Wazazi mmekuwaje?

Wazazi mmekuwaje?

Habari!

Nilipomaliza chuo nilipatwa na mkasa. Ile nimemaliza tu mitihani nikamtaarifu mama, tukaongea tu vizuri kwa muda mfupi chumbani kwake, sasa wakati natoka nje akaniuliza swali 'kwahiyo ushapata mtu wa kukuoa?' moyo ulishtuka halafu chap nikaendelea na safari hapo nikajifanya sijamsikia.

Ikawa wimbo anaoupenda 'ushapata wa kukuoa? Nikawa namwambia sipo tayari kwa sasa nikimjibu hivyo anaanza kutoa risala 'unajua inabidi uolewe mimi najisikia vibaya kukuona tu hapa nyumbani'

Siku moja nikamwambia mimi sijapata hata wa kunioa, akasema 'uzuri wote huo hakuna aliyesema anataka kukuoa' ilibidi tu nicheke mimi nilikuwa nishasoma akili yake kwamba uoga wa maisha unamsumbua.

Ishapita miaka 3 tokea kisa hiki kitokea, juzi nikasema acha niwaulize wenzangu kama wanakutana na maswahibu kama yangu sababu huu wimbo mama yangu bado anauimba.

Rafiki yangu FLORA
Yeye aliniambia alivyomaliza Mitihani alichelewa kurudi nyumbani kwa miezi kadhaa, sasa kuna siku akaumwa akalazwa mama yake alivyoenda hospital akamkuta Flora yupo na boyfriend wake ila huyo bf akawapisha waongee.

Mama yake akamuuliza 'huyo kijana ni nani' Flora akamjibu ni rafiki yake.
Mama yake akamwambia bills ni kiasi gani ili alipie! Flora akamwambia 'rafiki yangu ameshalipia' mama yake akaguna.

Sasa Flora alivyorudi kwao, mama yake akaanza kuimba nyimbo kila mara 'Yule rafiki yako yuko wapi akuoe kuliko kushinda ndani kila siku' Flora akaishia tu kucheka.

Rafiki yangu REBECCA
Yeye alikuwa anabanwa sana, ni wale watoto geti kali. Alivyomaliza chuo kuna siku akamuomba mama yake ruhusa ya kwenda kumsalimia rafiki yake. Mama yake hakumuuliza maswali mengi kama alivyokua anafanya hapo awali.

Jioni mapema Rebecca aliporudi mama yake akamwambia 'Mbona umerudi mapema' akamjibu nilienda kumuona tu mara moja. Mama yake akamwambia 'Ebu tembeatembea wachumba wakuone sio kujifungia tu ndani'

Ila ameniambia huo wimbo mama yake aliuacha baada ya yeye kupata kazi.

Rafiki yangu ASHA
Huyu ndiye amenichekesha sana, anasema tulivyomaliza chuo baba yake akawa anamwambia 'fanya uolewe sitaki kukuona nyumbani kwangu'

Kuna siku akaenda kazini kwa baba yake akamkuta yupo na wanaume wengine akawasalimia.
Kijana mmoja akamwambia mzee wake kwamba hakujua kama ana binti mkubwa vile! Mzee wake akajibu 'Huyu ni binti yangu kamaliza chuo mwaka huu na bado hajaolewa' wote wakaishia kucheka.

Haikupita miezi mingi baba yake akamletea mchumba, ubani ukachomwa sasa hivi yupo kwenye ndoa.

Nilichokiona wazazi wengi ambao hawajajipata kazi wanayotupa watoto wa kike ni kuolewa tena kama mtoto hajapata kazi ya kufanya.

Ila ukiwa na kazi nzuri unapata pesa, hii risala ya kuolewa hawatoi hata ukifikisha miaka 40.

