Watu wa Kaskazini watoka kifungoni; Moshi na Arusha zarejea kwenye hadhi tuliyozoea kabla ya 2016. Watu wanashangweka ile ile!

Watu wa Kaskazini watoka kifungoni; Moshi na Arusha zarejea kwenye hadhi tuliyozoea kabla ya 2016. Watu wanashangweka ile ile!

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Baada ya akina Gambo, Sabaya, Mneti, Muro, na viongozi wengine kutowesha amani na furaha ya Xmas Kaskazini kwa kisingizio cha kulinda amani na kuepusha vurugu hatimaye mwaka huu tunaona Ndugu zetu kwa mara nyingine wakirejea makwao Kwa furaha huku biashara zikipamba moto.

Ni kama wamepata Uhuru ulioibwa na baadhi ya watu walioaminishwa kwamba ukanda flani ni watu wasiopaswa kufurahi huku hata biashara zikitakiwa zimilikiwe na watu wa mrengo flani tu na ukitaka kufungua biashara ukiwa na mrengo tofauti basi utafilisiwa au kufanywa vyoVyote uondoke sokoni.

Nimpongeze Mama kwa kufuta ukiritimba wa akina Sabaya na akina Jeryy Muro na vikosi vyao, nimwombe atuwekee utaratibu mzuri wa kikatiba utakaozuia yaliyopita yasijirudie tena.

Akina Manka kuleni maisha msiwasikilize wasiojua kutafuta, msiwasikilize wasiopenda kwao, msiwasikilize akina ishomire tunaokimbia makwetu na kuja kuwekwa lockdown huko Kwa watu. Vibe la Moshi lafaa kusindikizwa na bia tamu
 
Haki ya watu kuwa na furaha iliporwa na wahuni wachache. Tulisifu na kuabudu mungu mtu.
... halafu kesho na keshokutwa tuanze tena kusemasema; "oooh nchi kwa ilipofikia inahitaji dikteta!". Haya yalisemwasemwa 2011 - 2014 "tukaonjeshwa" kweli mfano wa dikteta; tusirudie tena kuropoka tusiyoyajua! Kuna member juu hapo kashauri upuuzi ule yafaa udhibitiwe kikatiba usijirudie tena!
 
Amdika la kishenzi na andiko la kutuonesha nyinyi ni wabaguzi haijawahi kutokea baba wa Taifa alishatuonya kuhusu tabia zenu
 
Hivi si kuna kipindi uliaga hapa jamvini unataka kuachia namba mkuu au siyo wewe?
 
... halafu kesho na keshokutwa tuanze tena kusemasema; "oooh nchi kwa ilipofikia inahitaji dikteta!". Haya yalisemwasemwa 2011 - 2014 "tukaonjeshwa" kweli mfano wa dikteta; tusirudie tena kuropoka tusiyoyajua! Kuna member juu hapo kashauri upuuzi ule yafaa udhibitiwe kikatiba usijirudie tena!
Mtu kwenda kwao isiwe ishu kwamba ni kitu kipya maana kila mtanzania ana kwao na wanaendaga pia sema wao hawaendi kwa mkupuo kwa muda fulani kama ambavyo watu wa kaskazini tunafanya.

Hii maneno ya madharau isiwe Sasa kwamba watu hawana kwao hata kama ni vijijini na hii ndio ilisababisha Magufuli aliweka jealous sana na kuona kila mwenye pesa ni mwizi au kila anayeamua kula raha basi ni mwizi tu sababu kubwa ni wengi wakiwa na hela wanaanza kuletea madharau wengine na majigambo yasiyo na msingi, sasa isisababishe atokee mwingine akachukia hii madharau.

Kumbuka hao tunaowaletea madharau ndio wateja wetu madukani wakiamua hawanunui bidhaa kwetu itakuwa shida wakiamua wanunue wao kwa wao Kama wanavyofanya wakinga na wahindi.

Mkataa kwao mtumwa, naamini kama watu wa kaskazini ndio utaratibu wetu basi tusiwadharau wengine hata kama ndio tunajua kusaka pesa Iau tunaamini hivyo la kila mtu amekuja mjini kusaka pesa ndio maana wakinga na wanyakyusa, wasukuma na wahaya wapo kimya tu nao Wana hela kibao tu na wakiamua kujiorganise kama ambavyo ilivyo pale Kariakoo sijui tutakimbilia wapi.
 
Wakilimanjaro ulimbukeni hautawaisha, yaani kama ni utamaduni wenu iweje Leo iwe kitu kigeni? Kweli ushamba hauna bei
 
Back
Top Bottom