Watanzania wengi hawajui madhara ya usafirishaji haramu wa binadamu (human trafficking). Elimu izidi kutolewa

Watanzania wengi hawajui madhara ya usafirishaji haramu wa binadamu (human trafficking). Elimu izidi kutolewa

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Jana tarehe 14/08/2023 kupitia ukurasa wa ITV nimesoma habari ya kukamatwa kwa wahamiaji haramu huko Katavi waliokuwa wakisafirishwa kupitia tenki la mafuta. Ni habari ya kutisha sana. Kilichonitisha zaidi ni baada ya kusoma comments.

Kiufupi ni kuwa watu wengi wamelaumu mtu aliyewapa taarifa polisi hadi kufanikisha kukamatwa kwa watu hao. Baadhi wamediriki kusema kuwa dereva hana kosa bali ilikuwa ni jitihada za kutafuta riziki.

Madhara ya human trafficking ni mengi ila kubwa zaidi ni vifo. Watu wengi sana wanapoteza maisha kwenye hili jambo. Mchakato wake sio wa kibinadamu kabisa hivyo naunga mkono jitihada zinazofanyika kuzuia.

Ninasihi mamlaka zinazohusika kuendelea kutoa elimu kuhusiana na hili kuanzia shule za msingi.

 
Jitihada za kuzuia icho kitu ziende samabamba na kukuza uchumi wa nchi husika, bila hivyo ni kujisumbua bure.
sababu wote wanaofanya ivyo ni kukimbia Hali mbaya za uchumi zilizopo katika nchi zao.
 
Jitihada za kuzuia icho kitu ziende samabamba na kukuza uchumi wa nchi husika, bila hivyo ni kujisumbua bure.
sababu wote wanaofanya ivyo ni kukimbia Hali mbaya za uchumi zilizopo katika nchi zao.
Cha kushangaza World Bank inaitaja Ethiopia kama mojawapo ya nchi imara kiuchumi Afrika ikizidiwa na nchi chache mno.
 
Back
Top Bottom