Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Uwezo wako bado mdogo ila hatua kwa hatua utaelewa kuwa MUNGU yupo hapo hapataki haraka na mkurupuko na majibu ya jumla kama unayotoa,kaa na ufikiri utaona kitu kama hutaki kufikiri basi baki akili yako ndogo inayogoma kufikiri.Sio tu hayupo.
Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Uwezo wako bado mdogo ila hatua kwa hatua utaelewa kuwa MUNGU yupo hapo hapataki haraka na mkurupuko na majibu ya jumla kama uliyotoaSio tu hayupo.
Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Mm naamini wewe una akili nyingi sasa ktk hizo akili nyingi ulizonazo umewah kufanya jambo gani kwa vitendo na likawashangaza watu wengi na linaloshikika.Nimekwambia tangu mwanzo kwamba, Akili kila mtu anazo.
Hakuna uhusiano wowote wa kuwa na akili na kutoamini Mungu, Au kutokuwa na akili na kumwamini Mungu.
Imani ni maamuzi ya mtu. Na hukatazwi kuwa na imani.
Ila ukisema imani yako ina ukweli lazima uthibitishe hilo.
Hivyo hata kusema una imani ya Mungu ni uhuru wako kusema hivyo.
Ila ukidai kwamba imani yako ya Mungu ndio yenye ukweli lazima uthibitishe hilo.
Na ueleze Mungu huyo ni nini?
Na unathibitisha vipi Mungu huyo yupo?
Na si imani na mawazo yako ya kufikirika tu.
Uwezo wako bado mdogo ila hatua kwa hatua utaelewa kuwa MUNGU yupo hapo hapataki haraka na mkurupuko na majibu ya jumla kama uliyotoaSio tu hayupo.
Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Kwa uelewa wangu si kila jambo lisilo ingia akilini lina maana ya kwamba ni uongo au la kipuuzi, jambo laweza kuwa haliingii akilini kwa sababu ya kushindwa kwetu kuelewa tu au kwamba hilo jambo ni la ajabu kiasi cha kushindwa kukuingia akilini ila ni la kweli kabisa na hivyo ndio lilivyo.
Binadamu anaongozwa na ubongo, hivyo uwezo wako ndo umefikia hapo na upo sahihi kutokana na mawazo yako maana ubongo hauwezi kufikiri zaidi ya hapo.Inategeme Mungu wako ni yupi, maana watu qwana kila aina ya Miungu. Kuna wenye miungu watu, miungu ng'o,be, miungu vitu.
Sisi Waislam tunaamini hakuna mungu apasae kuabidiwa isipokuwa Allah.
Hazai wala hajazaliwa na hakuna anachofanana nacho.
Kwahiyo tunajadili imani kiupana wake au imani za dini?Nimesema kwenye imani KILA KITU KINAWEZEKANA........Inakuingia akilini?
Kipi hicho chenye kumfanya binaadamu atafute faraja na ina maana wasioamini Mungu hawana faraja au kukana Mungu nao ni faraja kwao?Mungu ametengenezwa na Mawazo ya Binadamu ili kupata faraja tu , bila Binadamu hakuna Mungu
Kwa muktadha wa uzi huuKwahiyo tunajadili imani kiupana wake au imani za dini?
Sasa utasemaje kwenye imani ya Mungu lolote linawezekana?Kwa muktadha wa uzi huu
Tunajadili imani ya Mungu ambayo huzaa dini
Tatizo umekula na umeshiba ndio maana unaongea utopolo ,ila ungekuwa na njaa hata hii jeuri usingekuwa nayo,na kiburi chako adabu yake ni siku ya kufa tu ndio utajua kuwa mungu yupo au hayupoKubadilika huku kwa watu bado haku thibitishi na kuonesha Mungu huyo yupo.
Swali ni je, Mungu huyo Alishindwaje kuumba binadamu watakao mtambua yeye yupo kwa wakati wote?
Kama lengo la huyo Mungu ni kutambuliwa yupo, Alishindwaje kuumba Binadamu watakao mtambua yeye yupo siku zote?
Kwa nini binadamu wengine hatumtambui Mungu huyo kama yupo?
Je Mungu huyo hakujua kwamba sisi Atheists tutakuja kumtambua yeye hayupo atudhibiti mapema na kutufanya tumtambue yupo?
Mungu huyo akisha tambuliwa yupo inamsaidia nini?
Kwani Mungu huyo hajitambui yupo mpaka sisi binadamu tumtambue yupo ndio ajue kwamba yupo?
Huyo Mungu anashindwa kuwapa chakula watoto wadogo wanaokufa kwa njaa maeneo mbalimbali duniani halafu aje anipe shibe mimi?Tatizo umekula na umeshiba ndio maana unaongea utopolo ,ila ungekuwa na njaa
hata hii jeuri usingekuwa nayo,
Ulishawahi kufa ukajua huyo Mungu yupo?na kiburi chako adabu yake ni siku ya kufa tu ndio utajua kuwa mungu yupo au hayupo
Soon atafika apo kwako na atakudhihirishia kwamba yeye yupo tena kwa vitendo ili ujue kuwa mungu hadhihakiwi, utaleta mrejesho.Huyo Mungu anashindwa kuwapa chakula watoto wadogo wanaokufa kwa njaa maeneo mbalimbali duniani halafu aje anipe shibe mimi?
Huyo Mungu uwezo wa kunishibisha Hana.
Huyo Mungu hajawahi kushibisha mtu yeyote kwa vile Hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.View attachment 2930960
Ulishawahi kufa ukajua huyo Mungu yupo?
Au unaleta vitisho na hofu ulivyo pumbazwa na dini yako?
Nakwambia hivi, huyo Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Kama Mungu huyo yupo mwambie aje hapa ajidhihirishe.
Mpaka sasa Mungu huyo Kashindwa kufanya chochote, Kashindwa kuja hapa kujidhihirisha.Soon atafika apo kwako na atakudhihirishia kwamba yeye yupo tena kwa vitendo ili ujue kuwa mungu hadhihakiwi, utaleta mrejesho.
Hiki kilikuwa kituko Cha mwaka.Nilikimbia seminary baada ya kunipatia bible verses, nitafakari na nisikilize sauti ya mungu na niwaambie Mungu kaniambia nini!