Watumishi kujazana kwenye ATM tarehe za mishahara ni kielelezo tosha cha umaskini na ukiukwaji wa haki za watumishi

Watumishi kujazana kwenye ATM tarehe za mishahara ni kielelezo tosha cha umaskini na ukiukwaji wa haki za watumishi

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
4,580
Reaction score
7,943
Kwema wakuu?
Miaka iliyopita mshahara ukitoka tu Maza alikuwa ananiambia nikamtolee fedha yote nitakayoikuta kwenye akaunti yake pindi tu mshahara unapoingia.

Nikifika tu NMB nakutana na foleni kubwa sana. Nikienda tarehe za kawaida kwa issue zingine pale Benki nikichungulia ATM sioni foleni kubwa.

Hii nimeishuhudia pia nilipoingia kwenye Utumishi wa Umma. Watumishi wa Umma na Wafanyakazi wa kampuni binafsi Tanzania hali zao ni ngumu, Waajiri wanakiuka haki za waajiriwa wao.

Waajiri (mabosi) wanawatesa watumishi wao kwa kuwapatia maslahi kiduchu huku wao wakipata viyoyozi nyumbani, kazini na barabarani. Watumishi wengine wana madeni mengi, furaha yao ni siku 5-10 tu ndani ya mwezi.

Mwingine anaweza kusema kama maslahi madogo acha kazi, na mwingine anaweza kusema shukuru maana wengine hata hicho kidogo hatuna, hizi ni hoja dhaifu na hazipaswi kutolewa na mtu mwenye akili timamu.

Viongozi Waandamizi muzipitie Sera za Utumushi.
 
.
IMG_20191022_072648.jpeg
 
Kuajiliwa serikalini ni kujiunga kwenye umasikini milele, njooni huku kwenye makampuni na international NGO tunakula maisha tu,,,unalipwa basic salary kuanzia 2million mpaka 8million unapewa accommodation laki nne kila mwezi na communication laki ,,,Sasa huko sijui mnafurahia maisha gani

MTU unafanya kazi serikalini miaka mitano hata IST au passo imekushinda kinunuwa sasa si utakufa na madeni na kula mihogo,,,mie nawashangaa sana wanaotaka kufanya kazi serikalini..

Ukitaka kufurahia maisha serikalini uwe mwanasiasa tyuu ila wengine ni shida tupu tena kama unafanya kazi kwenye halmashauri wewe juwa ushajiunga kwenye umasikini
 
Kwema wakuu?
Miaka iliyopita mshahara ukitoka tu Maza alikuwa ananiambia nikamtolee fedha yote nitakayoikuta kwenye akaunti yake pindi tu mshahara unapoingia.

Nikifika tu NMB nakutana na foleni kubwa sana. Nikienda tarehe za kawaida kwa issue zingine pale Benki nikichungulia ATM sioni foleni kubwa.

Hii nimeishuhudia pia nilipoingia kwenye Utumishi wa Umma. Watumishi wa Umma na Wafanyakazi wa kampuni binafsi Tanzania hali zao ni ngumu, Waajiri wanakiuka haki za waajiriwa wao.

Waajiri (mabosi) wanawatesa watumishi wao kwa kuwapatia maslahi kiduchu huku wao wakipata viyoyozi nyumbani, kazini na barabarani. Watumishi wengine wana madeni mengi, furaha yao ni siku 5-10 tu ndani ya mwezi.

Mwingine anaweza kusema kama maslahi madogo acha kazi, na mwingine anaweza kusema shukuru maana wengine hata hicho kidogo hatuna, hizi ni hoja dhaifu na hazipaswi kutolewa na mtu mwenye akili timamu.

Viongozi Waandamizi muzipitie Sera za Utumushi.
Waache tuu waisomage namba si hawajaziona kazi nyingine za kufanya
 
Kuajiliwa serikalini ni kujiunga kwenye umasikini milele, njooni huku kwenye makampuni na international NGO tunakula maisha tu,,,unalipwa basic salary kuanzia 2million mpaka 8million unapewa accommodation laki nne kila mwezi na communication laki ,,,Sasa huko sijui mnafurahia maisha gani

MTU unafanya kazi serikalini miaka mitano hata IST au passo imekushinda kinunuwa sasa si utakufa na madeni na kula mihogo,,,mie nawashangaa sana wanaotaka kufanya kazi serikalini..

