Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Watumishi wa Umma waombwa na Hazina kuorodhesha Dini na Kabila zao. Rais Samia na Wasaidizi wako, haya yanafanyika kwa lengo gani?

Huku kwenye taaluma yetu hiyo ni criteria ingawa it is qualified not absolute. Na imeisaidia sana Mahakama kufikia maamuzi ya haki mara kadhaa.

Nikuongezee mfano mwingine wa kwenye kesi za udhalilishaji (defamation). Kuna kabila mtu akikutamkia neno flani linakuwa ni udhalilishaji kwa kabila hilo, lakini kwa kabila lingine ni utani. Kwahiyo wafanya maamuzi wa Mahakama wanapaswa kulizingatia hili kabla ya kufanya maamuzi, vinginevyo watu watawajibishwa/kutowajibishwa kimakosa halafu mrudi humu kulalamika.

Hivyo ni lazima uelewe kwamba kwenye baadhi ya maeneo ni lazima ubainishe kabila lako kwa dhumuni jema kabisa ambalo huenda likakusaidia wewe mwenyewe.
Pengine upo sahihi!
Sasa hilo dhumuni linasomewa kozi gani ili lieleweke??
Mimi nadhani ifike mahali tukubaliane kuwa tuna vitambulisho rasmi vinavyopaswa kututambulisha kokote pale. Na hivyo vitambulisho vimebeba taarifa nyingi na nyeti sana! Kwanini zisiwe synchronized??
Mbona mitandao ya simu imefanikiwa?? Kwamba namba ya NIDA au kivuli cha kitambulisho husika kinatosha kutumika kutafuta taarifa nyingine pindi zinapohitajika.
Huko maofisini na kwingineko watu wasiombwe ombwe tena hizo taarifa sensitive!

NB: Kwa kuwa mnawaomba omba hizo taarifa wakiwatuhumu kwa udini na ukabila msikatae...!
 
Habari wana JF ..

Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.

Mimi niwaombe Serikali, niwaombe CCM, niwaombe washauri wa Rais, kama mmechoka, mtuachie hili Taifa.
Wengine bado tunataka kuliona Taifa letu likiwa moja.

Vyombo vya usalama, basi mshaurini mheshimiwa Rais vizuri, msijisahau sana mkaiacha nchi kwenye auto-pilot.
Niwakumbusheni Taifa hili halikujengwa kwa matofali, la hasha!

Mpitisheni Mh. Rais katika historia ndogo ndogo zile njema, zilizotufanya Watanzania japo tukawa wamoja, potelea pote na umaskini wetu.

Sasa hamuwezi amini, leo hii Hazina inaomba taarifa za watumishi (CV), na miongoni mwa taarifa wanazotakiwa kujaza hao watumishi ni:-
1. Kabila lako .....
2. Dini yako .......

Zipo taarifa zingine, za kipuuzi zinazoombwa, ila haina haja sana kuzitaja, kwani hazina athari sana kama hizi mbili.

Hivi kweli, leo mnataka DINI ya mtumishi, iwasaidie nini?
Hii taarifa mnaitumia kuboresha nini?
Udini wa nini katika Tz ya leo.
Tuna ajenda gani na Dini za watu, (watumishi). DINI, DINI.....DINI...!!!!?....,leo tunauliza DINI yako ni ipi? Kweli mh. Rais Samia.

Halafu mnataka na KABILA, kabila la mtumishi litumike kuboresha nini?
Mna ajenda gani huko?

KABILA, leo mnamuuliza mtu KABILA. Kweli mh Rais Samia , ulisema wewe huna kabila, sijui ni Mzanzibar, sasa hawa watumishi, karne ya 21, mwaka 2022, wawajazie makabila yao, muyajue, myafanyie nini?!

Mh Rais Samia, hebu kataa mambo mengine.

Siku Taifa hili likiparaganyika mikononi mwako, hao unaowaona, watakukataa.

Mfumo wa CV (format) na taarifa zinazotakiwa nimeambatanisha hapa.
denooJ , MTAZAMO , barafu , Tindo , Chige , shige2 , Malcolm X5 , MALCOM LUMUMBA ,

Mzee hii ni simple sana kung'amua.

Mfumo wa nchi umeshakwama kutambua raia wake na wale wa kigeni

Kuna baadhi ya taarifa zinasema kuna mapandikizi wa kigeni mpaka kwenye mifumo yetu ya usalama.

Sasa katika kushindwa huko, sasa wanatonesha dhahiri kuwa shughuli ewashinda na hii mannual aunthentication ndo inaenda kuharibu zaidi. Hawajui kukimbiza mwivi kimya kimya.

Hii mifumo yetu ya usalama ingelikuwa chama cha siasa, tungebadili tuweke wengine. Lakini mfumo wetu imara umejengwa kwenye misingi ya kisiasa ndo maana hata teknolojia ya udukuzi hawaumizi vichwa kuja na gadgets bali wanaagiza Israel ambao nao pia wanawadukua

Hii fomu ni kinyume na Katiba ya Tanzania
 
Polisi wanachukua taarifa za dini ya mtu na kabila lake, sijawahi kuona watu wakihoji hili
Ni makosa sana... Ni sawa na wale wanaochukua taarifa za jinsia ya mtu... Unaweza kuta mtu mwenyewe hana uhakika na jinsia yake!!

