Watato wakiniona huwa wanacheka sana na kunizoea hata niwe mkali

Watato wakiniona huwa wanacheka sana na kunizoea hata niwe mkali

Mimi kipindi sijajaaliwa mtoto walikua wananifuata ndani wanasema tugaiye mwanao tukacheze nae nikisema sina mtoto wananiambia muongo umemficha.


Ila wale ni malaika kama unawapenda ndan ya nafsi yako ata umuoneshe ukali hajali ila nafsi ikiw huwapendi hawatokusogelea watoto wapo kama mnyama ukimpenda atakupenda mala 1000.
 
Mimi kipindi sijajaaliwa mtoto walikua wananifuata ndani wanasema tugaiye mwanao tukacheze nae nikisema sina mtoto wananiambia muongo umemficha.


Ila wale ni malaika kama unawapenda ndan ya nafsi yako ata umuoneshe ukali hajali ila nafsi ikiw huwapendi hawatokusogelea watoto wapo kama mnyama ukimpenda atakupenda mala 1000.
Umefuga midev au....ila moyo wak ni saf mtoto anajua huwa anamacho kama X-ray anajua yupo mwema wake na mmbaya

Hahaha,
Watoto bwana!Halafu wakiona huwafanyi kitu wanakuonea sana!
 
Wasalaam.
Kumekuwa na kawaida sana kwamba watoto wadogo wakiniona wananiangalia sanaaaaa.
Halafu baadae wanaanza kucheka kweli kweli. Hadi wazazi wao wanaanza kushangaa maana huwa hawachekagi hivyo sana. Siku nyingine nimekaa sehemu naingia tu nakuja katoto fulani kakike kamekuja kukaa karibu yangu kananiangalia sana usoni, baadae nikakapa simu yangu kakaanza kucheza Game ya Temple Run. Mama yake akaja pale kuniomba radhi na kuanza kukaraipia kwanini kanaazima simu za watu kasiowajua. Wale majirani zangu wakasema walihisi labda ni katoto kangu hivi. Nilimwambia mama yake mimi sina shida acheze tu, tukakaa nako pale kakacheza mpaka simu ikakata chaji. Kakaanza kunipigisha stori yani tumeongea nako hadi kakalala nikakabeba. Ile naondoka wacha kaanze kunililia ova kananijua yani.

Mara nyingi watoto huwa wanaanzanga kuniongelesha na kunizoea hadi nashangaa sana.
Sasa juzi nidyo nimeishiwa na nguvu, nimekaa kwenye mstari wa hospitali nikaona kajaa fulani kana kama mwaka moja hivi. Yaani kadogo balaa (Andunje) kakamuacha maza wake kakanifuata pale nilipokuwa nimekaa, kakaniangalia kwa muda mrefu kweli halafu baadae kakaanza kucheka kama mtu mzima. Kalicheka hadi kanakaa chini, watu pale hawana mbavu wanaanza kuniangalia mimi hadi nkajistukia yani. Hii sii mara ya kwanza yaani sijui kuna nini kati yangu mimi na hivi vijamaa.

Nikiweka sura ya ukali ili kuvifukuza nidyo kabisaa vinazidi kucheka,
Yaani hata niwe mkali vipi vyenyewe hivyo mwilini. Mara kinivute sharubu, mara kinivue miwani.
Hiki kiko na andazi lake kinataka kunilisha na mimi yaani vurugu ova vinanijua atiii.
Yaani sijuia vinaniona mimi nimekaa kama likatuni fulani.
Inawezeakana unafanana na huyu h
26749dbfce8717abddb9eccceb54851e.jpg
apa
 
Mimi nasumbuliwa na vitoto vya majirani zangu hapa,yaani sijui hata vinanipendea nini maana vikiniona tu vinaniganda mpaka naenda navyo kwangu,sometime vinaanza kulialia viletwe kwangu na mimi muda huo nataka kupumzika basi tabu tu! Na vikija kwangu wala havitulii utavisikia tu jirani leo mi nalala hukuhuku kwako!
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mpe Mola shukran kwa baraka zake jombaa. Wengine wetu mitaani watoto wakikataa kula chakula huwa wanatishiwa na mama zao kwamba wataitiwa jirani. Wakisikia hivo tu hapo sasa ndo huwa wanaanzaga kumeza vijiko vinne vinne kwa mpigo. Afu kikombe cha maziwa wanakichapa flush. 😀😀😀
 
Mpe Mola shukran kwa baraka zake jombaa. Wengine wetu mitaani watoto wakikataa kula chakula huwa wanatishiwa na mama zao kwamba wataitiwa jirani. Wakisikia hivo hapo sasa ndo huwa wanaanzaga kumeza vijiko vinne vinne kwa mpigo. Afu kikombe cha maziwa wanakichapa flush. 😀😀😀
Hahahahhaha!
Hii hata mimi nilikuwa nafanyiwa sana!
 
Hawajakuvunjia miwani mkuu?

Mimi ni opposite. Watoto hawaivani na mimi kabisa na napenda iendelee hivyo.
 
Back
Top Bottom