Ukitaka kufurahia maisha serikalini uwe mwanasiasa tyuu ila wengine ni shida tupu tena kama unafanya kazi kwenye halmashauri wewe juwa ushajiunga kwenye umasikini
Unachosema.ni sahihi lakini mkuu hizo international.NGO ziko ngapi na zinaajiri wangapi?? tusema basi zinaajiri wengi sana laki moja, sawa hao wengine tuende wapi??
 
Unachosema.ni sahihi lakini mkuu hizo international.NGO ziko ngapi na zinaajiri wangapi?? tusema basi zinaajiri wengi sana laki moja, sawa hao wengine tuende wapi??
Muwe wanasiasa mkuu kazi mbona zipo nyingi za kufanya,,,, sasa mkuu hivi kwa nchi hii unaweza kutamani kuwa mwalimu? Au kufanya kazi kwenye hizi halmashauri? Si bora ufuge kuku tyuu zitakulipa
 
Muwe wanasiasa mkuu kazi mbona zipo nyingi za kufanya,,,, sasa mkuu hivi kwa nchi hii unaweza kutamani kuwa mwalimu? Au kufanya kazi kwenye hizi halmashauri? Si bora ufuge kuku tyuu zitakulipa
Wanasiasa huoni tunavyopigwa Virungu?? Mkuu tutatolewa kucha mpaka lini?
 
Hii nchi ina shida moja, ingawa tumeambiwa hapa kazi tu lakini mitazamo ya watanzania wengi kuwa kazi lazima wakafanye huko kwenye makampuni sijui mashirika 'useless'.

Dharau kubwa hapa ni kuajiriliwa kwenye halmashauri na hasa mtu kuwa mwalimu. Huu ni upuuzi mkubwa sana.

Naomba kutanguliza kwanza mimi ni mwalimu tena wa primary kabisa. Katika maisha yangu ya utumishi sijawahi kuona mzazi anaekaa bila kumpeleka mwanae shuleni akafundishwe na mtu ambae mzazi mwenyewe hamwamini kama mnavyosema humu ndani. Yaan mwalimu mnamuona kama ndezi fulani hivi wakati hata huku kuandika andika huku mlifunzwa na walimu.

Kibaya zaidi, hata watoto wenu mnawapelekaga private mnalipa mamilion kulipia A for Apple, B for Bapple, C for Chapple et.al. Nyie punguzeni madharau Ualimu ni fani nzuri tu tena yenye heshima na angalia safu ya pale juu kwenye serikali hii wote ni walimu ingawa wametusahau kwa muda sisi walimu wenzao.

Mwisho, serikali ione umuhimu wa kuboresha fani hii. Hasa hizi dharau ni kwakuwa maboresho yake yapo chini sana. Walimu na Sisi tujaliwe mfano kuwe na madaraja mahususi kwa walimu wanaojiendeleza kwenye level za MA na PhD kulikoni ilivyo sasa ambapo unaambiwaa unajifurahisha ukiwa na level hizo za Elimu. Pia nasi tunastaili posho za chakula, makazi na za wenza wetu kama wajeda na kada nyingine
 
Muwe wanasiasa mkuu kazi mbona zipo nyingi za kufanya,,,, sasa mkuu hivi kwa nchi hii unaweza kutamani kuwa mwalimu? Au kufanya kazi kwenye hizi halmashauri? Si bora ufuge kuku tyuu zitakulipa
Samahani mkuu kama watu wote watazikimbia ajira za ualimu nani atatufundishia watoto wetu?
 
Hii nchi ina shida moja, ingawa tumeambiwa hapa kazi tu lakini mitazamo ya watanzania wengi kuwa kazi lazima wakafanye huko kwenye makampuni sijui mashirika 'useless'.

Dharau kubwa hapa ni kuajiriliwa kwenye halmashauri na hasa mtu kuwa mwalimu. Huu ni upuuzi mkubwa sana.

Naomba kutanguliza kwanza mimi ni mwalimu tena wa primary kabisa. Katika maisha yangu ya utumishi sijawahi kuona mzazi anaekaa bila kumpeleka mwanae shuleni akafundishwe na mtu ambae mzazi mwenyewe hamwamini kama mnavyosema humu ndani. Yaan mwalimu mnamuona kama ndezi fulani hivi wakati hata huku kuandika andika huku mlifunzwa na walimu.

