Watumishi wa Halmashauri wana mishahara duni

paqwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2019
Posts
2,106
Reaction score
2,831
Kama kuna kitu nime-note kwenye mabango ya Mei Mosi ni kuwa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa, yaani Halmashauri n.k., wana hali mbaya sana.

Ukiangalia mabango yao wengi wanaomba mishahara ipande na maslahi yao, lakini watu wa taasisi mfano WCF, Wizarani, PSSSF, TASAC, TPA wao wapo busy na mabango ya "mazoezi ni afya. ..mara chanjo".

Ipo haja ya kuwaangalia kwanza hawa wa Local Government, wamechoka sana ,kwa sura na kiuchumi.
 
Watumishi wote wa Serikali lakini wengine viwango juu na wengine chini?
 
Naomba kuuliza iwapo kuna tofauti ya kimaana ama kisheria kuhusu "wafanyakazi wa serikali" na "watumishi wa serikali"


JESUS IS SAVIOR
 
Nawaza tu kuwa Kama PAYE nayo si itakuwa kubwa sana. Sikatai mshahara kupanda labda wangeongezewa wafanyakazi percentage ya hela ya kiinua mgongo.Mfano serikali itoe 30% au 40% mfanyakazi achangie 10% au 15%
 
Namshukuru Sana Rais samia pia nampa pole sana pia nampongeza walau kwa kuajiri japo kidogo,najua miradi iliyoachwa na mwenda zake ni mingi mikubwa na inayokula pesa mingi kwelikweli, kwa juhudi unazozifanya tunafahamu muda utafika mamiradi yatakwisha watanzania tutafaidi ukubwa wa mishahara minono,tuvute subra kidogo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…