Watu wa Dar acheni kuwatelekeza ndugu zenu stendi

Eti kabisa mlongo wangu kapanda Super Feo mpaka Magufuli halafu mi nimzimie simu? haiwezekani
Naanzajee kwani? Nishawahi mpokea jirani wa mtaani kwetu, alikujaga kwa interview, baada ya kukosa alio wa target, akaibukia kwangu.

Ananambia yuko mbezi stand, afu ilikua saa 6, nilimuelekeza akodi Boda anikute Shekilango, alikaa kwangu siku 4.

Leo yuko hapo Kurasini kazin, hasahau ule wakati, kuna tyme huwa ananitoa kwa muamala wa kunywa Fanta ya baridiii, sometimes namtembelea kwake.
 
Wema hauozi hakika!
 

[emoji1787][emoji1787][emoji1787] jamani
 
Tabia mbaya sana
 
Me waje napenda sana ndugu maana no mvivu, ko hapo nishapata wa kunisaidia kazi zangu.
Na watu wa bush wanapiga kazi
 
Hakuna ndugu mwenye akili akatelekeza ndugu kituoni hao wanaokwambia ni waongo tu.

NAKUPA KISA.

Napenda sana kusafiri usiku,kuna siku nikawa natoka Tanga kuja Dar basi kwenye siti nikabahatika kukaa na dada mmoja hivi.

Hatukuwa na story kwan ninapikuwa kweny gari napenda kulala,sasa tulivyofika Chalinze yule dada akaanza wasiliana na mtu ambae yupo dar,wakawa wanaelekeza ashuke kati ya mbezi au kibamba sikumbuki vizuri.

Baada ya muda simu ikawa haipatikani mpaka tunafika ubungo simu haipatikani ndio akaanza kunung'unika huku mm nikaona nikae nae mbali kabisa maana mwisho wa siku ataomba hifadhi.

NB;HAKUNA NDUGU MWENYE AKILI AKATELEKEZA NDUGU YAKE,WENGINE WANAKUJA KUJILIPUA KUTAFUTA MAISHA ILA KISINGIZIO WAMETELEKEZWA NA NDUGU.
 
Umaskini
Uchoyo
Ubinafsi
Roho mbaya.

Vs

Upendo
Ukarimu
Roho safi

Acha waje, muhimu wafuate kanuni na sheria za hapo kwako.
Mtakachopata Mtakula hichohicho.

Atakayevunja kanuni na sheria za hapo nyumbani atakuwa amejitakia kuondoka.

Lakini maisha magumu yasiwe Sababu ya kusaidia au kupokea ndugu zako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…