Wavaa nywele bandia wakiona picha hizi wanaumia sana

Wavaa nywele bandia wakiona picha hizi wanaumia sana

Son of Gamba

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2012
Posts
4,720
Reaction score
6,957
Binafsi nakerwa sana na Wanawake wenye tabia ya kuvaa wigs kichwani au kushonea nywele za bandia. Hii ni tabia ambayo kwakweli mimi huwa siipendi kabisa na huwa namwona Mwanamke wa namna hiyo kuwa ni mchafu na limbukeni.

Kwanini Wanawake msiridhike na kile mlichonacho? Kama nywele zako ni fupi, zitunze hivyo hivyo na unaweza ukazipendezesha bila kuvaa nywele za marehemu usiowajua wewe. Kuna mawigi mengine ni nywele halisi za watu, wengine ni marehemu, na wengine wana mikosi yao huko na wewe unavaa tu kichwani bila hata kutafakari. Wengine wameachiwa "laana" zisizofutika na wewe unavaa nywele zake na kumsaidia kubeba laana zake. Ndiyo maana Wanawake mnaandamwa na matatizo yasiyokwisha na mengine hata hamjui chanzo chake ni nini.
That is hair!.jpg

Naamini wavaa "mawigi" wakimtazama huyu binti na nywele zake za asili, wanaona wivu sana, roho zinawauma. Lakini binadamu siku zote tunafundishwa kushukuru kwa kila jambo. Mimi naamini MUNGU aliyewaumba wenye nywele fupi hakukosea, basi msivae mawigi, kwani kwa kufanya hivyo mnakuwa kama mnaukosoa uumbaji wa BABA MUNGU. Na wale wenye kunyoa nyusi zao pia, mnakera sana tena sana. Kwanini usitulie na uzuri wako wa asili?? Kwanini wanawake mnapenda kuwa FAKE?
SHORT HAIR.jpg

LUPITA HAIR.jpg
Jamani hata bila kuvaa "nywele za marehemu"(mawigi), kichwani bado mnapendeza sana tu. Ladies, be real!
 
Binafsi nakerwa sana na Wanawake wenye tabia ya kuvaa wigs kichwani au kushonea nywele za bandia. Hii ni tabia ambayo kwakweli mimi huwa siipendi kabisa na huwa namwona Mwanamke wa namna hiyo kuwa ni mchafu na limbukeni.

Kwanini Wanawake msiridhike na kile mlichonacho? Kama nywele zako ni fupi, zitunze hivyo hivyo na unaweza ukazipendezesha bila kuvaa nywele za marehemu usiowajua wewe. Kuna mawigi mengine ni nywele halisi za watu, wengine ni marehemu, na wengine wana mikosi yao huko na wewe unavaa tu kichwani bila hata kutafakari. Wengine wameachiwa "laana" zisizofutika na wewe unavaa nywele zake na kumsaidia kubeba laana zake. Ndiyo maana Wanawake mnaandamwa na matatizo yasiyokwisha na mengine hata hamjui chanzo chake ni nini.
View attachment 753448
Naamini wavaa "mawigi" wakimtazama huyu binti na nywele zake za asili, wanaona wivu sana, roho zinawauma. Lakini binadamu siku zote tunafundishwa kushukuru kwa kila jambo. Mimi naamini MUNGU aliyewaumba wenye nywele fupi hakukosea, basi msivae mawigi, kwani kwa kufanya hivyo mnakuwa kama mnaukosoa uumbaji wa BABA MUNGU. Na wale wenye kunyoa nyusi zao pia,

Siku zote Wanawake hufanya kile ambacho Wanaume huvutiwa nacho!
 
Watu Wanavichwa Vibaya Hawavai Kwakupenda Kaka[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hata kama anakichwa kibaya, anapaswa kuridhika na kile alichozaliwa nacho. Isitoshe hakuna binadamu mbaya, ni imani tu tuliyojiwekea vichwani mwetu kuwa mtu akiwa hivi ama vile, eti ni mbaya. Kila mwanadamu anapendeza jinsi alivyo akiwa na mwonekano wake wa asili.
 
Hata kama anakichwa kibaya, anapaswa kuridhika na kile alichozaliwa nacho. Isitoshe hakuna binadamu mbaya, ni imani tu tuliyojiwekea vichwani mwetu kuwa mtu akiwa hivi ama vile, eti ni mbaya. Kila mwanadamu anapendeza jinsi alivyo akiwa na mwonekano wake wa asili.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kaka Embu Utuache Bwna mawigy tutavaa Na Kunyoa Tutanyoa
 
Sasa nywele nivae mie kukereka ukereke wewe khaaa inahusu!!
Hiyo ndiyo kazi ya mvulana kutizama nani kavaa nini na kukereka!
Off-course, kila mnachokivaa mikitembea barabarani macho yanatazama na haijalishi anayetazama awe mwanamke au mwanaume, macho hayana pazia. Wanaume wengi sana tunakerwa na hayo manywele yenu ya bandia sema tu ninyi hamjui.

Naamini wanaume wengi kama mimi huwa tunavutiwa zaidi na wanawake wenye nywele halisi kuliko wale wanaoendekeza manywele ya "marehemu" sijui wa India sijuia wa Brazili sijui Peru, I don't know.

Mwanamke ni pambo, lakini pambo hili likianza kuwekewa manywele ya "bandia" linakuwa siyo pambo tena bali machukizo tu! Watazameni wanawake wa Kiarabu, Kizungu, Kichina na Kihindi; wao wako na nywele zao za asili na wanafurahia nywele zao za asili. Hata ninyi dada zetu wa Kibongo(Kiafrika), mtapendeza zaidi na zaidi kama mtazitunza nywele zenu za asili na kuona ufahari wa nywele zenu kuliko kukaa na kuzitukuza nywele bandia.
 
Sasa nywele nivae mie kukereka ukereke wewe khaaa inahusu!!
Hiyo ndiyo kazi ya mvulana kutizama nani kavaa nini na kukereka!


Aiseee kunywa soda hapo kwa mangi bili juu yangu
 
we n mtu wa ajabu Sana .
yani maisha ya MTU wew kwako keroo duuu
 
Mdada anavaa wigi akinyeshewa na mvua anakuwa kama kabeba kuku wa kisasa kichwani, mawigi mwengine yanatoa harufu kali hadi na mvuke.

Pia wigi linaendana na kichwa unakuta mtu ana Komwe anaenda kushonea kiwigi kama cha Rihanna hapo ukimwona kwa mbali utasema katuni za Kipanya.
 
we n mtu wa ajabu Sana .
yani maisha ya MTU wew kwako keroo duuu
Kama nakuona vile na wewe umevaa nywele za marehemu usiyemjua au umevaa maplastiki kichwani..... Tunakereka ndiyo sababu ninyi mpo ndani ya jamii hii hii na kila mnalolifanya linaweza kuwa linatupendeza sisi wanaume ama linatukera. Lile linalotukera lazima tuseme bila kuwaonea aibu.
 
Back
Top Bottom