Wazazi mnashirikiana na shule kuwatesa watoto

Wazazi mnashirikiana na shule kuwatesa watoto

Unapoint👏👏 imefika hatua secondary wanatoka mapema kuliko primary!! mfano mdogo tu huku arusha,Wanafunz wa Olorien secondary wanatoka saa tisa na nusu halaf wa Olorien primary(class 4&6&7) wanatoka saa kumi na moja😒
 
Niliwahi kuta mtoto ana miaka kama 4 yuko Bording na nikakjuta anaumaa sijui UTI aisee na ndii mazai anaoigiwa simu na cha ajabu mzazi yuko ndani ya huo huo mji, aisee niliumiaga sana, ni kitambo kidogo ila niliumia mno.

Ukiangalia International school,B ording wanaruhsu Umuri fulani tu, hasa wale walioko Madarasa ya juu kabisa na umuri mkubwa wahindi au Wazungu watoto wao hawakai Boring hata kama ni wakubwa.

Kibongobongo ni kawaida kukuta Bording ya Baby class na mzazi anatamba mtaa mzima kwamba yeye ndio mjanja mtoto wake yuko Bording.
Hao wazazi ni wajinga wanakwepa wajibu wao, walitakiwa kuchapwa viboko.
Mtoto wangu wa miaka 5 kulala tu nje ya chumba ninacholala ninaogopa seuze huko mbali boarding
 
Hili limekua tatizo, mzazi anaishi Buhongwa mtoto anasoma Ilemela.
School bus linampitia sa kumi na moja na dk 07, sa sijui anaamka muda gani

Au unakuta katoto kako darasa la tatu kako boarding school.
Wazazi siku hizi wana roho mbaya
Wazazi wanakimbizanq na shilingi..halafu imekuwa kama fasheni watoto kusoma English medium, imekuwa kama vile wazazi wanakwepa majukumu yao ya parenting..yani wanajitahidi wawe na mda mfupi na watoto wao..mda wote wawe shule, yani hata likizo hawataki wazazi wanawafukuzia watoto waende tuition, tena za kuchelewa kurudi, yani mzazi kamwachia mwalimu ajipigiage hela, na walimu wanafurahi maana wako busy na kutoa maswali na kusahihisha, wanashinda shuleni...elimu gani, ipi, inafaa nini? Tumesoma zamani no tuition no what ila hatukuwa worse!! Sikatai ulimwengu uko mbio sana ila malezi mhimu pia, tusiwaachie walimu pekee..kama ni likizo it's time for parents or guardians to have their time for their children, kuwapa yale ya nje ya mtaala wa shule,...mda wa kusoma shuleni uheshimiwe na watoto warudi nyumbani in good time, watoto wadogo chini ya miaka 10 parenting iwe closer na wazazi, wasome shule za karibu ili wasidamke sana japo ni kawaida kuanzia saa 12 lakini sio saa 10 alfajili, ni kuwatesa..pia watoto kuanza shule hata maneno hayajajiumba vema mdomoni, akili bado tunataka kuwahisha shule kwa visababu vingii eti awahi kumaliza masomo..unadhani waliosema aanze la kwanza miaka 6 au 7 walikuwa hawana akili, au kwakuwa tunasema watoto wasasa wanakua haraka? Hapana!!
 
Tatizo ni upumbavu wa akina Baba Junior na Mama Junior. Mtu umezaa mtoto halafu unakosa muda wa kuwa nae si bora ungepiga tu nyeto? Mtoto wa chini ya miaka 12 anatakiwa kuwa karibu na wazazi. Mzazi hakikisha kila siku jioni unapata chakula cha usiku na wanao mezani. Pia hakikisha kila siku asubuhi watoto wanakusalimia face to face na sio mambo ya watoto kuandaliwa na dada wa kazi kuwahi school bus bila kusalimiana nao. Wakati wa likizo kataa habari za tuition. Watengenezee programs ya kazi ndogondogo za mikono.
 
Wazazi wanachangia hili. Siku wakiamua linaisha.
Wazazi,wazazi,wazazi.Inaanza na nyie.Acheni kufuata mikumbo.eti shule hii nzuri sana.... ndio mtoto wako wa nursery au primary school aamke saa 10 alfajiri na kurudi nyumbani saa 1 usiku!!! Sasa ina maana gani? Kuna uzuri gani hapo?
Halafu katika mazingira haya wamama huwaendesha waume zao na limwanaume badala ya kusimama imara kama baba anaacha liwalo na liwe mama mtoto ndio kaipenda hiyo shule!!!
 
Kabisa aisee.. Wazazi wengi wa Tanzania hawaelewi majukumu yao kwenye elimu ya mtoto past kulipa ada.
Yaani shule ikisema kitu, wazazi hawana la kubisha ilhali mzazi anawajibika kuamua welfare ya mtoto wake.
Pia kuna wale wazazi waliopo kamati za shule,wale ndio machawa wanajifanya ndio wanaleta hoja ya wazazi na mzazi unakuwa tayari ushasalitiwa na mzazi mwenzenu.
 
Hili limekua tatizo, mzazi anaishi Buhongwa mtoto anasoma Ilemela.
School bus linampitia sa kumi na moja na dk 07, sa sijui anaamka muda gani

Au unakuta katoto kako darasa la tatu kako boarding school.
Wazazi siku hizi wana roho mbaya
Yote ni kutaka sifa na kushindana kwanin mtoto asisome Buhongwa hapo hapo
 
Kuna kipindi nilikuwa namuamsha mwanangu saa kumi na moja, yaaani anaandaliwa sare anavalishwa anasinzia, chai anakunywa hawezi anasinzia kikombe mdomoni achilia mbl baridi kali ya umande iliyokuwepo!!!

Nikaona hii nikumtesa mtoto daah mpk roho ilikuwa inauma 😁😁😁
Nikaachana na huo ujinga
😂😂😂😂😂
 
Mbona sisi enzi zetu tulisoma shule nasomo yanaanza saa moja na nusu hadi saa nane kamili shule za serikali na binafsi utaratibu ulikuwa huo. Masomo ya ziada ya kulipia ilikuwa hiari ya mzazi.
Nakumbuka nikienda mikoani nilikuwa nawaona wanasoma hadi saa sita halafu wanaenda nyumbani halafu saa nane wanarudi shule hadi saa kumi.
Hiyo ratiba ikirudi itakuwa vizuri sana ,nakumbuka tulikuwa tunapishana wengine wataenda asubuhi wanatoka saa sita,wengine tunaenda saa nne tunatoka saaa nane wengine wanaingia saa sita mchana wanatoka saa 10 ,au mkienda asubuhi mnatoka saa nane
Ratiba ilikuwa nzuri sana na watu walifauru vizuri ,aloleta hii ratiba alaaniwe aisee mi nishaktaa watoto kusoma boarding na likizo marufuku nawasafirisha 😂😂
 
Na bado na likizo wanalazimishwa kuendelea kusoma au wanapewa mzigo wa holiday homework.

Ila nikitafakari ni mateso yamebadilishwa tu, sísi tulilimishwa hadi mashamba ya walimu enzi zetu.
 
Back
Top Bottom