Watu wameendekeza tamaa kwa kisingizio cha usasa

Watu wameendekeza tamaa kwa kisingizio cha usasa

Unakuta mtu kazaliwa na wazazi wastaarabu na wenye dini lakini baada ya kuyajua ya ke na me(mapenzi) mtu huyo anawakana hadi wazazi kwa tabia mbovu na za kishenzi kwa kisingizio cha usasa

Wengi wetu tumezaliwa na familia duni na za kawaida kiasi ila baada ya kuyajua ya duniani mtu anaacha ya kwao kwa kigezo cha usasa na kuanza kuvaa vichupi na kukaa uchi tafauti na alivyo lelewa.

Hata waliozaliwa katika utajiri bado familia zao hazikuwa nyuma kuwalea katika maadili lakini badala yake wakawapuuza wazazi kwa kisingizio cha usasa

Wazazi wengi wanashindwa kuwalea watoto katika maadili kwa kisingizio cha usasa badala yake watoto wanakuwa wapumbavu, watembea uchi na wagawaji kiholela na wavuta bangi ilhali wazazi hao wapo stable kimaadili na kiuchumi pia

Matokeo yake jamii imekuwa haiangaliki, haishauriki na haitamaniki kwa uovu na ukahaba uliopitiliza unaochagizwa na uvaaji wa nguo fupi na tabia mbovu mbovu za vijana na watu wazima kwa kisingizio cha usasa baada ya kushindwa kwa uwajibikaji wa wazazi kwenye famila zao hatimae kuiharibu jamii kwa ujumla.
Ni ushamba tu
 
Masikini huwa wana brag sana. Ndio maana ni ngumu masikini kuwa Gentleman au a lady. Ni ngumu sana.
Ni sawa tu mkuu utaniita masikini, wengine washanambia mshamba mwingine akasema muoga yote sawa

Maada yangu inajieleza kuwa mm ni mtu wa namna gani(mimi sio wa kizazi kipya)
 
Huyu jamaa ni mjinga hakuna analojua. Na mara nyingi mwanaume aliyekamilika hawezi ongelea mambo ya ushoga kila mara kwasababu ni mambo ya hovyo hata kutamka. Mtu kama mleta mada ni wale wanaojihusisha na ushoga ila hadharani wanapinga ili kujitengenezea kinga pale mambo yao yanapovuja.
Kuna uzi nilileta humu kuelezea jinsi gani kulegalega kwa mfumo dume kumeongeza mmomonyoko wa maadili

Nikiwa na maana kuwa wanaume wamekwepa majukumu yao katika familia na kuendekeza tamaa

Yaani siku izi mwanaume anaufurahia mmomonyoko wa maadili uliopo kwakua anapata wasichana kwa urahisi

Wanawake wamedunishwa na kushuka thamani(wananunuliwa kama bidhaa) kwa kigezo cha 50/50 na wenyewe wanaona sawa

Wanaume wamekimbia majukumu ya kuoa na kumtunza mke na mtoto kwakuwa nyuchi(mbususu kwa lugha ya jf) zinapatikana kiurahisi, nahii ni kwakuwa hamna mila wala tamaduni inayomlinda huyu mwanamke na wanawake wenyew wanaona sawa tu

Kiufupi wanaume ndio chanzo cha matatizo yote hayo kwa ajili ya tamaa za macho na kimwili kumuona mwanamke dhariri akitembea uchi ndio wao waona raha.

Tukiyasemea haya twaitwa washamba maana kila zama na kitabu chake
 
Kuna uzi nilileta humu kuelezea jinsi gani kulegalega kwa mfumo dume kumeongeza mmomonyoko wa maadili

Nikiwa na maana kuwa wanaume wamekwepa majukumu yao katika familia na kuendekeza tamaa

Yaani siku izi mwanaume anaufurahia mmomonyoko wa maadili uliopo kwakua anapata wasichana kwa urahisi

Wanawake wamedunishwa na kushuka thamani(wananunuliwa kama bidhaa) kwa kigezo cha 50/50 na wenyewe wanaona sawa

Wanaume wamekimbia majukumu ya kuoa na kumtunza mke na mtoto kwakuwa nyuchi(mbususu kwa lugha ya jf) zinapatikana kiurahisi, nahii ni kwakuwa hamna mila wala tamaduni inayomlinda huyu mwanamke na wanawake wenyew wanaona sawa tu

Kiufupi wanaume ndio chanzo cha matatizo yote hayo kwa ajili ya tamaa za macho na kimwili kumuona mwanamke dhariri akitembea uchi ndio wao waona raha.

