Watu waliokataa Magufuli asiongezewe Miaka ndio haohao wanashadadia Mbowe aendelee kuongoza. Ndio haohao wanakapinga CCM isiendelee! Unafiki mtupu!

Watu waliokataa Magufuli asiongezewe Miaka ndio haohao wanashadadia Mbowe aendelee kuongoza. Ndio haohao wanakapinga CCM isiendelee! Unafiki mtupu!

Si umesema CHADEMA ni yawanachadema?
Na sio chama cha Watanzania.

Ndio nikakuambia kuwa madai ya wanaosema CHADEMA ni Saccos kumbe ni sahihi?

Unafikiri ni Kwa nini vyama vya upinzani vinapewa ruzuku?
Umeuliza CHADEMA ni SACCOS ya Mbowe
Kama umeona ni swali la kiwaki uliloulizaza ni SACCOS ya Mbowe, jibu swali nililokuuliza kazi za SACCOS ni zipi.
Halafu SACCOS zinaruhusiwa kufanya siasa katika nchi hii?
Je chama chochote au umoja ambo sio wa umma ni lazima iwe SACCOS??
 
Umeuliza CHADEMA ni SACCOS ya Mbowe?
Kama umeona ni swali la kiwaki uliloulizaza ni SACCOS ya Mbowe, jibu swali nililokuuliza kazi za SACCOS ni zipi.
Halafu SACCOS zinaruhusiwa kufanya siasa katika nchi hii?
Je chama chochote au umoja ambo sio wa umma ni lazima iwe SACCOS??

Maswali yako yanaonyesha CHADEMA ni Saccos iliyojificha kwenye siasa
 
Maswali yako yanaonyesha CHADEMA ni Saccos iliyojificha kwenye siasa
Basi ungekuwa na akili ungeipigia kelele serikali yako na kuitaka isipeleke pesa za walipa kodi kwenye SACCOS badala ya kutaka kuibadilisha SACCOS ya watu walioamua kujifanyia mambo yao wakati wewe sio mwanachama/mjumbe wa hiyo SACCOS.
 
Kwa kinachotaka kutokea ni mara Mia CCM
Najuta kupoteza muda wangu kuipambania CHADEMA miaka yote hii. Niliyakanusha ma-ccm yaliposema cdm ni saccos ya mtu.
Mtazamo wangu wa sasa. Heri tubaki na ccm tu. Zimwi likujualo .. kuliko zimwi jipya ambalo tayari limeonekana litang'ang'ania madaraka miaka 1000. Narudi kujituliza na Simba na Yanga. CCM KAMATIA HAPOHAPO. NA UCHAGUZI MKUU MWAKANI KAMA MWAKA HUU. SAFI SANA.
 
Najuta kupoteza muda wangu kuipambania CHADEMA miaka yote hii. Niliyakanusha ma-ccm yaliposema cdm ni saccos ya mtu.
Mtazamo wangu wa sasa. Heri tubaki na ccm tu. Zimwi likujualo .. kuliko zimwi jipya ambalo tayari limeonekana litang'ang'ania madaraka miaka 1000. Narudi kujituliza na Simba na Yanga. CCM KAMATIA HAPOHAPO. NA UCHAGUZI MKUU MWAKANI KAMA MWAKA HUU. SAFI SANA.

Acha uongo
 
Mkuu Robert Heriel Mtibeli mimi nakushauri tubaki kule kule kwenye kujadili mambo mengine tofauti na hizo siasa.

Kwa hali yetu hizi siasa, sawa ni haki na wajibu kuzijadili ila kwa ushamba wa wanasiasa wetu zinaleta uadui wa kijinga sana hadi kuhatarisha maisha wakati mwingine.

Mambo mengine haya ya kijamii ni rahisi tofauti zetu kuishia hapa hapa, kesho tukacheka.

Usalama wa kwanza ni kuhakikisha upo salama.
 
