Watu 4 wanaotuhumiwa ‘kutumwa na afande’ kumlawiti na kumbaka binti mkazi wa Yombo Dovya Mkoani Dar, Wafikishwa Mahakamani

Watu 4 wanaotuhumiwa ‘kutumwa na afande’ kumlawiti na kumbaka binti mkazi wa Yombo Dovya Mkoani Dar, Wafikishwa Mahakamani

Walipaswa kuonyeshwa sura zao zionekane live jamii iwaone hao binadamu wajinga na wapumbavu.

Siku zote wanazopelekwa mahakamani sura zao zionyeshwe kwenye vyombo vya habari.

Serikali iwakamate haraka watuhumiwa wengine akiwepo mmoja ambaye hayupo hapo na bosi wao aliyewatuma
 

Hapa kuna tafsiri ya maandishi yako kwa Kiswahili:

Ushahidi wa kielektroniki unakubalika kwa mujibu wa
Sheria ya Miamala ya Kielektroniki ya mwaka 2015.
Kifungu cha 18 cha Sheria ya Miamala ya Kielektroniki kinaeleza kuwa ili ushahidi wa kielektroniki ukubalike mahakamani kama kielelezo, kinachohitajika kuthibitishwa ni uaminifu wa ushahidi wa kielektroniki kuhusu jinsi rekodi ilivyorekodiwa na jinsi ilivyohifadhiwa hadi ilipoletwa mahakamani kama ushahidi.

Shahidi anayetarajia kutoa ushahidi wa kielektroniki lazima kwanza aonyeshe ushahidi unaoondoa uwezekano wa kudanganywa kwa ushahidi wa kielektroniki kabla ya kuwasilisha.
Kabla ya kuwasilisha ushahidi wa kielektroniki, shahidi anapaswa kuridhisha Mahakama kwa ushahidi kwamba ushahidi wa kielektroniki unaotarajiwa kuwasilishwa ni halisi. Hii inafanywa kwa kuthibitisha hali ya kiufundi ya kifaa wakati wa kurekodi, jinsi rekodi ilivyofanywa, na nani aliyeifanya na kuhifadhi hadi ushahidi ulipowasilishwa mahakamani.

Ikiwa rekodi ya kielektroniki ilibadilishwa kuwa vyombo vya sekondari kama flash, njia ya kubadilisha kuwa vyombo vya sekondari pia inapaswa kuthibitishwa.

Asante sana japo sehemu nyingine imekuwa tafsiri sisisi.
 
kuna madai kuwa mwanamke huyo alikuwa anajiuza, yaani kazi yake ni ukahaba.
kama ni hivyo basi hapo hamna kesi.
labda washitakiwe kwa kosa la kusambaza picha za ngono.
 
Watu wanne wanaotuhumiwa ‘kutumwa na afande’ kumlawiti na kumbaka binti mkazi wa Yombo Dovya, jijini Dar es Salaam leo Jumatatu Agosti 19, 2024 wamefiksihwa mahakamani na kusomewa mashktaka mawili.

Watuhumiwa hao wamefikishwa katika Mahakama ya Kanda Dodoma na kusomewa mashtaka ya kubaka kwa kikundi (gang rape) na kumwingilia kinyume na maumbile binti ambaye hakutajwa jina lake mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania mkoani Dodoma, Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Mashtaka Makao Makuu, Renatus Mkude amesema vijana hao wamekana mashtaka hayo na kutokana na unyeti wa shauri hilo wataendelea kuwa mahabusu.

Watuhumiwa hao waliofikishwa mahakamani ni MT. 140105 Clinton Honest Damas maarufu Nyundo, Amin Lord Lema, Nickson Idala Jackson na C.1693 Playgod Edwin Mushi

Kwa mujibu wa taarifa ya Renatus Mkude, Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka amesema kesi hiyo itasikilizwa kwa siku tano kuanzia leo Agosti 19 hadi Agosti 23 siku ya Ijumaa.

Pia soma:

1. Polisi yaanza kufuatilia tukio la Binti aliyebakwa na wanaume watatu

2. Watuhumiwa wa mande ya Ubakaji na ulawiti waliotumwa na afande wakamatwa
Tunamtaka aliewatuma hao vibaka
 
Kwani yule RC aliyefikishwa mahakamani kwa kesi ya ubakaji kulikuwa na video? Binti si ndiye aliyetendewa? Binti si ndiye aliyeenda kushitaki? Video(Picha jongefu) au CCTV footage ni just a supporting evidence tu na wala mahakama hawatorelay na hizo clips ,watarelay na maelezo ya Binti maana yeye ndiye aliyelawitiwa na madaktari watathibitisha kama kweli binti aliingiliwa.


Kesi hazifanani. Kila kesi huamuliwa kulingana na muktadha wake.

Kesi ya RC na ya Binti wa Yombo zina utofauti, na hivyo maamuzi yake hayawezi kufanana na wala huwezi kuchukua uamuzi wa kesi hizi mbili kama kitu kimoja.

Kwanza kesi moja ni ulawiti pekee wakati nyingine ni ubakaji wa kundi (gang rape na ulawiti).

Halafu kuwa na ushahidi ni jambo moja, na kuuthibitisha* ushahidi ni jambo lingine.
 
Kesi hazifanani. Kila kesi huamuliwa kulingana na muktadha wake.

Kesi ya RC na ya Binti wa Yombo zina utofauti, na hivyo maamuzi yake hayawezi kufanana na wala huwezi kuchukua uamuzi wa kesi hizi mbili kama kitu kimoja.

Kwanza kesi moja ni ulawiti pekee wakati nyingine ni ubakaji wa kundi (gang rape na ulawiti).

Halafu kuwa na ushahidi ni jambo moja, na kuuthibitisha* ushahidi ni jambo lingine.

Nazungumzia video kama ndiyo hoja ya kuwatia hatiani ,hizo kesi ni tofauti kabisa...video ni supporting evidence tu ,kesi nyingi za waliofungwa miaka thalatha za ubakaji hazina video so hoja ya kuthibitisha kwenye video siyo ya msingi sana maana kuna watu wamefungwa kwa kesi za ubakaji na wala kulikuwa hakuna video clip.
 
Nazungumzia video kama ndiyo hoja ya kuwatia hatiani ,hizo kesi ni tofauti kabisa...video ni supporting evidence tu ,kesi nyingi za waliofungwa miaka thalatha za ubakaji hazina video so hoja ya kuthibitisha kwenye video siyo ya msingi sana maana kuna watu wamefungwa kwa kesi za ubakaji na wala kulikuwa hakuna video clip.

Hoja ya uthibitisho wa video ni ya msingi kwa sababu maelezo ya historia ya kesi, ushahidi muhimu ni wa video.
 
Back
Top Bottom