengi ni watu wa ajabu Sana, ukienda vijiweni ukaanzisha Mada ya Siasa hutapata wachangiaji wengi, na wengi watakuambia hawapendi kujadili wala kujiingiza kwenye Siasa. Hilo sio tatizo kwani kila mtu anamaamuzi na Uhuru wake, lakini tatizo ni pale mtu asiyejihusisha na Siasa halafu muda huohuo utamkuta ananilaumu serikali au kuwasema viongozi. Huo Kama sio wendawazimu ni nini!

Siasa ni mchezo wa maslahi, vita ya kupata kikubwa, silaha ya kuitafuta kesho iliyobora kabisa.

Huwezi kuwa Mfanyabiashara mkubwa bila kuwa mwanasiasa, huwezi kuwa mtu Mkubwa bila kuwa mwanasiasa, huwezi kuwa Sheikhe, Imamu au Mchungaji au Askofu bila kuwa Mwanasiasa.
Huwezi kuwa Mwandishi, Mwanamuziki mkubwa bila kuwa mwanasiasa,

Kujitenga na wanasiasa kunamaanisha Jambo moja tuu, kutafuta kuwa mnyonge, mtu asiye na maslahi.
Msindikizaji,

Kama kuna Jambo ambalo watoto wangu nitawaambia wasije kujitenga nalo basi ni Siasa. Kujitenga na Siasa ni kutaka kutawaliwa, kukaliwa kooni, kuwa tabaka la chini.

Watu wote wakubwa katika sekta zote wanajihusisha na Siasa iwe Direct au indirect.

Kujiingiza kwenye Siasa Kwa watu wote ndio huitwa Demokrasia, yaani kila mmoja kuyapigania maslahi yake kivyovyote, Kwa Amani au kwa vita, Kwa mazungumzo au Kwa silaha.
Kugawana na sio kugawiwa.
Kupeana na wala sio kupewa.

Wanasiasa wote Duniani wanatabia zinazofanana, Hawana tungo isemayo; Kesho yangu ni bora kuliko leo.
Wao wananeno moja tuu, nalo ni; Leo ni leo asemaye kesho muongo.
Wanasiasa wanamsimamo wa tumalizane leoleo, kila mtu achukue chake leo, mambo ya kesho yatajijua yenyewe.

Wakiwa mbele za watu watasema, Mradi au mpango huu utaleta tija miaka kumi ijayo" ilhali wao wananufaika na mpango huo Leo hii,

Ni Kama Siasa za wachungaji na waganga wajanja, atakuambia Akuombee na mwaka ujao utafanikiwa tuu! Lakini wao watakuambia uwape pesa Leo hiyohiyo. Hiyo ni Siasa, janja janja na utapeli uliohalalishwa.

Watanzania wenzangu sijui nilikuwa nazungumzia nini, hapa nimeshajichanganya.
Ila niseme tuu; Kujitenga na Siasa ni kujitenga na maisha mazuri ya Dunia.
Kukimbia maslahi yako na familia yako.

Nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Mkuu, umejadili suala lenye mantiki kubwa sana.
 
Mashoga hao

In ney wamitego voice
 
Umesema kweli siasa ndiyo inaamua maisha yetu ya kila siku, hasa wasomi wajinga wa kibongo wanajifanya hawataki siasa ndiyo maana CCM inateua mpk maDC walioishia F3 ni aibu sn
 
Kama maendeleo ni kuzunguka sana nje ya nchi, hiyo nchi ya Oman kiongozi wao mkuu huwa anafanya ziara wapi?
 
Unatuchanganya mpwa, juzi kuna thread yako umeandika "ili ufankiwe kwny biashara inabidi upate kibali kutoka kwa Mungu au Shetani. Leo hii unatuambia biashara ni bahati sasa tushike lipi ?

Back to the point,,,,,,,watanzania wengi hawajihusishi na siasa kwa sababu ya ugumu wa maisha mda mwngi mtu anatumia kutafta riziki. Mfano mtu kama machinga au mamantilie au bodabod anapata wapi mda wa kufatilia siasa?

Wengne hawajihusish na siasa ili kukwepa maumiv ya kihisia kwa saabu "Its very bad to be correct when the government is wrong" yaan we kila sku unaskia mara sjui tumepokea mkopo trilion kadhaa lakn huon chochote cha maana kinachofanyika

Unaangalia news hv unakuta kiongozi fulani anasifiwa asubuh mpaka majogoo lakn ukitafakari kwa undani unajiuliza huyu wanamsifia nn? Mbna hakuna anchofanya zaid ya kusafiri nje ya nchi kila sku huku bei za bidhaa zikipanda kila sku na maisha kuzd kuwa magumu? Just assume kipande cha sabun saiz ni 800 yaan khaaa afu kuna mtu yy kila kukicha ni kupanda ndege unajiuliza what f*uck is she???

Ukireact unashitakiwa kwamba ww ni mchochez, yan unajikuta unabaki na internal conflict ambayo u cant solve in any means sasa ili kuepuka yote hayo unaamua kuachana na siasa

Mfano mm nshaachaga mda sana kusikiliza taarifa za habar mana naona wanasifiana tu
 
Unatuchanganya mpwa, juzi kuna thread yako umeandika "ili ufankiwe kwny biashara inabidi upate kibali kutoka kwa Mungu au Shetani. Leo hii unatuambia biashara ni bahati sasa tushike lipi ?

Back to the point,,,,,,,watanzania wengi hawajihusishi na siasa kwa sababu ya ugumu wa maisha mda mwngi mtu anatumia kutafta riziki. Mfano mtu kama machinga au mamantilie au bodabod anapata wapi mda wa kufatilia siasa?

Wengne hawajihusish na siasa ili kukwepa maumiv ya kihisia kwa saabu "Its very bad to be correct when the government is wrong" yaan we kila sku unaskia mara sjui tumepokea mkopo trilion kadhaa lakn huon chochote cha maana kinachofanyika

Unaangalia news hv unakuta kiongozi fulani anasifiwa asubuh mpaka majogoo lakn ukitafakari kwa undani unajiuliza huyu wanamsifia nn? Mbna hakuna anchofanya zaid ya kusafiri nje ya nchi kila sku huku bei za bidhaa zikipanda kila sku na maisha kuzd kuwa magumu? Just assume kipande cha sabun saiz ni 800 yaan khaaa afu kuna mtu yy kila kukicha ni kupanda ndege unajiuliza what f*uck is she???

Ukireact unashitakiwa kwamba ww ni mchochez, yan unajikuta unabaki na internal conflict ambayo u cant solve in any means sasa ili kuepuka yote hayo unaamua kuachana na siasa

Mfano mm nshaachaga mda sana kusikiliza taarifa za habar mana naona wanasifiana tu

Unaposema bahati unazungumzia mambo ya Imani,
Bahati hutoka Kwa Mungu au Kwa Shetani

Unajiingiza huko sio kuwa msikilizaji au mtazamaji wa Siasa ukadhani ndio umeingia kwenye Siasa.

Epuka kuwa Mshabiki kwenye Siasa. Utaumizwa mpaka ukome.

Ingia kwenye vita, aidha uumize au uumizwe
 
Unaposema bahati unazungumzia mambo ya Imani,
Bahati hutoka Kwa Mungu au Kwa Shetani

Unajiingiza huko sio kuwa msikilizaji au mtazamaji wa Siasa ukadhani ndio umeingia kwenye Siasa.

Epuka kuwa Mshabiki kwenye Siasa. Utaumizwa mpaka ukome.

Ingia kwenye vita, aidha uumize au uumizwe
CCM imeharibu nchi sn
 
Back
Top Bottom