Tupinge dalili za ubaguzi pindi tuzionapo!!
 
Mama anataka kufanya usawa wa kidini kwenye uteuzi.

Huoni leo akiteua mkirito lazima ateue na musilamu, akiondoa mkiristo anaweka muislamu.

Angalia baraza la mawaziri toka ameingia, ameondoa wakristo 7 akateua waislamu 7 ila akawawekea wasaidizi wakristo.

Yeye mama akiteua boss muislamu basi msaidizi wake ni mkiristo.

Kwa sasa anataka dini zenu ili anapofanya uteuzi ajue wewe ni dini gani akupe ama ampe mwingine.

Wanasema wanataka kuvunja mfumo kristo.
Usawa wa kidini ni ushenzi tu.

Ina maana nchi hii ni ya wakristo na waislam pekee?

Nawaambia itakuja mvua kufagia fagia hizi taka za udini mshangae
 
Kwa uzoefu wangu hizi taarifa sio mpya kwenye utumishi wa umma, unapoajiriwa kwa mara ya kwanza taarifa hizo huwa zinachukuliwa kupitia fomu flani ambayo mtumishi huwa anajaza. Pia, kama upo Wizarani na umefanyiwa vetting, taarifa za ajabu ajabu kama hizo huhitajika ikiwemo hadi details za wakwe zako na dada na kaka wa mkeo. Mimi kwangu cha kushangaza, kwanini wanazitaka hivi sasa wakati tayari taarifa hizo zote wanazo? Ni uvivu wa kupekua nyaraka au?
Kwa leo zinahitajikaje?
 
Ni makosa sana... Ni sawa na wale wanaochukua taarifa za jinsia ya mtu... Unaweza kuta mtu mwenyewe hana uhakika na jinsia yake!!

Tupinge dalili za ubaguzi pindi tuzionapo!!
bora wewe uko fair.

Wengine hawana tabu na tatizo kuchukua taarifa za jinsia, marital status ila inapokuja suala la Dini wanang'aka kwelikweli. Huenda ni kwa sababu wanataka ajira za serikalini ziende kwa watu wa dini yao halafu hayo yafanyike gizani
 
Kwa leo zinahitajikaje?
Ni jambo la kawaida, sio jambo geni labda kama wewe ni mgeni kwenye utumishi wa umma. Hizo takwimu, ni muhimu sana kujua, kwasasa Serikalini waislamu ni wa kumulika na tochi, binafsi sijui ni kwa nini.
 
kwa hiyo wako sahihi ila tu kwa nini wahoji leo? weka facts acha kulialia. Logic ya kutaka dini na kabila ni ipi,weka facts
Tunapinga udini na ukabila
Twende kwenye hizo facts;

2015-2020 ulikuwa na miaka miwili (infant) kwamba hukuona lolote linaloendelea?!!

Ulikuwa na usonji kwamba hukuona chochote chenye uashiria wa udini au ukabila ukakikemea?!!

Kama issue ni kufuta hivyo vipengele, kwanini mng'ang'anie kumshambulia huyu mama kuwa mdini wakati kavikuta wala hajavianzisha yeye?!! Si angalau mngetoa ushauri kwa serikali kwa ujumla wake kuwa iviondoe. Sasa suala la anataka kuweka waislamu wenzie linatoka wapi km sio chuki za kidini?!!

Mna chuki sana nyie!!
 
Tanzania ni nchi ya kijinga sana.

Sasa kwa mfano hali ya ndoa ya mtu inahusu nini? Inahusiana nini na kazi aifanyayo mtu?
Ni mengi ya kushangaza. Hawakusaidii kulea mke au hawara, ila wanataka mtumishi uwaambie.
Ni kama vile ofisi za umma hazina KPIs..
 
Waandishi wa habari nchi hii hopeless kabisa zingekuwa nchi zingine zilizoendelea wangekuwa wangemshukia kama mwewe kuhoji waziri wa fedha au Raisi

Naomba BBC wamhoji raisi ukabila na udini wa mini na motive ya hii kitu ni nini?

BBC hojini Rais hilo
Mbona jinsia imewekwa hapo na huoni Kama tatizo!?..kinachokutisha kujua dini za watz ni nini!?
 
Pengine upo sahihi!
Sasa hilo dhumuni linasomewa kozi gani ili lieleweke??
Mimi nadhani ifike mahali tukubaliane kuwa tuna vitambulisho rasmi vinavyopaswa kututambulisha kokote pale. Na hivyo vitambulisho vimebeba taarifa nyingi na nyeti sana! Kwanini zisiwe synchronized??
Mbona mitandao ya simu imefanikiwa?? Kwamba namba ya NIDA au kivuli cha kitambulisho husika kinatosha kutumika kutafuta taarifa nyingine pindi zinapohitajika.
Huko maofisini na kwingineko watu wasiombwe ombwe tena hizo taarifa sensitive!