Tukiyasemea haya twaitwa washamba maana kila zama na kitabu chake
Jiunge na wanawake upiganie haki zao.
 
Usiwasukumie vijana lawama zisizo wahusu, hizo lawama zipeleke moja kwa moja kwa hawa wazee kwa kuharibu hiki kizazi.

Unampa mtoto malezi ya kighaibuni alafu huyo mtoto aje kuishi maisha ya kiafrica. Utamlaumu bure huyu mtoto

Mzazi umeweka Demokrasia kwenye malezi, mtoto anayohaki ya kuchagua anachokitaka, huyu akikua akafanya maamuzi yake bila kumsikiliza mtu utamlaumu?

Kama unampa mtoto malezi ya kimagharibi basi hakikisha anakwenda kuishi huko, Hapa Africa ataonekana hana adabu na anaendekeza ukisasa ambao kiuhalisia kapewa na wazazi wake.
Waafrica tunashangaza sana, ni juzi tu hapa hata vizazi vinne nahisi vingi tulikuwa tunazurua juu wazi na chini ni juu ya magoti na amani ilitawala leo mtu akivaa nguo fupi tu inaonekana sio utamaduni na amekengeuka

Juzi tu hapo mlikuwa mnazunguka mbuyu, leo mtoto akihama kwenye dini moja kwenda nyingine ambazo zote zimeletwa mnasusa na hata kutishia kuwapa laana

All in all, tuwalee watoto katika maadili ila haimaanishi watakapofanya maamuzi yao kama watu wazima basi mzazi ujilaumu kuwa hukumpa malezi, binadamu ana akili timamu na kuna muda huitumia pasi kuingiliwa na mtu

Ukitaka umchunge mtu pale anapooona kajipata utajilaumu bure upate presha
 
Hapo utawatenga watoto wasiojua asili za wazazi wao kwa sababu mbalimbali, kwahiyo hao mtawatambua kwa namna ipi??

mkuu usilazimishe jambo lisilo na manufaa, mpaka sasa hujanambia hizo tamaduni zako zimesaidiaje kutatua changamoto nchini.

Nani kakwambia ukizaliwa marekani unakua huna kabila ni nani??
Kwahiyo mtoto wa AY sio mnyakyusa kisa kazaliwa marekani?? Namna gani kijana
Mkuu unatengeneza maada yako mpya

Sasa kumbe mtoto wa AY ni mnyakyusa ni jukumu la AY na jamii ya AY kumfunza tamaduni za kinyakyusa hapo shida iko wapi

Na kuhusu kutatua changamoto za kouchumi cjui na kisiasa hizo utaelezwa kwenye jukwaa la siasa na uchumi mm nimeangazia malezi na maadili na nikakuuliza swali ili jamii tuone kuwa tumepiga hatua kiutamaduni tunaangalia kitu gani?

Na kuhusu mila ya kiafrika ni mila gani nikakujibu kuwa Afrika ina makabila na kila kabila lina mila zake, hakuna mila za nchi kwakuwa nchi inaendeshwa kibepari serikali haina mila wala dini
 
Mkuu ukweli ni kwamba nyie watu mnaojifanya kuongelea ushoga ndo nyuma ya pazia mnafanya ushoga na mambo mengine machafu. Mtu mwenye maadili hana sababu ya kuuaminisha umma kwamba ana maadili mazuri bali matendo yake yataongea zaidi. Wewe ni shoga ambaye una hofu ya mambo yako kujulikana hivyo unatengeneza kinga mapema uje utetewe. Mwanaume uliyekamilika unazihofia nini sketi fupi?
Sawa kwakua hiyo ndio hoja yako, nilijua nikiongelea haya ntatukanwa kila aina ya tusi na nitaambiwa mshamba

Ila kuna mkuu hapo juu amesema uovu usipo kemewa utachukuliwa kama ndio utamaduni wa eneo husika kwaiyo tuna jukumu la kuukemea upotovu wa maadili uliojificha kwenye kichaka cha muda/zama za kizazi kipya
 
Mimi nilitegemea useme tuchukue yaliyo mazuri na mabaya tuwaachie wao.
Na uzuri au ubaya wa jambo hupimwa na mtu/jamii husika lakini pia ni kulingana na sheria za nchi husika.