Najuta kupoteza muda wangu kuipambania CHADEMA miaka yote hii. Niliyakanusha ma-ccm yaliposema cdm ni saccos ya mtu.
Mtazamo wangu wa sasa. Heri tubaki na ccm tu. Zimwi likujualo .. kuliko zimwi jipya ambalo tayari limeonekana litang'ang'ania madaraka miaka 1000. Narudi kujituliza na Simba na Yanga. CCM KAMATIA HAPOHAPO. NA UCHAGUZI MKUU MWAKANI KAMA MWAKA HUU. SAFI SANA.
Tanzania mtu anaweza kumiliki SACCOS?

Mtu anatakiwa kufuata taratibu gani ili aweze kumiliki SACCOS binafsi?
 
Mpo salama!

Watu wenye ndimi mbili. Watu wenye mawe mawili ya kupimia ni watu Hatari Sana popote walipo. Ni watu wanafiki na muda wowote wanaweza kukuuza.

Alipokuwepo Magufuli, Chawa wake walitoa maoni Yao kuwa Magufuli aongezewe Muda, Magufuli atawale milele, na kama Magufuli angekataa wapo walioapa wangemshikia kiboko kumlazimisha aendelee kutawala. Yalikuwa ni maoni Yao.

Sisi wengine maoni yetu tulikataa tukasema Hapana. Miaka yake ikiisha inatosha. Wengine tukasema Katiba hairuhusu lakini Katiba ni kitabu tuu tunaweza kukibadilisha sehemu ndogo (Constitution amendment) ili kuweka kipengele cha kuongeza Muda.

Haya walewale ambao waliwaka, walimkalia kooni JPM ambaye yeye mwenyewe hata hakuwahi kusema ataongeza Miaka zaidi ya yeye kutamka hataongeza Miaka. Leo hii kile walichokuwa hawakitaki kwa JPM wanakifanya kwenye chama Chao.

Mbowe hata angekuwa kiongozi mzuri kama Malaika, kumuongezea Miaka mingine juu ya ishirini sio Sawa.

Alafu Mbowe angetakiwa aonyeshe uzuri wake katika kuandaa viongozi wengine wazuri zaidi yake wa kumrithi.

Siongei kumtetea Lisu awe kiongozi nope! Anaweza kugombea mtu mwingine Nje ya Lisu na akawa kiongozi wa CHADEMA hii itaonyesha kuwa CHADEMA inaakiba ya kutosha ya viongozi.

Kama kuna watu wanaona Mbowe aendelee Basi wasishangae wale wanaoona CCM iendelee.

Wanasema Mbowe kaitoa CHADEMA Mbali.
Watu wanasema CCM imeitoa nchi Mbali.

Uongozi mzuri ni pamoja na kuweza kuachia nafasi wengine waongoze.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Gentleman,
chairman Mbowe alikusudia kuachia ngazi mara baada ya uchaguzi huu wa Chadema kwisha.

Atagombea tena uenyekitia wa Chadema Taifa, kutokana na tamaa na uchu wa madaraka wa viongozi wagombea wa nafasi mballimbali za uongozi Chadema.

Lililo mshtua sana chairman Mbowe na hata kuamua kugombea tena, ni lile la kiongozi kutangaza nia ya kugombea umakamu mwenyekiti taifa asubuhi, halafu ghafla jioni kiongozi huyo huyo anatangaza kugombea uenyekiti wa chama hicho hicho Taifa.

Mbowe akajiuliza hivi kulikoni hasa, mtu asubuhi anaongea hili na jioni anaongea jengine?

hii tamaa na uchu ni vya nini hasa?

akaona hapana, ni lazima awajibike kukilinda chama ambacho amekijenga kwa gharama na kwa maumivu makali sana.

Na sasa Mbowe anatarajiwa ataiongoza Chadema Taifa hadi 2030🐒
 
Basi ungekuwa na akili ungeipigia kelele serikali yako na kuitaka isipeleke pesa za walipa kodi kwenye SACCOS badala ya kutaka kuibadilisha SACCOS ya watu walioamua kujifanyia mambo yao wakati wewe sio mwanachama/mjumbe wa hiyo SACCOS.

Maoni yako ni yapi?
Kwamba nisijadili Jambo ambalo kila mwezi wanapewa ruzuku ambayo ni Kodi yangu?

