Watu wazima 25+: Ukiachana na kufiwa, ni TUKIO gani kubwa liliwahi kukutoa machozi hadharani 😭

Watu wazima 25+: Ukiachana na kufiwa, ni TUKIO gani kubwa liliwahi kukutoa machozi hadharani 😭

Tukio lingine lililonifanya nilie hadharani my Dada alipograduate chuo ..alivyorudi home kwenye kumpokea nilijikuta nalia tu Mimi...loh[emoji1787][emoji1787] ingawa sikua Nimefika 25
Mate unampenda sana dada yako eeh?
 
Kuna mambo nlipanga maishani hayakutimia kwa wakati, nililia usku kuchaaa.

Wakat mwngne kulia huwa kunanipa ahueni, lkn swez lia mbele za watu huwa nalia peke yangu chumbani mpk nakaa sawa
 
Aisee nilibaki home mwenyewe nikasema ngoja nipike, nimekata kitunguu aisee machozi yalinitoka nikaacha hiyo biashara.
 
Mwaka 2014 nilipata breakdown ya gari mlima kitonga, ilikuwa ni mida ya jioni na kwa kuwa pale pana vibaka , nikashauriwa nitafute mwenyeji kwa ajili ya ulinzi . Nilimoata jamaa , kuitwa 'Tizo' akanisaidia usiku kucha na kutwa nzima kwa ulinzi na supports kadhaa , katika story alinisimulia mengi sana , jamaa alikuwa yatima na maisha magumu kupita kiasi na nikagundua 'Tizo ' ni kifupisho cha matatizo, na ndo lilikuwa jina lake halisi.
Baada ya breakdown kuisha niliachana naye na kumpatia stahiki yake , nikamatia nguo kadhaa na viatu kadhaa nikaondoka zangu , nilifanya hivi kwa miaka kadhaa mbele kila nilipokuwa nafasi na kupita eneo hilo maana hakuwa mbali na barabara ,baadaye tukapotezana ,
Nimekuja kumuona mwaka 2020 , baada ya kuanza kupita tena njia hiyo , kumuangalia vizuri hana mkono wa kulia , yani umekatika kwenye bega kabisa , namuuliza Tizo mkono umefanyaje tena akaniambia alianguka kwenye lori wakati anauza mahindi ya kuchoma ,akateleza na kukanyagwa na tairi , mkono, ulikuwa wa kupona ila hakukuwa na pesa ya matibabu hadi ulipoanza kuoza ndo ukakatwa.
Nilishindwa kujizuia kutoa chozi!
Mkuu, pole ukiwa unapita hapo jitahidi kumpelekea hata zawadi ndogo kama nguo na hata chakula au hela ya kujikimu
[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Mi siku moja nilikua bar sasa wakati naenda toilet nikakutana na jamaa analia kinoma na mimi nikamuungia nikaanza kulia na kumpa ushauri mara nimwambie yataisha tu mara kaza ndio uanaume huo.Nalifikiriaga hilo tukio sijui hata kwa nini nilianza kulia na mimi.Mimi ni matukio mawili tu yameniliza hili na msiba wa mzazi wangu.Kwa sasa na kuendelea sina mpango wa kulia.
 
Back
Top Bottom