Mfano, kuvaa vimini sio kosa kisheria lakini inaweza kua tabia mbaya kwako, basi pambania hilo kwenye familia yako lakini kaa ukijua sheria za nchi hailitambui.

Kuimba/kusikiliza nyimbo hasa hizi bongo fleva nk, inaweza kua mbaya kwako lakini sheria za nchi hazitambui hilo, kwako baya ila kwa wengine inawalipa vizuri. Pambana na jamii yako.

Kwahiyo kwenye hizo unazoita "mila za wazungu" kuna mbaya na nzuri, nzuri zibebwe na mbaya zitupwe na hayo ndio maendeleo kiutamaduni.

Mila na desturi sio static, huwa zinabadirika mkuu, 1800's hawakua wanavaa t shirt na jeans, suits, raba nk lakini kutokana na muingiliano wa watu leo hii wewe unaona jeans ni vazi zuri na linafaa, gauni au skirt ndefu kwa ke ni vazi zuri na linafaa.
Umeongelea vizuri mkuu ila hebu tuchukue mfano wa wahadzabe na wamaasai walioganda kwenye tamaduni na mila zao wamebadilika kiasi gani?

Halafu pia sheria za nchi hazifuati mila ya kabila lolote ila linafata world order ambayo kwangu mm ndio usasa wenyewe maana hatukuwa na utaratibu wa democracy

Kwaiyo ni jukumu la familia na koo kujisimamia na kusimamia mila zao kama yafanyavyo hayo makabila niliyotaja

Swali ni je? Kusimamia mila na tamaduni kama wafanyavyo wamaasai ni ushamba! Je hatuwezi kusema wameendelea kiutamaduni?
 
Umeongelea vizuri mkuu ila hebu tuchukue mfano wa wahadzabe na wamaasai walioganda kwenye tamaduni na mila zao wamebadilika kiasi gani?

Halafu pia sheria za nchi hazifuati mila ya kabila lolote ila linafata world order ambayo kwangu mm ndio usasa wenyewe maana hatukuwa na utaratibu wa democracy

Kwaiyo ni jukumu la familia na koo kujisimamia na kusimamia mila zao kama yafanyavyo hayo makabila niliyotaja

Swali ni je? Kusimamia mila na tamaduni kama wafanyavyo wamaasai ni ushamba! Je hatuwezi kusema wameendelea kiutamaduni?
Unaweza kufananisha wamasai na wachaga??
Wamasai na wanyakyusa??
Wamasai na wahaya?

Vipi wahaya hawafati mila zao, wachaga hawafati mila zao, maendeleo yao yakoje??

Kila mwisho wa mwaka kaskazini kuna matambiko, lakini ona maendelo yao!!.

Ujue labda tunatofautiana kitu kidogo sana.
Hizo mila zina msaada gani katika kutatua matatizo yako??
Wamasai tupo nao town wanauza sendo na dawa za nguvu za kiume, hizo mila walizoshikiria zinafanya washindwe hata hiyo biashara maana wengi wao hawajui kiswahili wala kingereza zaidi ya lugha yao ya kimasai!!

Sasa hivi wengi wao wamebadilika ila zamani kidogo ilikua huwezi kaa karibu nao, kuna harufu walikua nayo sijui ilikua inatokana na nini, zote hizo ni mila zao.

Wahadzabe mila zao zimewasaidia nini zaidi ya kukosa mahitaji muhimu.

Nachohitaji mm ni umuhimu wa hizo mila.
 
Mkuu unatengeneza maada yako mpya

Sasa kumbe mtoto wa AY ni mnyakyusa ni jukumu la AY na jamii ya AY kumfunza tamaduni za kinyakyusa hapo shida iko wapi

Na kuhusu kutatua changamoto za kouchumi cjui na kisiasa hizo utaelezwa kwenye jukwaa la siasa na uchumi mm nimeangazia malezi na maadili na nikakuuliza swali ili jamii tuone kuwa tumepiga hatua kiutamaduni tunaangalia kitu gani?