Kwamba Kodi zinazochukuliwa na kutolewa kama ruzuku zinataka kwa wajumbe na wanachama tuu?
 
Lissu anajua 100% hawezi kushinda, na wahafidhina na wachumia tumbo ndani ya CHADEMA hawawezi kuruhu ashinde.
Lakini kama ataruhusiwa kugombea, au atafanyiwa mizengwe akakatwa atakua ameingia katika vitabu vya kihistoria, na angalau lengo lake moja litakuwa limefanikiwa!
Kumbuka Lissu ni mwanaharakati, wanaharakati lengo lao ni kupaza sauti, sauti ikisikika lengo limetimia!
ndiyo bana afadhalli akae huko kwenye historia ili vizazi vijavyo wajifunze athari za makelele na mdomo bila mipango 🐒
 
Gentleman,
chairman Mbowe alikusudia kuachia ngazi mara baada ya uchaguzi huu wa Chadema kwisha.

Atagombea tena uenyekitia wa Chadema Taifa, kutokana na tamaa na uchu wa madaraka wa viongozi wagombea wa nafasi mballimbali za uongozi Chadema.

Lililo mshtua sana chairman Mbowe na hata kuamua kugombea tena, ni lile la kiongozi kutangaza nia ya kugombea umakamu mwenyekiti taifa asubuhi, halafu ghafla jioni kiongozi huyo huyo anatangaza kugombea uenyekiti wa chama hicho hicho Taifa.

Mbowe akajiuliza hivi kulikoni hasa, mtu asubuhi anaongea hili na jioni anaongea jengine?

hii tamaa na uchu ni vya nini hasa?

akaona hapana, ni lazima awajibike kukilinda chama ambacho amekijenga kwa gharama na kwa maumivu makali sana.

Na sasa Mbowe anatarajiwa ataiongoza Chadema Taifa hadi 2030🐒

😃😃

Kwamba mtu haruhusiwi kubadili nafasi ya uongozi anayotaka kugombea?
 
Lissu anajua 100% hawezi kushinda, na wahafidhina na wachumia tumbo ndani ya CHADEMA hawawezi kuruhu ashinde.
Lakini kama ataruhusiwa kugombea, au atafanyiwa mizengwe akakatwa atakua ameingia katika vitabu vya kihistoria, na angalau lengo lake moja litakuwa limefanikiwa!
Kumbuka Lissu ni mwanaharakati, wanaharakati lengo lao ni kupaza sauti, sauti ikisikika lengo limetimia!

Lisu akishindwa kwa haki sio tatizo kwetu

Tatizo kwetu ni falsafa za CHADEMA zimekaa kinafiki
 
Najuta kupoteza muda wangu kuipambania CHADEMA miaka yote hii. Niliyakanusha ma-ccm yaliposema cdm ni saccos ya mtu.
Mtazamo wangu wa sasa. Heri tubaki na ccm tu. Zimwi likujualo .. kuliko zimwi jipya ambalo tayari limeonekana litang'ang'ania madaraka miaka 1000. Narudi kujituliza na Simba na Yanga. CCM KAMATIA HAPOHAPO. NA UCHAGUZI MKUU MWAKANI KAMA MWAKA HUU. SAFI SANA.

Kumbe kuna wakati watu wakawaida huyaona mambo kiuhalisia kuliko Sisi tunaojifanya wasomi.
Angalia sasa tunaumbuka
 
Mkuu Robert Heriel Mtibeli mimi nakushauri tubaki kule kule kwenye kujadili mambo mengine tofauti na hizo siasa.

Kwa hali yetu hizi siasa, sawa ni haki na wajibu kuzijadili ila kwa ushamba wa wanasiasa wetu zinaleta uadui wa kijinga sana hadi kuhatarisha maisha wakati mwingine.

Mambo mengine haya ya kijamii ni rahisi tofauti zetu kuishia hapa hapa, kesho tukacheka.

Usalama wa kwanza ni kuhakikisha upo salama.

Ahsante Sana Mkuu kwa ushauri wako
 
Back
Top Bottom