Sasa sijui wa kulaumiwa ni CCM, wazazi wetu au sisi watoto.
Acha malalamiko binti, umefika muda, olewa au ondoka hapo nyumbani ukajitegemee. Wazazi wamechanga sana harusi na sendoff za watu. Ni muda wao nao kuitisha vikao, ebooo
 
Anaweza asiolewe ila washenzi wakamjaza mimba anatotoa watoto km kuku broiler hawana baba hapo hapo kwenu.
Miaka 25-30 fukuzilia mbali.
We unamjengea nyumba babaako na mama ila kuna litoto lipo linafukuliwa mitaro hapohapo nyumbani.
Hapo umekariri sio lazima kufanya hayo mapenzi , kujazwa mimba ni yeye ndio kataka
 
Sina mpango wa kuolewa, sifikirii hata kwa sasa
Yaani kuhusu ndoa mimi bado sana..!
Vp maswala yetu ya mengine... najua utando ulishatolewa pasina shaka.
 
Habari!

Nilipomaliza chuo nilipatwa na mkasa. Ile nimemaliza tu mitihani nikamtaarifu mama, tukaongea tu vizuri kwa muda mfupi chumbani kwake, sasa wakati natoka nje akaniuliza swali 'kwahiyo ushapata mtu wa kukuoa?' moyo ulishtuka halafu chap nikaendelea na safari hapo nikajifanya sijamsikia.

Ikawa wimbo anaoupenda 'ushapata wa kukuoa? Nikawa namwambia sipo tayari kwa sasa nikimjibu hivyo anaanza kutoa risala 'unajua inabidi uolewe mimi najisikia vibaya kukuona tu hapa nyumbani'

Siku moja nikamwambia mimi sijapata hata wa kunioa, akasema 'uzuri wote huo hakuna aliyesema anataka kukuoa' ilibidi tu nicheke mimi nilikuwa nishasoma akili yake kwamba uoga wa maisha unamsumbua.

Ishapita miaka 3 tokea kisa hiki kitokea, juzi nikasema acha niwaulize wenzangu kama wanakutana na maswahibu kama yangu sababu huu wimbo mama yangu bado anauimba.

Rafiki yangu FLORA
Yeye aliniambia alivyomaliza Mitihani alichelewa kurudi nyumbani kwa miezi kadhaa, sasa kuna siku akaumwa akalazwa mama yake alivyoenda hospital akamkuta Flora yupo na boyfriend wake ila huyo bf akawapisha waongee.

Mama yake akamuuliza 'huyo kijana ni nani' Flora akamjibu ni rafiki yake.
Mama yake akamwambia bills ni kiasi gani ili alipie! Flora akamwambia 'rafiki yangu ameshalipia' mama yake akaguna.

Sasa Flora alivyorudi kwao, mama yake akaanza kuimba nyimbo kila mara 'Yule rafiki yako yuko wapi akuoe kuliko kushinda ndani kila siku' Flora akaishia tu kucheka.

Rafiki yangu REBECCA
Yeye alikuwa anabanwa sana, ni wale watoto geti kali. Alivyomaliza chuo kuna siku akamuomba mama yake ruhusa ya kwenda kumsalimia rafiki yake. Mama yake hakumuuliza maswali mengi kama alivyokua anafanya hapo awali.

Jioni mapema Rebecca aliporudi mama yake akamwambia 'Mbona umerudi mapema' akamjibu nilienda kumuona tu mara moja. Mama yake akamwambia 'Ebu tembeatembea wachumba wakuone sio kujifungia tu ndani'

Ila ameniambia huo wimbo mama yake aliuacha baada ya yeye kupata kazi.

Rafiki yangu ASHA
Huyu ndiye amenichekesha sana, anasema tulivyomaliza chuo baba yake akawa anamwambia 'fanya uolewe sitaki kukuona nyumbani kwangu'

Kuna siku akaenda kazini kwa baba yake akamkuta yupo na wanaume wengine akawasalimia.
Kijana mmoja akamwambia mzee wake kwamba hakujua kama ana binti mkubwa vile! Mzee wake akajibu 'Huyu ni binti yangu kamaliza chuo mwaka huu na bado hajaolewa' wote wakaishia kucheka.

Haikupita miezi mingi baba yake akamletea mchumba, ubani ukachomwa sasa hivi yupo kwenye ndoa.

