Lovelovie
JF-Expert Member
- Oct 2, 2021
- 12,582
- 26,053
Sawa hakuna shida akikuzingua nakugawia kaka mwingineSubiri kwanza! Tuvute miaka
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sawa hakuna shida akikuzingua nakugawia kaka mwingineSubiri kwanza! Tuvute miaka
Sisi ni washika pembe tu mkuu. Nipe connection ya watawala nianze kukupigia promo 😁Nitatwanga hicho kichwa mpaka akili zikukae sawa.
Kabisa yani ,sijui nirudishe kadi tu🤔ATI hataki timu kataa ndoa😂😂😂
Kuna nn tena😂Kama eqn x 😂😂😂😂😂😂uuuuuuuuh uwiiiiiiiiiiii.
Bora Countrywide
Hapana kitu kaka angu 😁😁😁Kuna nn tena😂
Utakosa warembo kisa kataa ndoaKabisa yani ,sijui nirudishe kadi tu🤔
Koo za simba hatuulizwi namna hiyo, unakuta tayari unajijuwa ukimaliza kusoma, tena mara nyingi hawangoji kumaliza kusoma chuo, huku unaendelea kusoma huku unafungishwa ndoa kwenye koo ya kisimba. Sherehe baada ya masomo.Habari!
Nilipomaliza chuo nilipatwa na mkasa. Ile nimemaliza tu mitihani nikamtaarifu mama, tukaongea tu vizuri kwa muda mfupi chumbani kwake, sasa wakati natoka nje akaniuliza swali 'kwahiyo ushapata mtu wa kukuoa?' moyo ulishtuka halafu chap nikaendelea na safari hapo nikajifanya sijamsikia.
Ikawa wimbo anaoupenda 'ushapata wa kukuoa? Nikawa namwambia sipo tayari kwa sasa nikimjibu hivyo anaanza kutoa risala 'unajua inabidi uolewe mimi najisikia vibaya kukuona tu hapa nyumbani'
Siku moja nikamwambia mimi sijapata hata wa kunioa, akasema 'uzuri wote huo hakuna aliyesema anataka kukuoa' ilibidi tu nicheke mimi nilikuwa nishasoma akili yake kwamba uoga wa maisha unamsumbua.
Ishapita miaka 3 tokea kisa hiki kitokea, juzi nikasema acha niwaulize wenzangu kama wanakutana na maswahibu kama yangu sababu huu wimbo mama yangu bado anauimba.
Rafiki yangu FLORA
Yeye aliniambia alivyomaliza Mitihani alichelewa kurudi nyumbani kwa miezi kadhaa, sasa kuna siku akaumwa akalazwa mama yake alivyoenda hospital akamkuta Flora yupo na boyfriend wake ila huyo bf akawapisha waongee.
Mama yake akamuuliza 'huyo kijana ni nani' Flora akamjibu ni rafiki yake.
Mama yake akamwambia bills ni kiasi gani ili alipie! Flora akamwambia 'rafiki yangu ameshalipia' mama yake akaguna.
Sasa Flora alivyorudi kwao, mama yake akaanza kuimba nyimbo kila mara 'Yule rafiki yako yuko wapi akuoe kuliko kushinda ndani kila siku' Flora akaishia tu kucheka.
Rafiki yangu REBECCA
Yeye alikuwa anabanwa sana, ni wale watoto geti kali. Alivyomaliza chuo kuna siku akamuomba mama yake ruhusa ya kwenda kumsalimia rafiki yake. Mama yake hakumuuliza maswali mengi kama alivyokua anafanya hapo awali.
Jioni mapema Rebecca aliporudi mama yake akamwambia 'Mbona umerudi mapema' akamjibu nilienda kumuona tu mara moja. Mama yake akamwambia 'Ebu tembeatembea wachumba wakuone sio kujifungia tu ndani'
Ila ameniambia huo wimbo mama yake aliuacha baada ya yeye kupata kazi.
Rafiki yangu ASHA
Huyu ndiye amenichekesha sana, anasema tulivyomaliza chuo baba yake akawa anamwambia 'fanya uolewe sitaki kukuona nyumbani kwangu'
Kuna siku akaenda kazini kwa baba yake akamkuta yupo na wanaume wengine akawasalimia.
Kijana mmoja akamwambia mzee wake kwamba hakujua kama ana binti mkubwa vile! Mzee wake akajibu 'Huyu ni binti yangu kamaliza chuo mwaka huu na bado hajaolewa' wote wakaishia kucheka.
Haikupita miezi mingi baba yake akamletea mchumba, ubani ukachomwa sasa hivi yupo kwenye ndoa.
Nilichokiona wazazi wengi ambao hawajajipata kazi wanayotupa watoto wa kike ni kuolewa tena kama mtoto hajapata kazi ya kufanya.
Ila ukiwa na kazi nzuri unapata pesa, hii risala ya kuolewa hawatoi hata ukifikisha miaka 40.
Sasa sijui wa kulaumiwa ni CCM, wazazi wetu au sisi watoto.
Asha sema kuna mtu kamzimia na mimi simo lakini🤣Utakosa warembo kisa kataa ndoa
UNAZINGUA....!Countrywide ety ephen_ kasema ako single
Hakuna alomzimia huyu anatuzingua tu hap😁😁Ame
Asha sema kuna mtu kamzimia na mimi simo lakini🤣
Usipoolewa na kaka yangu yoyote mwaka huu.UNAZINGUA....!
Koo za simba tunaoana umri tu ukifika, tena wote tunakua na moto wa kuoa kuolewa.Kumlazimisha mtoto kuolewa si sawa.
Sitafuti mwenza, Ila akinipa napiga. Na naipiga vizuri tuCountrywide ety ephen_ kasema ako single
👺👺👺👺👺Mimi sipo single