Tundu anatukwamisha na kutukwaza. Watu tunataka kujua sababu ya tukio lile lakini yeye binafsi halichukulii serious kabisa. Sijui kwanini haoni kama uhai wake ulikua mashakani na sijui kwanini haoni kupatikana kwa ukweli utasaidia raia wengine kama yeye kuwa salama kwa kile watakachokijua na kukielewa
Nguvu ambazo amekua akizunguka nazo kuongea angezitumia kuweka mambo bayana ingemsaidia yeye familia yake na watanzania kwa ujumla
Kuendelea kuongea maongezi anayojua wazi hayaleti suluhu ni kutufanya tuanze kuwaza mambo mengine.
Sipendi kuongelea kabisa hili swala la Tundu sababu liliniumiza sanaaa.... lakini kitendo cha yeye kuja kwa kampeni na kuondoka kwa haraka baada ya kushindwa uchaguzi huku akiacha mambo yake yakiwa yananing'inia kwenye vyombo vya usalama inafikirisha sana
Tuache ushabiki tuwaze sawasawa