Kibaya zaidi, hata watoto wenu mnawapelekaga private mnalipa mamilion kulipia A for Apple, B for Bapple, C for Chapple et.al. Nyie punguzeni madharau Ualimu ni fani nzuri tu tena yenye heshima na angalia safu ya pale juu kwenye serikali hii wote ni walimu ingawa wametusahau kwa muda sisi walimu wenzao.

Mwisho, serikali ione umuhimu wa kuboresha fani hii. Hasa hizi dharau ni kwakuwa maboresho yake yapo chini sana. Walimu na Sisi tujaliwe mfano kuwe na madaraja mahususi kwa walimu wanaojiendeleza kwenye level za MA na PhD kulikoni ilivyo sasa ambapo unaambiwaa unajifurahisha ukiwa na level hizo za Elimu. Pia nasi tunastaili posho za chakula, makazi na za wenza wetu kama wajeda na kada nyingine
Tatizo la Mwl. wa Tanzania ni mwl mwenyewe.Ona Rais,Makamu na Waziri mkuu wote pamoja na wenza wao ni walimu,lakini ni mwaka wa nne walimu hawajapata japo increment achilia mbali nyongeza.
Poleni na kinachoendelea,yajayo hayajulikani
 
Kuajiriwa haiitwi tukutajirishe. Ajira ni kama biashara nyingine yoyote ile. Unauza muda wako na ujuzi wako kwa masaa 40 kwa wiki kwa hela hiyo unayopata mwisho wa mwezi.
Kama huridhiki na mkataba huo, unauacha na kuutafuta mwingine. Au unaongeza shughuli nyingine unapopata muda.
Hamna utumwa wowote. Ni wewe mwenyewe kuogopa kufanya maamuzi mengine.
Kwani duka lako likiwa halikulipi, unafanyaje?

Tena watumishi wa serikali huwa wananichekesha wakiita ajira zao ni utumwa.
Mfano, mtu analipwa average ya 700,000 yaani 31,800 per day. Kumbuka hiyo sio mapato bali faida (in business terms); halafu kazi zenyewe anategea na analipua. Huku kuna fundi ujenzi anapandisha tofali siku nzima kwa hela robo tatu ya hiyo na akizingua halipwi. Ila bado mtumishi wa serikali anajiita mtumwa. Hela nyingine iliyokatwa inaenda kwenye haki zake zingine na madeni, bado anajiita mtumwa. Ajira yake ni dhamana ya kuchukua mkopo popote pale kirahisiii, bado anajiita mtumwa. Kasoma mwenyewe, mkataba kasaini mwenyewe, na ana-cheat kazini na bado anakula mshahara na miposho.
Akienda sekta binafsi anasema, kule wana roho mbaya! Kumbe ni kwa sababu sekta binafsi hawawezi kumlipa mtu mshahara anayetegea kazi maana ni kujipa hasara.
Lakini bado atatoka kazini, atakuja mtaani atasema, "Tanzania bado sana, vyuma vikali".
Yaani yeye kaitapeli serikali, halafu yeye ndio mtendaji wa hiyo hiyo serikali, halafu tena anakuja kuungana na wengine mtaani kutukana serikali kuwa imejaa wezi ndio maana hatuendelei. Yeye keshaiibia hiyo hiyo serikali kwa kuwa overpaid zaidi ya kazi anayoifanya, lakini bado kelele.
Sasa hapo ndio utajiuliza, kama Serikali sio watendaji wake, Serikali ni nini?
 
Hii nchi ina shida moja, ingawa tumeambiwa hapa kazi tu lakini mitazamo ya watanzania wengi kuwa kazi lazima wakafanye huko kwenye makampuni sijui mashirika 'useless'.

Dharau kubwa hapa ni kuajiriliwa kwenye halmashauri na hasa mtu kuwa mwalimu. Huu ni upuuzi mkubwa sana.

Naomba kutanguliza kwanza mimi ni mwalimu tena wa primary kabisa. Katika maisha yangu ya utumishi sijawahi kuona mzazi anaekaa bila kumpeleka mwanae shuleni akafundishwe na mtu ambae mzazi mwenyewe hamwamini kama mnavyosema humu ndani. Yaan mwalimu mnamuona kama ndezi fulani hivi wakati hata huku kuandika andika huku mlifunzwa na walimu.

