Wazazi mnashirikiana na shule kuwatesa watoto

Wazazi mnashirikiana na shule kuwatesa watoto

Kuna shule anasoma mtoto wa jirani wanaenda had j2, afu ni private.
Najisemeaga Pesa zinatolewa ilo watoto wateseke, lol [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hivi wazazi wamekuwaje zama hizi.. Cha kusomesha watu Weekend ni nini hasa?
Tena madarasa ya mitihani ni mwaka mzima utaratibu ni uleule..
 
Kuna school, ilitaka 50elfu kwa likizo ya mwezi wa sita. Nikagoma watoto nikashinda nao home wiki zote nne nikawa nasikilizia waniulize mtoto wenyewe darasa la tatu ati mwezi wa sita asifunge aamkie shule na kurudi mchana. Huu upuuzi ulikubaliwa na walimu na wazazi mimi sikuhudhuria kikao hicho wife akaja na maazimio nikasema hiiiii!. Shida ni kuwa wazazi wengi hawajenda shule na kukosa kwao elimu wanataka watoto wao wasikose pia. Hiibinapelekea kudanganywa na waalimu kwa kupewa mipango hewa kama hii na wao wana ogopa kuhoji ili ujinga wao usidhihirike na uwoga pia umo.
 
Kuna shule anasoma mtoto wa jirani wanaenda had j2, afu ni private.
Najisemeaga Pesa zinatolewa ilo watoto wateseke, lol [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kwa shule za msingi kiukweli utaratibu ubadilishwe ikiwezekana waingie saa mbili watoke saa 9 masaa 6 ni mengi kwa siku kama yatatumika vizuri hawa bado wanakuwa kuwachosha sana inakuwa si vizuri aisee sasa weekend wanapata lini?
 
Msisahau kuwaandalia mazingira ya kazi watoto wenu wanaosoma hizo shule wakimaliza.

Sifa zisishie tu kupoteza pesa bure kwa kujibana na kujitesa katika hizo shule.

Nawakumbusha elimu ya hapa nchini haitofautiani kati ya shule za pesa na zisizo za pesa kazi inabaki kwako kunyoa au kusuka.
Si kwa shule zote mkuu mfano hizi international school m.f Tanganyika, st contstatine , braeburn na nyenginezo kama hizo wale watoto kwanza wazazi wapo vizuri halafu hata elimu ipo vizuri pia ila upo sahihi kwa kiwango kikubwa.
 
Si kwa shule zote mkuu mfano hizi international school m.f Tanganyika, st contstatine , braeburn na nyenginezo kama hizo wale watoto kwanza wazazi wapo vizuri halafu hata elimu ipo vizuri pia ila upo sahihi kwa kiwango kikubwa.
Hizo shule ulizoandika hazitoi elimu ya hapa Tanzania tofauti na shule zengine ambazo ndizo zinazungumziwa katika huu uzi.
 
Wazazi ndo mmeamua hivyo sasa kama hutaki mwanao awahi acha kumlipia school bus umpeleke hio saa mbili inayoitaka au wote mkatae huo mda wa watoto kuchukuliwa saa kumi .....
 
Yaani mimi my young anasoma grade 4 anaenda anaamka saa 11 anareport shulw saa 12 kamili anaanza na remedial then masomk saa 1 mpaka saa 10 then anaanza remedial tena saa 10-2 usiku...saa mbili ndio naumona home tena..sometimes hatuonani ata siku mbili hivi nakuta tuu kaniachia ujumbe au kanipigia sim dada uko wapi?Dad alienda shule kuweka complains akaambiwa either avumilie au amuhamishe shulw
Duh.. mkuu, hii inatisha..wazazi wengine wanasemaje?
Kwenye magroup ya madarasa pia wanatia pin admins tu ndiyo wacomment.. mi nna imani wazazi wengi hawaridhishwi na hiyo hali..
 
Yaani mimi my young anasoma grade 4 anaenda anaamka saa 11 anareport shulw saa 12 kamili anaanza na remedial then masomk saa 1 mpaka saa 10 then anaanza remedial tena saa 10-2 usiku...saa mbili ndio naumona home tena..sometimes hatuonani ata siku mbili hivi nakuta tuu kaniachia ujumbe au kanipigia sim dada uko wapi?Dad alienda shule kuweka complains akaambiwa either avumilie au amuhamishe shulw
Hiyo ratiba unaona ni sawa kwa mtoto wako?
 
Wazazi, mnashirikiana na shule kuwatesa watoto.

Vitoto vyenyewe bado vidogo, miaka 11-13, vinaamshwa saa 10 au 11 alfajiri kuwahi shule. Wanawahi nini exactly?

Na bado watakaa shule mpaka saa 12 kisa remedials, kurudi nyumbani saa 1 jioni.. mtoto anafika hoi, hajiwezi, hajacheza, hajafanya hobby zake. Kateseka tu.

Yote kwa faida gani?

- Mitihani ya darasa la saba haina umuhimu tena kama ilivyokuwa.
Wenye shule wanawatumia watoto wetu ku-market shule zao ili waonekane wana average ya A, ilhali hata kwa C mtoto anaenda zake secondary school. Au mnataka wakasome St. Francis na Marian? Shule zipo tu. Waliosoma huko si tumewaona chuo na mitaani tunao.

- Masomo ya ziada si kwa kila mwanafunzi kama ambavyo hizi shule zimewaaminisha. Mwanao kipanga, remedials za nini?
Acha wanaostruggle ndo wapambane.
Obviously, wanaunda tu room ya kupiga hela ya michango ya hapa na pale.

Mwisho, tuache watoto wakue kwa amani. Hizo efforts tuzitie form 4 na kuendelea, watakuwa wamekuwa wakubwa na matokeo ya form 4 yana impact mpaka kwenye admission ya chuo, so ni muhimu. Siyo darasa la saba.
Usomaji usio na tija wala manufaa kwa taifa we mtoto aamke saa 10 usiku arudi saa 12 mpaka saa 1 usiku naapo bado ana home workers zinamtolea macho rikizo yenyewe hana anacho kisoma shule akija kuki aplay mtaani hakifanyi kazi apo ndipo mkoloni alituweza ifikie mahala wazazi tuamke kutoka usingizini🥶
 
Bahati mbaya sana wazazi wengine hawafikirii.. matron 1, watoto 20 kwenye bweni.
Mtoto hawezi pata attention ya kutosha kama ya baba na mama yake.
Tena mtoto akiwa mtundu kidogo tu ndiyo kabisaaa matron/patron anaachana naye anafocus na wale watulivu..

Wazazi waache uvivu wa malezi.
Wazazi wanata kuwa free, watoto ni mzigo kwao
 
Wazazi wanachangia hili. Siku wakiamua linaisha.
Wataamuaje wakati wazazi wenyewe ni watumwa? Wanachofanya ni kutengeneza watoto watumwa. Hicho kitu wanapambana watoto wakifuate shule kipo hata kwenye simu zao.
Ifike muda serikali yetu ijitambue. Lakini nachelea kuamini kuwa hamna serikali tuliyonayo au itakayokuja yenye kujitambua kwenye hili
 
Sasa wakuu haya mambo mnayosema hapa si tayari serikali wkt wa msoga ilishatakaga kuingilia kati na kuyakomesha mkawajia juu kuwa yapo private skuls ambako serikali haihusiki na wengine mkaenda mbali zaidi kudai serikali ifanye ivo kwa shule zake tu
 
Back
Top Bottom