Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,843
- 31,057
Nimekuwa nikijiuliza Katika mazingira ya nchi yetu, iliyobarikiwa na Mungu, rasilimali za kila aina, kama vile, gesi, madini ya kila aina, ardhi yenye rutuba, inayoweza kustawisha mazao ya biashara na chakula kwa kipindi chote cha mwaka.
Hivi Katika mazingira hayo, ndiyo watawala wetu wameona njia moja pekee, ya kutukamua kwa tozo za Kila aina wananchi wake, hadi tuna-suffocate??
Kwa kufafanua zaidi mada yangu ni kuwa bei za mafuta ya Petroli, hapa nchini, haishikiki na imeleta taharuki kubwa Sana Katika nyanja mbalimbali za usafiri za uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, Hadi kutokelezea kupanda kwa bidhaa Karibu zote.
Japo tunafahamu kuwa kupanda huko kwa bei ni kwa Dunia nzima, hata hivyo mataifa mbalimbali yamechukua hatua za dharura za kuondoa tozo kwenye mafuta hayo na Serikali yenyewe kuchukua hatua za ziada kwa ku-subsidize, Ili bei hizo zisiweze kuwaumiza wananchi wao masikini.
Hebu tuchukulie mfano wa nchi jirani za Zanzibar na Kenya, ambazo aidha zimefuta tozo mbalimbali za kwenye mafuta au zime-subsidize bei ya watumiaji wa mafuta hayo.
Mfano ni nchi "jirani" yetu ya Zanzibar, ambayo wananchi wake wameendelea kununua mafuta kwa shilingi 2,600 wakati sisi watanganyika tukikwamuliwa kwa zaidi ya shilingi 3,100!
Nakuwa nikijiuliza, hivi inakuwaje kwa baadhi ya viongozi wetu, wakitamba kwenye majukwaa ya kisiasa kuwa nchi yetu ni tajiri Sana, Hadi tunaweza kuwa "donor county"Hadi kwenye hizo nchi za magharibi, zinazotamba kuwa ni matajiri wa Dunia??
Ni hayo tu maoni yangu machache kwa watawala wetu.
Hivi Katika mazingira hayo, ndiyo watawala wetu wameona njia moja pekee, ya kutukamua kwa tozo za Kila aina wananchi wake, hadi tuna-suffocate??
Kwa kufafanua zaidi mada yangu ni kuwa bei za mafuta ya Petroli, hapa nchini, haishikiki na imeleta taharuki kubwa Sana Katika nyanja mbalimbali za usafiri za uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, Hadi kutokelezea kupanda kwa bidhaa Karibu zote.
Japo tunafahamu kuwa kupanda huko kwa bei ni kwa Dunia nzima, hata hivyo mataifa mbalimbali yamechukua hatua za dharura za kuondoa tozo kwenye mafuta hayo na Serikali yenyewe kuchukua hatua za ziada kwa ku-subsidize, Ili bei hizo zisiweze kuwaumiza wananchi wao masikini.
Hebu tuchukulie mfano wa nchi jirani za Zanzibar na Kenya, ambazo aidha zimefuta tozo mbalimbali za kwenye mafuta au zime-subsidize bei ya watumiaji wa mafuta hayo.
Mfano ni nchi "jirani" yetu ya Zanzibar, ambayo wananchi wake wameendelea kununua mafuta kwa shilingi 2,600 wakati sisi watanganyika tukikwamuliwa kwa zaidi ya shilingi 3,100!
Nakuwa nikijiuliza, hivi inakuwaje kwa baadhi ya viongozi wetu, wakitamba kwenye majukwaa ya kisiasa kuwa nchi yetu ni tajiri Sana, Hadi tunaweza kuwa "donor county"Hadi kwenye hizo nchi za magharibi, zinazotamba kuwa ni matajiri wa Dunia??
Ni hayo tu maoni yangu machache kwa watawala wetu.