NB: Kwa kuwa mnawaomba omba hizo taarifa wakiwatuhumu kwa udini na ukabila msikatae...!
Unajua kuna mtu ukisoma comment yake unajua kabisa ana akili na anaitumia ipasavyo, wewe ni mmoja wao mkuu, hongera! Umeeleza vizuri sana. Na kama kuna wadau wa mamlaka zinazohusika na hili basi hawanabudi kuufanyia kazi ushauri wako.
 
Du hata kwenye sensa kipengele cha dini na kabila halipo,kwa kuamini Tanzania haina udini na ukabila, hata ukitaka kufanya tafiti mojawapo ya masharti ya kupitishwa kwa dodoso la utafiti ni kutokuweka kipengele cha dini na kabila.
Ni kweli, unataka kufanya utafiti, utalazimika kutouliza Dini, Kabila. Na hii ni sahihi kabisa.
Umri sawa, una maana. Jinsia, ina maana. Elimu ina maana
Dini na Kabila vinatija gani? Tunataka kuamua jambo gani?
 
Unataka kujaza wat Serikalini kwa dini zao na si kwa ubora wa viwango? Ndiyo sababu mmemtoa Lukuvi na kumweka Riziwani? Hii nchi si ya kidini. Kama mnataka kujenga nchi kwa misingi ya dini nendeni mkaanzishe himaya kwenye jangwa la Syria halina watu. Tanzania ni ya watu wote bila kujadli dini wala makabila yao. Usinipe hasira kwa kuonyesha ujinga.
Ni jambo la kawaida, sio jambo geni labda kama wewe ni mgeni kwenye utumishi wa umma. Hizo takwimu, ni muhimu sana kujua, kwasasa Serikalini waislamu ni wa kumulika na tochi, binafsi sijui ni kwa nini.
 
Data na information yoyote ya mambo ya kijamii ni muhimu kwa serikali. Inasaidia serikali kwenye mambo mengi ikiwemo affirmative action ikibidi au kwenye kuzuia udini na ukabila kwenye ajira.
Basi tufufue na matamasha ya kikabila na kidini, na yafanyike Kila mkoa, na serikali isimamie.
Na hizi Ngoma za kikabila zifanywe Kila shule, na ziende hadi Taifa.
Tushindanishe na Dini,
Tufungue kabisa, serikali ijue watu wake.
Asante.
 
Habari wana JF ..

Mimi niliahidi sitamkosoa Rais Samia, kwa sababu nilishawakosoa sana ma Rais wa nchi hii hadi nachoka; lakini Kuna mambo ni mazito huwezi hata kufikiri yanaweza kufanyika kwa karne hii.

Mimi niwaombe Serikali, niwaombe CCM, niwaombe washauri wa Rais, kama mmechoka, mtuachie hili Taifa.
Wengine bado tunataka kuliona Taifa letu likiwa moja.

Vyombo vya usalama, basi mshaurini mheshimiwa Rais vizuri, msijisahau sana mkaiacha nchi kwenye auto-pilot.
Niwakumbusheni Taifa hili halikujengwa kwa matofali, la hasha!

Mpitisheni Mh. Rais katika historia ndogo ndogo zile njema, zilizotufanya Watanzania japo tukawa wamoja, potelea pote na umaskini wetu.

Sasa hamuwezi amini, leo hii Hazina inaomba taarifa za watumishi (CV), na miongoni mwa taarifa wanazotakiwa kujaza hao watumishi ni:-
1. Kabila lako .....
2. Dini yako .......

Zipo taarifa zingine, za kipuuzi zinazoombwa, ila haina haja sana kuzitaja, kwani hazina athari sana kama hizi mbili.

Hivi kweli, leo mnataka DINI ya mtumishi, iwasaidie nini?
Hii taarifa mnaitumia kuboresha nini?
Udini wa nini katika Tz ya leo.
Tuna ajenda gani na Dini za watu, (watumishi). DINI, DINI.....DINI...!!!!?....,leo tunauliza DINI yako ni ipi? Kweli mh. Rais Samia.

Halafu mnataka na KABILA, kabila la mtumishi litumike kuboresha nini?
Mna ajenda gani huko?

KABILA, leo mnamuuliza mtu KABILA. Kweli mh Rais Samia , ulisema wewe huna kabila, sijui ni Mzanzibar, sasa hawa watumishi, karne ya 21, mwaka 2022, wawajazie makabila yao, muyajue, myafanyie nini?!

Mh Rais Samia, hebu kataa mambo mengine.

Siku Taifa hili likiparaganyika mikononi mwako, hao unaowaona, watakukataa.

Mfumo wa CV (format) na taarifa zinazotakiwa nimeambatanisha hapa.
denooJ , MTAZAMO , barafu , Tindo , Chige , shige2 , Malcolm X5 , MALCOM LUMUMBA ,

Mkuu mbona hiyo form Ina mambo mengi mkuu, umeona dini na kabila tu
 
Back
Top Bottom