Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali ya Lori na Hiace mkoani Tabora

Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali ya Lori na Hiace mkoani Tabora

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
1730985839627.png
Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari ya abiria dogo aina ya Toyota Hiace kuligonga lori kwa nyuma wilayani Nzega mkoani Tabora leo Alhamisi Novemba 7, 2024.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.


================

Watu 14 wamefariki Dunia na wengine 9 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari ya abiria aina ya Toyota Hiace yenye namba T562 DGG ambalo imeligonga Mistubishi Fuso T361 CSB kwa nyuma Wilayani Nzega, leo Novemba 7, 2024.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amesema Dereva wa Toyota bado hajafahamika kwa kuwa alikimbia baada ya tukio hilo na chanzo cha ajali imebainika ni uzembe wa dereva wa Hiace alipokuwa akijaribu kulipita Lori na kuligonga kwa nyuma.

Waliofariki Wanaume ni 8, Wanawake 4 na Watoto wenye umri chini ya umri wa mwaka mmoja (wawili).
 
View attachment 3146171
Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari ya abiria dogo aina ya Toyota Hiace kuligonga lori kwa nyuma wilayani Nzega mkoani Tabora leo Alhamisi Novemba 7, 2024.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Madereva wa magari ya abiria wawe na minimum education japo form VI, hii mambo itakwisha!
 
Hi ni breaking news nimeiona pale Mwananchi kwamba watu 14 wamepoteza maisha baada ya gari la abiria dogo la aina ya Toyota Hiace kugonga lori kwa nyuma wilayani Nzega, mkoani Tabora, hii leo, Alhamisi, Novemba 7, 2024.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Richard Abwao, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

So far updates zaidi zinasubiriwa.

Mwananchi 2.png

Source: Mwananchi
 
Overspeeding ni janga kwa madereva wetu - hilo somo la defensive driving limekuwa gumu sana kwao.

Sasa ni wakati wa kutunga sheria kali kati ya wamiliki kuhakikisha magari yao ni salama na Dereva kuhakikisha anafuata sheria barabarani ikiwepo hili sugu la over speeding.

Akisababisha na akapona basi kifungo miaka 30 ama maisha jela imuhusu dereva huyu mzembe.
 
Back
Top Bottom