Nilichokiona wazazi wengi ambao hawajajipata kazi wanayotupa watoto wa kike ni kuolewa tena kama mtoto hajapata kazi ya kufanya.

Ila ukiwa na kazi nzuri unapata pesa, hii risala ya kuolewa hawatoi hata ukifikisha miaka 40.

Sasa sijui wa kulaumiwa ni CCM, wazazi wetu au sisi watoto.
Heshima ya Mwanamke yeyote hapa diniani ni KUOLEWA.

Kuna kitu labda wewe ephen_ na baadhi ya wanawake hamkijui vizuri, nitakufahamisha. Iko hivi;

MUNGU alimuumba Eva kwa lengo moja tu, la kuwa MKE wa Adamu. Hakukuwa na sababu nyingine zaidi ya hiyo.

Ukisoma Biblia utaona baada ya Eva kuumbwa BWANA MUNGU alimpeleka moja kwa moja kwa Adamu. Hakumpeleka sehemu nyingine youote ile ya Bustani bali alimpeleka pale alipo Adamu moja kwa moja.

Vivyo hivyo na ninyi Wanawake mmezaliwa ili muishi na Wanaume. Wewe ili ukamilike unapaswa kuwa na MUME.

Mama yako mzazi analitambua hilo na yuko SAHIHI kabisa kukukumbusha kuhusu kuolewa. Mwanamke hakuumbwa ili aishi peke yake hata kama ana pesa na mali zote za duniani bado ili akamilike kihisia na kimwili na kisaikolojia anahitaji MUME!

Tafiti mbalimbali zinaonesha Wanawake wanaoishi peke yao bila Mume wanapitia MSONGO MKUBWA wa mawazo maisha yao yote. Why? Because something is missing in their lives.

BWANA MUNGU alikutoa kwenye ubavu wa Mwanaume, hivyo ili ukamilike ni lazima uungane na MWANAUME. Kitendo cha kukutoa kwenye UBAVU wa Mwanaume kilikuwa na maana kubwa wala MUNGU hakufanya kwa kubahatisha.
 
Heshima ya Mwanamke yeyote hapa diniani ni KUOLEWA.

Kuna kitu labda wewe ephen_ na baadhi ya wanawake hamkijui vizuri, nitakufahamisha. Iko hivi;

MUNGU alimuumba Eva kwa lengo moja tu, la kuwa MKE wa Adamu. Hakukuwa na sababu nyingine zaidi ya hiyo.

Ukisoma Biblia utaona baada ya Eva kuumbwa BWANA MUNGU alimpeleka moja kwa moja kwa Adamu. Hakumpeleka sehemu nyingine youote ile ya Bustani bali alimpeleka pale alipo Adamu moja kwa moja.

Vivyo hivyo na ninyi Wanawake mmezaliwa ili muishi na Wanaume. Wewe ili ukamilike unapaswa kuwa na MUME.

Mama yako mzazi analitambua hilo na yuko SAHIHI kabisa kukukumbusha kuhusu kuolewa. Mwanamke hakuumbwa ili aishi peke yake hata kama ana pesa na mali zote za duniani bado ili akamilike kihisia na kimwili na kisaikolojia anahitaji MUME!

Tafiti mbalimbali zinaonesha Wanawake wanaoishi peke yao bila Mume wanapitia MSONGO MKUBWA wa mawazo maisha yao yote. Why? Because something is missing in their lives.

BWANA MUNGU alikutoa kwenye ubavu wa Mwanaume, hivyo ili ukamilike ni lazima uungane na MWANAUME. Kitendo cha kukutoa kwenye UBAVU wa Mwanaume kilikuwa na maana kubwa wala MUNGU hakufanya kwa kubahatisha.
Nimekuelewa vizuri sana!
Lakini tatizo lipo kwenye umri, wadau wanasema age ya 27+ ni ngumu kupata mtu wa kukuoa wakati mimi naona huo umri ndio sahihi mimi kuingia kwenye ndoa.
 
