Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Taarifa za dini ya mtu ni muhimu. Labda hatujakaa tufikiri vizuri tu.Mfano, watumishi wanakufa kila leo na wanahitaji huduma kwa mujibu wa dini zao. Kama serikali haina taarifa sahihi itawahudumiaje hawa watu?
kwani ndugu na jirani hawajui dini yake mpaka aandike kwenye CV?
 
Point kubwa:

Kuna faida kubwa sana kuacha kuulizana Dini na Kabila, kuliko kuyadadisi.

Unataka upate tija gani ktk utendaji wa mtumishi?

Au tusalishane maofisini, au tuongee kikabila.
Ndio hapo , sijui wanatuchukuliaje !
 
Taarifa za watumishi wote zitapelekwa Kwa Msajili wa Hazina.
Nafikiri ipo chini ya Wizara ya Fedha.
Hawa ndio wasimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma.
Msajili wa hazina amekosa kazi za kufanya kiasi Hichi?
Hata wamama wavaa Madera hawaulizagi kabila. Ukileta za kuleta unasutwa kwa kiswahili ukianza kulia na kujutia kosa mchezo umeisha.
 
Sijui lakini labda wewe ndio ume ipa hype, mimi sijawahi kuwaza kwamba ita niadhiri maana hata hospitali huwa wana niuliza hivo hivo na sikuwahi kuwaza tofauti
 
Taarifa za dini sio muhimu, badala ya kulazmisha dini kwa kigezo cha kifo ni vyema hao watumishi wafundishwe kuandika wosia au wawe wanajaza fomu fupi za wakifa wanataka wazikweje.
Point kubwa sana hii.

Halafu hawa wanaosema mara vifo mara maziko.
Wajue, ktk taratibu za mazishi, serikali haihusiki kabisa
Serikali hutoa ubani tu wa rambirambi, na kusafirisha tu.
Mambo yote, hufanywa na ndugu, jamaa, basi!
 
kwa hiyo wako sahihi ila tu kwa nini wahoji leo? weka facts acha kulialia. Logic ya kutaka dini na kabila ni ipi,weka facts
Tunapinga udini na ukabila
 
Vyote vinatakiwa vifutwe.
Haijalishi ni nani alileta.
Kama huoni hatari mbele, endelea kutulia.
 
Kwani anataka kuteua watumishi wote yeye apange safu yake aweke dini na kabila alionalo lamfaa
 
Ina sikitisha sana ukiangalia mitandaoni watanzania ni watu wa kulalamika na kutukana tu hakuna mwenye suluhisho. Sasa kama unafuta sheria una ogops nini mtu kujua dini na kabila lako, yani mpaka mtu uwe na hofu hiyo lazima utakua mdini ma mkabila.
 
Ndugu yangu, jamaa anasema tuache kazi apate kazi, sijui anamaanisha nini .

Leo Kila sehemu tukianza kuulizana Dini na Kabila, tutakuwa na Taifa kweli.!
 
Acha wenge jaza fomu hiyo mama yuko kazini
 
kwa hiyo wako sahihi ila tu kwa nini wahoji leo? weka facts acha kulialia. Logic ya kutaka dini na kabila ni ipi,weka facts
Tunapinga udini na ukabila
Hata mimi wakati naomba ajira nilijaza.
Ila leo wanataka nini?
Dini ili iweje, tusalishane?
Kabila la nini?
Je tutapima utendaji wa mtumishi kwa kuangalia hizo Kabila? Au Dini?
 
Unawaza kujua Kabila na Dini ya mtu Kwa ajili ya maziko??? Kweli...
You are so myopic. Una upeo mfupi sana.
Wakristo mbona mna hofu Sana,au kwakuwa mmejazana kwenye maofisi mnajishtukia, muacheni Rais apige kazi,hizi kelele mngezipiga kipindi kile Cha dikteta
 
Zamani walikuwa wanawaondoa watu wanaotaka kuivuruga ccm, kwa kuwaita dodoma, sasa hawa wanaoplan mazito kuliko kuigusa ccm nadhani ni kuwashughulikia fasta zaidi, kwa wale TISS wazalendo maana hata TISS imeshavamiwa bila shaka sasa mwisho wa siku nahisi kila eneo litatekwa na hawa wavuruga nchi,
 
Just imaging, kwenye ardhi unam - substitute Lukuvi kwa rizi-one, hii ni akili timamu au matope??? alafu wasio jielewa bado wanasema oohoo atatuvusha tuuu…………………….
 
Use mkweli siku zingine! Magufuli alitumbua yeyote pamoja na wasukuma! Kama akina Charles Kitwanga waziri wa mambo ya ndani pamoja Charles Mlingwa mkuu wa mkoa wa mara! Msiwe waongo kwa chuki zenu za kikabila!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…