Wazazi mnaofungia watoto ndani acheni ulimbukeni; mnawanyima watoto ujuzi wa kuyaishi maisha watayoishi ukubwani

Wazazi mnaofungia watoto ndani acheni ulimbukeni; mnawanyima watoto ujuzi wa kuyaishi maisha watayoishi ukubwani

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Sisemi kutoka kwenda mitaa ya mbali mbali kuzuruara mbali kama enzi zetu zamani, La hasha!! kwa sasa dunia imebadilika hivyo uhuru inabidi upungue lakini isiwe kuwanyima kabisa uhuru.

Ni vema uwe unamruhusu majirani marafiki zake wawe wanakuja kucheza nae kwako nae awe anaenda kwa marafiki zake wa jirani kucheza kwa sharti la kutoa taarifa mapema ili ujue sehemu alipo.

Hii mambo ya kufungia ndani watoto ni unyanyasaji, kumbuka huyo ni mtoto hivyo ni busara kumpa haki yake ya kuupitia utoto ila iwe chini ya uangalizi wako.

Unamzuia mtoto asitoke nje, huoni kwamba yupo hatarini kukosa uzoefu wa kujenga urafiki akaishia kuwa mtu anaependa kukaa pekeyake.

Unamfungia mtoto ndani awe anaangalia katuni ni nani kakwambia haya maisha yapo kikatuni katuni?

Unaogopa mtoto atapigwa na wenzie kwani sisi tulipokuwa watoto hatukupitia hivi vitu? Hata sisi tulipitia huko na tukajifunza mapema kujua kutatua hayo mambo aidha kwa kupambana nayo, kuyazuia, kujenga urafiki ili usaidiwe yakikukuta, n.k. Haya mambo hayakwepeki kwa kufungia ndani mtoto, yapo na atayakuta,

Maisha haya tumezungukwa na watu, huwezi fanya chochote bila watu, kuna watu wabaya na wazuri na kuwajua ni kwa kupata uzoefu wa kuishi nao na uzoefu huo kuupata ni lazima uishi nao, wazazi mnafungia watoto ndani waaicheze hata na wenzao majirani huu si uungwana.
 
Upumbav-u Cha mawazo ya Uswazi., Shenzi kabisa nyie ndio Mnalawiti watoto wa watu.
Ungekuwa karibu ningekulamba Makofi.
Cheza na wadogo zako na wanao.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]dingi punguza hasira
 
Kilawakati

Mbona una hasira kias hiki mkuu?jamaa kaandika mbona fresh tu kwa watoto kiume kulea hivo kwa kufungia fungia ndani ni hatari toto linakua lelemama haliwezi hata kujitetea.. nimesoma jamaa mmoja jirani alikua anafungiwa kifala boya sana yani mwili mkubwa ila haliwezi kupigana.
 
[emoji1787][emoji23] mbona una hasira kias hiki mkuu?jamaa kaandika mbona fresh tu kwa watoto kiume kulea hivo kwa kufungia fungia ndani ni hatari toto linakua lelemama haliwezi hata kujitetea.. nimesoma jamaa mmoja jirani alikua anafungiwa kifala boya sana yani mwili mkubwa ila haliwezi kupigana
Upumbavu mwingine huu
Kwa iyo kupigana ndo uanaume
 
Wanaofanya hivyo sio wajinga. Dunia imebadilika Sana.
Nyumba ikiongezeka panya inabidi uichome ili uwaue panya?

Dunia inabadilika lakini isiwe kisingizio cha kuwanyima kabisa watoto uhuru wao wa kufurahia utoto.
 
Asubuhi kulipokucha tuliona nazi mayai vyungu vimepasuliwa njiani kwa bahat mbaya kulikuea na watoto wakaogota nazi zile na kuanza kuzila kwa kugombaniana wengine walipita nakusema watu wanapadua nazi na kutupa wakat tunakuka maharage bila nazi,, watoto wale walijificha nakuzifakamia zile nazi.

Nakuuliza mtoa mada kwa style hiyo utamruhusu mwanao azurure au unaongea kwavile bado haujafanikiwa kutoa nyonga yako iishi hapa duniani.
 
Kwa hiyo unataka mtoto azurule tu mitaani na wenzao akirudi jioni sawa tu
Wengine sisi utotoni ndiyo tulikulia life style hiyo...sema ina hatari sana kwa mtoto

Ova
 
[emoji1787][emoji23] mbona una hasira kias hiki mkuu?jamaa kaandika mbona fresh tu kwa watoto kiume kulea hivo kwa kufungia fungia ndani ni hatari toto linakua lelemama haliwezi hata kujitetea.. nimesoma jamaa mmoja jirani alikua anafungiwa kifala boya sana yani mwili mkubwa ila haliwezi kupigana
Eti hajui kupigana kwani umesikia wanaandaa mabondia
 
Back
Top Bottom