Na kuhusu mila ya kiafrika ni mila gani nikakujibu kuwa Afrika ina makabila na kila kabila lina mila zake, hakuna mila za nchi kwakuwa nchi inaendeshwa kibepari serikali haina mila wala dini
Unajua kwanini Nyerere na wenzie walipigania kiswali kitumike nchini?

Unadhani kwanini mtoto akifaulu form 4 pale wa kusini atapelekwa kaskazini na kaskazini atapelekwa kusini, nakumbuka advance shule moja huko kusini 80% ni watu toka Arusha na Moshi.
Ili kukuza umoja na mshikamano.

Una mila zako nina mila zangu, heshimu mila zangu na ili kusiwe na upendeleo basi tuwasiliane kwa kiswahili.
Anavaa kimini ni yeye, hao wamasai wanavaa lubega kifua chote wazi, mipaja yote nje, we waheshimu tu na mila zao.
Je wewe unaweza kutembea kifua wazi na mapaja nje??
 
Ukute neno "maadili" lenyewe hujui maana yake ndio maana waongea mambo za mini skirt
hakuna njia yoyote ya kupambana na mabadiliko zaidi ya kufa mkuu.

Huwezi kuzuia hilo kwa namna iwayo yote.
 
Unajua kwanini Nyerere na wenzie walipigania kiswali kitumike nchini?

Unadhani kwanini mtoto akifaulu form 4 pale wa kusini atapelekwa kaskazini na kaskazini atapelekwa kusini, nakumbuka advance shule moja huko kusini 80% ni watu toka Arusha na Moshi.
Ili kukuza umoja na mshikamano.

Una mila zako nina mila zangu, heshimu mila zangu na ili kusiwe na upendeleo basi tuwasiliane kwa kiswahili.
Anavaa kimini ni yeye, hao wamasai wanavaa lubega kifua chote wazi, mipaja yote nje, we waheshimu tu na mila zao.
Je wewe unaweza kutembea kifua wazi na mapaja nje??
Jibu kwanza hili swali, ili jamii tuone kuwa tumepiga hatua kiutamaduni tunaangalia kitu gani?
 
Jibu kwanza hili swali, ili jamii tuone kuwa tumepiga hatua kiutamaduni tunaangalia kitu gani?
Kupiga hatua kitamaduni ni kupreserve asili yenu.
Kama mmebadilika basi hapo hakuna maendeleo ya kitamaduni.
 
Usiwasukumie vijana lawama zisizo wahusu, hizo lawama zipeleke moja kwa moja kwa hawa wazee kwa kuharibu hiki kizazi.

Unampa mtoto malezi ya kighaibuni alafu huyo mtoto aje kuishi maisha ya kiafrica. Utamlaumu bure huyu mtoto

Mzazi umeweka Demokrasia kwenye malezi, mtoto anayohaki ya kuchagua anachokitaka, huyu akikua akafanya maamuzi yake bila kumsikiliza mtu utamlaumu?

Kama unampa mtoto malezi ya kimagharibi basi hakikisha anakwenda kuishi huko, Hapa Africa ataonekana hana adabu na anaendekeza ukisasa ambao kiuhalisia kapewa na wazazi wake.
Sasa tatizo nn? Au liko wapi mtu kuwa huru juu yake binafsi?
 
Kupiga hatua kitamaduni ni kupreserve asili yenu.
Kama mmebadilika basi hapo hakuna maendeleo ya kitamaduni.
Baki hapo hapo mkuu, kuendekeza usasa ni kujirudisha nyuma kiutamaduni na sio maendeleo

Wapewe heko wamang'ati, maasai, wahadzabe kwa kuonesha jitihada za maendeleo ya kiutamaduni

Pia walaaniwe wasanii wa kizazi kipya, bongo movies na wahuni wote kwa kutuletea mila na tamaduni za kigeni zinazopoteza asili yetu
 
Sasa tatizo nn? Au liko wapi mtu kuwa huru juu yake binafsi?
Tujifunze kulea mkuu, watoto sio wa kuwapa uhuru wa kujiamulia ilimradi tunaishi tuwalee katika maadili hadi siku tunakufa au wao kufa kabla yetu
 
Back
Top Bottom