Lakini mjue pia kwamba, bila kujali namna gani au wakati gani mtu anakufa, binadamu waliowengi watakufa ingawa najua si wote. Ila ukweli mmoja ni huu, binadamu wote watakaokuwa hai, na watakuwa walikufa, ipo siku tutasimama Mbele za Mungu, aliyetuumba na kutupa fursa ya kuishi duniani lakini tukiwa upande wake. Waliomkataa Mungu watahukumiwa adhabu na waliomkubali Mungu, watakirimiwa.
Kumkataa Mungu ni pamoja na kumpiga jirani yako kwa siri, uasherati, uzinzi, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, uwongo, kiburi, uuaji, uchawi, ushirikina, hila, wizi, chuki, usengenyaji, na yanayofanana na hayo.
Wafanyao mambo ya jinsi hii watahukumiwa. Lakini wakitubu dhambi hizi na kuacha kuzitenda, watasamehewe na Mungu hatazikumbuka tena.
Kama vile waliotaka kumuua Tundu Lisu wasipotubu watasimama hukumuni, vile vile na wanaofanya dhambi kutokana na tukio hilo, watasimama katika hukumu ya Mungu.
Ninyi nyote, MNAOMLAANI NA KUMPIGA MAWE RAIS MAGUFULI KWA KUAMINI KWAMBA NI YEYE ALIHUSIKA katika tukio la kupigwa kwa Tundu Lisu, MNAHAKIKA KWAMBA YEYE NDIYE ALIWATUMA WAUAJI, AU ALIRATIBU MPANGO WA MAUAJI YA TUNDU LISU, AU ALIFURAHIA MOYONI MWAKE TUKIO HILO? MNA HAKIKA KWAMBA ALISHIRIKISWA MPANGO HUO KABLA HAUJATEKELEZWA?
Angalieni ndugu zangu, ushabiki wa mambo msiyoyajua, usije ukawasababisha kufanya dhambi kwa Mungu kisha kuwaingiza hukumuni.