Jile79
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 17,668
- 13,263
Ili uelewe na usichanganyikiwe lazima uwe tayari kuelewa kwanza na uwe na akili timamu na uwe na uwezo wa kuchanganya za kuambiwa na za kwako......Ntaka nikufundishe kwa kutumia mfano km utakuwa tayari kuelewa maana mnaongoza kwa ubishi wa kulazimisha mambo hata km jambo ni jepesi na rahisi kueleweka. Kabla ya maelezo mengine ni kuwa Yesu ni Mungu na Yesu ni Mwana wa Mungu. Kwanza uelewe kuwa neno Mungu limetokana na "umba" au "uumbaji" au "kuumba" yaani kutengeneza----Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake(huu ni ubishi mwingine wa waislamu maana allah hafanani wala hafananishwi). Wewe ni fundi vitanda, baadaye umemfundisha mtoto wako kutengeneza kitanda, baadaye mkashirikiana pamoja kutengeneza kitanda kizuri.Je, prs nani atakuwa ametengeneza hicho kitanda kizuri? Jibu ni wote. Kama watapewa jina moja bila kujali kuwa mmoja ni baba mwingine ni mwana wataitwaje? Jibu ni kuwa wote wataitwa Fundi lakini kuna fundi baba(Mungu baba) na Fundi Mwana (Mungu mwana).Kwenye Biblia Mungu baba anajulikana kama Yehova na Yesu haitwi Yehova na wala Yehova haitwi Emmanuel. Unajua Biblia ni tamu na raha mno lakini anaweza kuelewa yule tu niliyemwelezea hapo mwanzo. Kumbuka Bibilia haisomwi km vile unasoma kurani na vitabu vingine.Mkuu Jile79 Hapa ndipo wakristo mnapotuchanganya..
Yesu ni Mungu?
au
Mwana wa Mungu?
Ama Mtume?
Naomba majibu Mkuu..