Nimekuelewa vizuri sana!
Lakini tatizo lipo kwenye umri, wadau wanasema age ya 27+ ni ngumu kupata mtu wa kukuoa wakati mimi naona huo umri ndio sahihi mimi kuingia kwenye ndoa.
27+ kwa Mwanamke ni umri mkubwa. Ukiolewa na 27+ unakuwa umebakiza 13 yrs kufika 40. Kipindi cha miaka 13 ni kifupi sana kwa Mumeo kukufurahia. Kipindi hicho utakuwa busy na masumbufu ya watoto, attention yako itakuwa kwa watoto na siku hazigandi ghafla miaka 40 hii hapa!
By the time unafika 40 unaanza kuzeeka automatically wakati huo Mumeo anawaona mabinti wadogo wenye 20yrs. Wewe tayari anakuona "Mzee" ndiyo hapo sasa unatafutiwa msaidizi kisirisiri.

Nikuambie kitu, mwanamke ili ufurahie maisha olewa ukiwa na 20 yrs to 23yrs.

Zaidi ya hapo ni stress tu.
 
27+ kwa Mwanamke ni umri mkubwa. Ukiolewa na 27+ unakuwa umebakiza 13 yrs kufika 40. Kipindi cha miaka 13 ni kifupi sana kwa Mumeo kukufurahia. Kipindi hicho utakuwa busy na masumbufu ya watoto, attention yako itakuwa kwa watoto na siku hazigandi ghafla miaka 40 hii hapa!
By the time unafika 40 unaanza kuzeeka automatically wakati huo Mumeo anawaona mabinti wadogo wenye 20yrs. Wewe tayari anakuona "Mzee" ndiyo hapo sasa unatafutiwa msaidizi kisirisiri.

Nikuambie kitu, mwanamke ili ufurahie maisha olewa ukiwa na 20 yrs to 23yrs.

Zaidi ya hapo ni stress tu.
Sasa nimegundua kua niolewe mapema ili nikazae mapema tupate muda mwingi wa kufurahi🙄
Maisha hayana formular atii! Sanasana kipindi hiki ambacho kila mtu anasumbuka na maisha.

Mimi nafata moyo wangu sababu kuna wengine wanaolewa na 20yrs ndoa inawashinda baada ya miaka 5 mwingine anaolewa na 30yrs na ndoa yake ina last.
 
Nimekuelewa vizuri sana!
Lakini tatizo lipo kwenye umri, wadau wanasema age ya 27+ ni ngumu kupata mtu wa kukuoa wakati mimi naona huo umri ndio sahihi mimi kuingia kwenye ndoa.
mwanamke hawezi kupanga ataolewa lini.

mimi nataka nikuoe mwaka huu alafu wew unasema hauko tayar hadi miaka 5 mbele nitakusubiria tuu kweli ?
Ni uongo...

labda mipango yako iendane na anaetaka kuoa kwa muda huo,
tofauti na hapo, muda wew upo tayari unakuta hamna wa kukuoa.
au unaolewa na mtu ilimradi tuu.

Kapeace amekupa mifano mizuri,

kaolewe mkuu mipango yako utatimiza tu hukohuko,

kwani usipoolewa ndo guarantee ya kutimiza malengo ?

feminists wanawaharibu
 
mwanamke hawezi kupanga ataolewa lini.

mimi nataka nikuoe mwaka huu alafu wew unasema hauko tayar hadi miaka 5 mbele nitakusubiria tuu kweli ?
Ni uongo...

labda mipango yako iendane na anaetaka kuoa kwa muda huo,
tofauti na hapo, muda wew upo tayari unakuta hamna wa kukuoa.
au unaolewa na mtu ilimradi tuu.

Kapeace amekupa mifano mizuri,

kaolewe mkuu mipango yako utatimiza tu hukohuko,

kwani usipoolewa ndo guarantee ya kutimiza malengo ?

feminists wanawaharibu
Ni kweli mkuu! Lakini kila mtu ana kitabu chake cha maisha na wala mimi sio feminist
 
Back
Top Bottom