Watoto wengi wanakutwa na Saratani iliyofikia hatua mbaya

Watoto wengi wanakutwa na Saratani iliyofikia hatua mbaya

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani na Damu kwa Watoto kutoka Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dkt. Heronima Kashaigil amesema kuwa watoto 5 hadi 7 wanahudhuria Kliniki ya matibabu ya Saratani kila siku, sawa na watoto 250 kwa mwezi.

Utafiti uliofanywa na Shirika la ICCARE Tanzania ulibaini wagonjwa wengi waliokuwa wanafika Bugando kupata matibabu ya Saratani walikuwa wanaishia kwenye dozi ya kwanza kutokana na gharama za kusubiria matibabu kuwa juu ambapo wengi wao hukatisha matibabu na kufariki.

Kutokana na hali hiyo Hospitali ya Bugando imewataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto Hospitalini kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya Saratani ili waanze matibabu mapema.
 
Taka chafu kutoka kwenye migodi, Dawa za kuhifadhia maiti..shida sana
 
Kanda ya ziwa wengi wakiona hali ya kuumwa wanatumia kwanza mitishamba au kwenda kwa wataalamu mambo yakiharibika kabisa ndo wanawaleta wagonjwa hosptal haswaa watoto na wakiwa stage mbaya sana ambayo kuishi inakua asilimia ndogo mno.
 
https://doi.org/10.1016/j.scitotenv.2012.07.019 ..... The results suggested an association between risk of dying due to digestive, respiratory, hematologic and thyroid cancers and proximity to Spanish mining industries. These associations were dependent on the type of mine.
 
Sumu zote za migodini huko kanda ya ziwa ndio chanzo cha saratani. Huo ndio ukweli.

Maji, vyakula, samaki, mbogamboga n.k vyote vina kemikali za hatari za kuchochea saratani.


Sumu za migodini nyingi ni carcinogenic na zina heavy metals mbalimbali. Sasa hayo majimaji na uchafu yanaelekezwa kwenye vyanzo vya maji na sumu nyengine zinatunzwa kwenye mabwawa ambayo masumu yanapenya kidogokidogo kwenye ardhi mpaka kwenye vyanzo vya maji, mito,ziwani na visima vya chini ya ardhi vya maji.


Huko mbeleni kanda ya ziwa patakuwa na wagonjwa wengi sana wa kansa.


Ila wataalam wakipewa rushwa wanasema ni mavi ya ng'ombe 😂😂😂
 
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani na Damu kwa Watoto kutoka Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dkt. Heronima Kashaigil amesema kuwa watoto 5 hadi 7 wanahudhuria Kliniki ya matibabu ya Saratani kila siku, sawa na watoto 250 kwa mwezi.

Utafiti uliofanywa na Shirika la ICCARE Tanzania ulibaini wagonjwa wengi waliokuwa wanafika Bugando kupata matibabu ya Saratani walikuwa wanaishia kwenye dozi ya kwanza kutokana na gharama za kusubiria matibabu kuwa juu ambapo wengi wao hukatisha matibabu na kufariki.

Kutokana na hali hiyo Hospitali ya Bugando imewataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto Hospitalini kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya Saratani ili waanze matibabu mapema.
Hatari hii!!
 
Lakini, mbona kama kasi ya cancer inaenda kasi kila mahala? Nina watu wangu watatu wa karibu ndani ya muda mfupi hapa dar na mkoani wamekutwa na cancer, na wawili wameshaondoka, aliyebaki wamempa maximum kuishi ni miezi miwili-Kiukweli napata wasiwasi sana.
 
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani na Damu kwa Watoto kutoka Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dkt. Heronima Kashaigil amesema kuwa watoto 5 hadi 7 wanahudhuria Kliniki ya matibabu ya Saratani kila siku, sawa na watoto 250 kwa mwezi.

Utafiti uliofanywa na Shirika la ICCARE Tanzania ulibaini wagonjwa wengi waliokuwa wanafika Bugando kupata matibabu ya Saratani walikuwa wanaishia kwenye dozi ya kwanza kutokana na gharama za kusubiria matibabu kuwa juu ambapo wengi wao hukatisha matibabu na kufariki.

Kutokana na hali hiyo Hospitali ya Bugando imewataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto Hospitalini kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya Saratani ili waanze matibabu mapema.
Hii ni hatari sana kwa jamii Mungu wetu aingilie kati

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Ukilinganisha habari ya kwanza kuhusu samaki, halafu inafatia hii, kuna uhusiano wowote?
tunatisha sana kwa kweli
 
Sumu zote za migodini huko kanda ya ziwa ndio chanzo cha saratani. Huo ndio ukweli.

Maji, vyakula, samaki, mbogamboga n.k vyote vina kemikali za hatari za kuchochea saratani.


Sumu za migodini nyingi ni carcinogenic na zina heavy metals mbalimbali. Sasa hayo majimaji na uchafu yanaelekezwa kwenye vyanzo vya maji na sumu nyengine zinatunzwa kwenye mabwawa ambayo masumu yanapenya kidogokidogo kwenye ardhi mpaka kwenye vyanzo vya maji, mito,ziwani na visima vya chini ya ardhi vya maji.


Huko mbeleni kanda ya ziwa patakuwa na wagonjwa wengi sana wa kansa.


Ila wataalam wakipewa rushwa wanasema ni mavi ya ng'ombe [emoji23][emoji23][emoji23]
SIO KWELIII!...EVIDENCE TAFADHALIII!!!!
 
Back
Top Bottom