Watu wa Musoma tukumbushane stori za Musoma kuanzia 2000-2010

Watu wa Musoma tukumbushane stori za Musoma kuanzia 2000-2010

Kurutu wa Mungu

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2017
Posts
366
Reaction score
578
Nakumbuka enzi hizo kwenda Disco Toto Tembo Beach kila sikukuu za Mwisho wa mwaka, Wasanii wakija Karume Stadium tunasubiria mda wa fungulia mbwa ndipo tuingie wakati kiingilio ni 1000 tu watoto.

Watu maarufu kama Tajiri mwenye mbwembwe Nyakiteri, Dereva wa mbio za magari Mama's, Hussein Sokoni, Redio yetu pendwa Victoria FM hapo utawakuta wakina Boke Wambura, Maregesi Girishon, Emmanuel Chibasa, Issa Nundu, mzee wa Mafua Robson Wangaso na wengineo, mitaa ya Nyasho hapo ndilo chimbo la kujipatia mavazi.

Fujo za Musoma Tech na Songe hadi kupelekea Songe kuwa ya wadada, Mitaa maarufu kama Mukendo, Iringo, Mwigobelo, Majita Road bila kusahau vibaka wa Magamaga, na kila likizo tunakutana tuition Mwembeni hapo utakutana na watoto wa Isenye, Ikizu na sisi wa Bweri Makatani.
 
Mass town mwaka 2005 yalianzishwa makundi ya vijana kwa ajili ya kampeni za siasa vijana wapige kura kuanzia miaka 18 mpaka 30 muasisi akiwa mgombea ubunge ccm. Baada ya kampeni kuisha tu hilo kundi la WEST LAWAMA likageuka na kua kundi la wahuni wavuta bangi vibaka na waanzisha fujo musoma.mjini.ilipofika mwaka 2007 yaliibuka makundi ya vijana mengi sana karibia kila kata inakundi lake la kufanyiana fujo na makundi ya mitaa mingine:

1. USWAZI kata ya kamyonge mpaka mkendo, iringo
2. MBIO ZA VIJITI kata ya nyakoto na kigera
3. MDOMO WA FURU kata ya nyamatare
4. WABEPARI kata ya mwisenge

Ilifika kipindi wakawa musoma nzima wanafunzi wengi wako kwenye makundi ya uhuni. Siku za sikukuu hasahasa complex na tembo beach lazima mzike uzimwe mapema kisa fujo za haya makundi hasimu MBIO NA USWAZI . Tulishudia mapanga live kama picha za wahindi. Ilifika kipindi wakawa wanafungiana maeneo ya kutembea kama vile nyasho ikotokea umekutana nao we kimbua tu utapigwa lugoe.

Kuna vijana walikua maarufu sana enzi hizo kwa ubabe na uhuni kama vile Kasinia na wengine wengi nishawasahau.
 
Mass town mwaka 2005 yalianzishwa makundi ya vijana kwa ajili ya kampeni za siasa vijana wapige kura kuanzia miaka 18 mpaka 30 muasisi akiwa mgombea ubunge ccm. Baada ya kampeni kuisha tu hilo kundi la WEST LAWAMA likageuka na kua kundi la wahuni wavuta bangi vibaka na waanzisha fujo musoma.mjini.ilipofika mwaka 2007 yaliibuka makundi ya vijana mengi sana karibia kila kata inakundi lake la kufanyiana fujo na makundi ya mitaa mingine:

1. USWAZI kata ya kamyonge mpaka mkendo, iringo
2. MBIO ZA VIJITI kata ya nyakoto na kigera
3. MDOMO WA FURU kata ya nyamatare
4. WABEPARI kata ya mwisenge

Ilifika kipindi wakawa musoma nzima wanafunzi wengi wako kwenye makundi ya uhuni. Siku za sikukuu hasahasa complex na tembo beach lazima mzike uzimwe mapema kisa fujo za haya makundi hasimu MBIO NA USWAZI . Tulishudia mapanga live kama picha za wahindi. Ilifika kipindi wakawa wanafungiana maeneo ya kutembea kama vile nyasho ikotokea umekutana nao we kimbua tu utapigwa lugoe.
Nadhani unamaanisha JAMAICA MOCKERS badala ya USWAZI.
 
Dah umenikumbusha musoma tech pale baruti kuna jamaa alikua anaonyesha movie kwenye kibanda umiza,jpili na jmosi zilikua zile xxx tukawa tunaita kikao ili kuweka tafsida,yani kuna mshikaji ilikua ikifika kumi na mbil jioni keshawahi kwenye kikao,daah noma sana enzi hizo
Aaaah haaaa haya maisha bwana
 
Mass town mwaka 2005 yalianzishwa makundi ya vijana kwa ajili ya kampeni za siasa vijana wapige kura kuanzia miaka 18 mpaka 30 muasisi akiwa mgombea ubunge ccm. Baada ya kampeni kuisha tu hilo kundi la WEST LAWAMA likageuka na kua kundi la wahuni wavuta bangi vibaka na waanzisha fujo musoma.mjini.ilipofika mwaka 2007 yaliibuka makundi ya vijana mengi sana karibia kila kata inakundi lake la kufanyiana fujo na makundi ya mitaa mingine:

1. USWAZI kata ya kamyonge mpaka mkendo, iringo
2. MBIO ZA VIJITI kata ya nyakoto na kigera
3. MDOMO WA FURU kata ya nyamatare
4. WABEPARI kata ya mwisenge

Ilifika kipindi wakawa musoma nzima wanafunzi wengi wako kwenye makundi ya uhuni. Siku za sikukuu hasahasa complex na tembo beach lazima mzike uzimwe mapema kisa fujo za haya makundi hasimu MBIO NA USWAZI . Tulishudia mapanga live kama picha za wahindi. Ilifika kipindi wakawa wanafungiana maeneo ya kutembea kama vile nyasho ikotokea umekutana nao we kimbua tu utapigwa lugoe.
Haaa haaa kasinia kaisha yupo anakunywa gongo tu huku majita road, na maeneo ya mwisenge kwenye vilabu choka mbaya kwao si ni hapo mkinyerero
 
Back
Top Bottom