Hyrax
JF-Expert Member
- May 20, 2023
- 964
- 2,675
Kuna ka-reserch nimekafanya kwa muda kidogo kuhusu tabia za watanzania na kugundua kuwa watanzania wengi wana tabia ya kuzubaa, akili kama inachelewa kuload, kuchelewa kufikiri na kutofanya maamuzi kwa usahihi na kwa ufanisi, Ninachelea kusema kwamba maisha ya watanzania ni mabovu kwasababu ya uzubavu wa akili, hata matatizo mengi yanayohususiana na ukatili wa kila namna kwenye jamii shida inaanzia kwenye uzubavu wa akili za watanzania wengi, Naomba watalaamu wa afya mnisaidie kuelewa tatizo hili kama shida ni chakula tunachokula, maji tunayokunywa au maisha tunayoishi. ?