Watumiaji wa simu - mambo yanayokera

mtu kujibu text kwa vifupi , unakuta umetuma text ndefu mtu anajibu p,k, pp, kuandika texts za msingi kwa vifupi ani dah me mtu akiniandikia p,k,pp simjibu hadi akili imkae sawa
Hawa wenye haka kamtindo ni washamba sana eti mtu anaandika xaxa badala ya sasa........ Akinijibu mtu hivo namfutilia mbali
 
MDAU😱y niaje

WEWE:shwari vipi hali

MDAU:safi habari za huko?

WEWE:nzuri tunamshukuru Mungu

MDAU:vipi shemeji na watoto

WEWE:hawajambo kabisa.

MDAU:mambo yanakwendaje huko?

WEWE:tupo tunakomaa

MDAU:mmetunyima nini huko?

WEWE:hamna ndg jus tu

MDAU:wanasemaje huko?


Huwa nachoka kabisa maana ni kama sms kumi zote za aina moja tu.
 
Du..[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
a) Umenipigia simu sijapokea, Baada ya muda kukuta call zako, nakupigia "Unaanza lawama" hawa naona nachoka kuwavumilia sasa.

b) Mtu kaanzisha mada mwenyewe kwa sms! Unamjibu kwa kutulia kabisa tena kwa ufafanuzi zaidi (kumbuka ni text) umeacha kufanya ulokuwa nalo. Kaipata kaisoma, Anauliza swali. Unacopy sehemu ya ile text uliomtumia, maana ndio jibu la swali lake lilipo! Anakuuliza tena, unacopy sehemu nyingine tena unamtumia! Baadae anakujibu 'Aaah' sawa.

c) Unachart na Mtu anatuma vitext vifupi, kukamilisha habari yake unajipata Haikuwa na haja ya text ziwe sita, kwa jambo lilelile moja, angelitumia tu sms moja, wala isingalikuwa refu ya kumaliza kurasa moja ya sms. Dah hivi Watu wa hivi huwa Mnaandika sms Miguu ikiwa wapi? Naona inapoteza muda aise!

Tuishi tu Tutaelewana.
 
Aisee tabia ya kukata simu inanikera kweli yaani ameona unaongea pumba
 
Haha umetisha boss
Namba 9 hapo. Nikupigie simu usipokee, nikutext usijibu halafu ndio ukae kimya, Hiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!! Hata ukikutana na mimi barabarani usithubutu kuongea na mimi
 
Hahaha that means she doesn't know her place yaani hajaelewa bado kwamba yeye ni mpango wa kando kwa hiyo anajikuta anakumiliki mzima mzima
Michepuko: unaweza kukupigia na kukuta upo kwenye kwenye mazingira hatarishi (upo na waziri mkuu kwa mfano) na inabidi uikate ile simu. Badala ya mtu kujiongeza, unashangaa anapiga tena na tena na tenaaa😀
 
Nitakunyoosha
Mimi namba 9 nipo.... Naweza nikatoka nyumbani wanataka kuniuliza kitu au kuniagiza akianza kupiga inaita alipo.


Nimeshindwa kuacha hii.
 
Haha pole boss
 
Ukiona hivyo hujatuma ya kutolea teh
 
Haha ukiona hivyo anakupanga kuna shida anataka kukwambia
 
Haha mtu anauliza swali anatuma neno kiulizo anaweka kwenye text nyingine...na huu mtindo umeanza baada ya simu janja na hivi vifurushi vya unlimited sms mbona enzi zile sms moja unatuma kwa sh 59 watu walikuwa hawafanyi huu ujinga
 
Me katika yote ayo sina matatizo nayo lakini me ni lile swala la late replies na blue tick za whatsapp... fanya mambo yote lakin sio izo vitu mbili
Kama upo hivyo kwenye kuangalia blue tick na mie huwa nakereka mtu akikomaa nimekutumia msg nimeona blue tick ukauchuna (na mie huwa naamini mtu anaehitaji kitu cha muhimu lazima atapiga ama atatuma sms ya kawada ambayo uwe na kifurushi huna kifurushi itaingia (lazima nitamchimba mkwara wakati message inaingia nilikuwa na bundle yaani 4MB yaani muda ule ule nataka kujibu ikakata (maana kuna watu message za muhimu wanatuma kuitia whatsapp ambayo ni subject to bundle kwa mpokeaji hao mie ndo hinikera)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…