Kibaya zaidi, hata watoto wenu mnawapelekaga private mnalipa mamilion kulipia A for Apple, B for Bapple, C for Chapple et.al. Nyie punguzeni madharau Ualimu ni fani nzuri tu tena yenye heshima na angalia safu ya pale juu kwenye serikali hii wote ni walimu ingawa wametusahau kwa muda sisi walimu wenzao.

Mwisho, serikali ione umuhimu wa kuboresha fani hii. Hasa hizi dharau ni kwakuwa maboresho yake yapo chini sana. Walimu na Sisi tujaliwe mfano kuwe na madaraja mahususi kwa walimu wanaojiendeleza kwenye level za MA na PhD kulikoni ilivyo sasa ambapo unaambiwaa unajifurahisha ukiwa na level hizo za Elimu. Pia nasi tunastaili posho za chakula, makazi na za wenza wetu kama wajeda na kada nyingine
Ni bora tukawapeleka huko maana walimu wa private nao lazima wafundishe kwa nguvu zote na juhudi zote njaa yao sio Kali sana kama nyie mnaotembea na mihogo kwenye vibegi au kashata au barafu za kuja kuwauzia wanafunzi,
Pia mwalimu wa private asipofundisha vizuri anafukuzwa sasa nyie huko government nani atakufukuza hata kama hujui lolote unakuwa unawajaza tu ujinga watoto.
Na naiomba tu serikali nyie walimu wasiwaongezee hata mia maana hamjielewi nyie na hamna hamfanyi kazi ipasavyo mpo mpo tu mnalalamika salary ndogo salary ndogo,, mnafanya kazi kiujanja ujanja mnataka salary kubwa ya nini? Ili muoongeze wake? Maana wafanyakazi wa government wanaongoza kwa kuwa na wake wengi ni walimu na police
 
Kuajiriwa haiitwi tukutajirishe. Ajira ni kama biashara nyingine yoyote ile. Unauza muda wako na ujuzi wako kwa masaa 40 kwa wiki kwa hela hiyo unayopata mwisho wa mwezi.
Kama huridhiki na mkataba huo, unauacha na kuutafuta mwingine. Au unaongeza shughuli nyingine unapopata muda.
Hamna utumwa wowote. Ni wewe mwenyewe kuogopa kufanya maamuzi mengine.
Kwani duka lako likiwa halikulipi, unafanyaje?

Tena watumishi wa serikali huwa wananichekesha wakiita ajira zao ni utumwa.
Mfano, mtu analipwa average ya 700,000 yaani 31,800 per day. Kumbuka hiyo sio mapato bali faida (in business terms); halafu kazi zenyewe anategea na analipua. Huku kuna fundi ujenzi anapandisha tofali siku nzima kwa hela robo tatu ya hiyo na akizingua halipwi. Ila bado mtumishi wa serikali anajiita mtumwa. Hela nyingine iliyokatwa inaenda kwenye haki zake zingine na madeni, bado anajiita mtumwa. Ajira yake ni dhamana ya kuchukua mkopo popote pale kirahisiii, bado anajiita mtumwa. Kasoma mwenyewe, mkataba kasaini mwenyewe, na ana-cheat kazini na bado anakula mshahara na miposho.
Akienda sekta binafsi anasema, kule wana roho mbaya! Kumbe ni kwa sababu sekta binafsi hawawezi kumlipa mtu mshahara anayetegea kazi maana ni kujipa hasara.
Lakini bado atatoka kazini, atakuja mtaani atasema, "Tanzania bado sana, vyuma vikali".
Yaani yeye kaitapeli serikali, halafu yeye ndio mtendaji wa hiyo hiyo serikali, halafu tena anakuja kuungana na wengine mtaani kutukana serikali kuwa imejaa wezi ndio maana hatuendelei. Yeye keshaiibia hiyo hiyo serikali kwa kuwa overpaid zaidi ya kazi anayoifanya, lakini bado kelele.
Sasa hapo ndio utajiuliza, kama Serikali sio watendaji wake, Serikali ni nini?
Wanaibia serikali tuu magufuri akaze hapo hapo hakuna kuongeza hata mia, mpaka wajielewe kwanza
 
Back
Top Bottom