Watumishi wengi wa Serikali hawana tija. Mishahara inapotea bure

Watumishi wengi wa Serikali hawana tija. Mishahara inapotea bure

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,587
Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana. Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake.

Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.

Halafu unakuta mtu ana elimu nzuri kabisa.

Hii nchi dah.
 
Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.
 
Acheni wivu wakuu watumishi ndio watumiaji wazuri wa hela na wanafanya pesa izunguke..... mfanyabiashara wa duka kwa siku faida haizidi 50000 hawezi kwenda bar kutumia laki ila mtumishi kawaida TU kutumia hata laki mbili kwa siku moja....
 
Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana.

Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake...
Yaan kuna watumishi hawana faida hasa wale wa ustawi wa jamii
 
Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana.

Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake...
Tatizo serikalini hakuna targets kwa mfanyakazi na hawafanyiwi tathmini kwakua hawasign KPI na ndio wanakwamisha sana Taifa hizi performance na mafanikio tunayoona kwenye sekta binafsi wafanyakazi wake wana sifa sawa kabisa na hawa waserikali ni kwakua wamesoma vyuo hivi hivi lakini utamaduni wakifanya kazi kwa malengo ndio unawatofautisha
 
Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.
Mimi wakati nasoma shule ya msingi na sekondari kuna walimu waliingia darasani na kufundisha vipindi vitatu, vinne ama vitano tu kwa mwaka hali ni wazima kiafya na wakiwa wanakuja shuleni kama kawaida, wengine walitutumia wanafunzi kuandika notisi, kusahihisha mitihani na majaribio na hata mtihani wa mock wilaya fulani nilishiriki kusahihisha.

Si hivyo tu niliwahi kuachiwa na mwalimu wangu wa somo la jiografia shule fulani nikawaandikia wenzangu na mimi nikasimamia na kufanya mtihani uleule ila nilikuwa sipendi kuibia mitihani hivyo sikupata zote.

Nenda mahospitalini hali no ileile, nenda kwa maafisa wa shamba, mifugo na afya ni majanga matupu ndo maana hakuna mabadiliko ya kimaisha na kimapato kwa wananchi richa ya wataalam hao kuongezeka toka uhuru bali mapato yao yanashuka kwa sababu wanatumia njia zilezile na rutuba ya mashamba inazidi kudorora.

Hakika umesema jambo la kweli kabisa. Dawa ni kubadili methodi ya malipo yao na kuwalipa kwa masaa badala ya malipo ya mwezi na kwa wale walio vijijini au katani malipo yao masaa yao yajazwe huko huko wanapokwenda kufanya kazi.

Haiwezekani taifa liendelee kwa aina hii ya watumishi. Huko vijijini hali ya wananchi kiafya ni tete wakiteswa na ndwele zinazowezekana kuepukika kwa kutunza mazingira, kuzuia mazalia ya wadudu hatarishi kama nzi na mbu, kutumia vyandarua, kuchemsha maji na kutumia vyoo.

Badala ya kuzuia tuna kimbilia kuponya kwa sababu watumishi wetu wa afya wanaiibia serikali kwa kuutumia vibaya muda na kushindwa kutimiza wajibu wa majukumu yao waliyoandika barua maombi kuzifanya tena kwa mikataba halali.
 
Wivu ni kitu kibaya sana katika maisha ! Ukiona mtumishi amekaa bila kazi ujue kashatimiza wajibu wake ! Kama ni kero mbalimbali za umma wapo wa kuzisemea kwenye umma na huleta kwa watu wa chini na kufanyia kazi. Siyo kila mda mtumishi anakuwa busy ofisini kuna wakati kazi ambazo amepewa anakuwa ameshazimaliza kwanini asipumzike .
 
Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.
Eti kaulamba 🤣🤣
 
Back
Top Bottom