guojr
Member
- Dec 4, 2015
- 62
- 95
Kama wazazi au walezi tunapenda watoto wetu wapate elimu ili iwasaidie maishani mwao. Ila kuna hili jambo la wazazi na walezi kupeleka watoto wao kusoma kwenye hivi vyuo vya kati hasa hivi vinavyotambulika kama vyuo vya mipango ambavyo vipo mikoa mbalimbali. Watoto hawa wengine wakiwa chini ya miaka 18 pengine wakiwa bado wanahitaji malezi au uangalizi wa wazazi wao lakini wameachiwa kuishi maisha huru bila uangalizi wowote ni hatari kwa maisha yao ya baadae.
Watoto hawa wakiwa katika mazingira haya mapya na huru wanaweza kujifunza tabia mbalimbali nzuri na mbaya. Wengi wao bado wakiwa bado ni wadogo ki umri na kiakili wanaweza kujifunza mambo yasiyofaa ambayo yanaweza kufuta ndoto zao. Mtoto labda alikua akisoma shule ya bweni maisha yake yote au wazazi walikua wakimuangalia kwa ukaribu ila kumuacha mtoto kwenye mazingira haya yenye uhuru wa kila kila kitu unaweza kuchangia kumuaribu mtoto kitabia. Wawapo vyuoni wanakuatana na watu wenye tabia mbalimbali ila kibinadamu huwa wanavutiwa zaidi na mambo yasiyofaa kama ulevi, uzinifu na hata utumiaji wa madawa ya kulevya.
Watoto hawa wamekua rahisi kudanganyika na vitu vidogo, kama pesa, simu janja, nguo na kadhalika ambavyo vinaweza kuwashawishi kujiingiza kwenye ngono katika umri mdogo. Pia wanaweza kuashawishiwa na vijana wenzao au jamii inayowazunguka na kuwangiza katika tabia zisizofaa. Inauma sana kuona mtoto mdogo kabisa ametoka nyumbani huku wazazi wakiwa na matarajio makubwa na mtoto wao lakini anaporudi nyumbani anakua ameharibikiwa kabisa.
Wazazi na Serikali chukueni hatua mara moja kudhiti janga hili ili kudhibiti mmomonyoko wa maadili kwenye jamii, lakini pia kuwasadia wasije haribikiwa wakiwa wangali wadogo, nao wanamatarajio yao ya baadae. Kwa Serikali ningeshauri wangevifanya vyuo hivi kama shule ya sekondari nikimaanisha kuwe na sheria kali kama vile wapangiwe muda wa kuamka na kulala, wavae sare maalum, kurekodi mahudhurio na kadhalika.
Lakini pia kwa wazazi tuangalie maisha ya baadae ya watoto wetu, hautajisikia vizuri mwanao anarudi nyumbani ni mjamzito au mtumiaji wa madwa ya kulevya, ameathirika na magonjwa ya zinaa au amebadilika kabisa kitabia. Ningeshauri tusiwapeleke watoto wetu mbali ambapo hatuna njia ya kuwaangalia kwa ukaribu.
Nawasilisha.
Watoto hawa wakiwa katika mazingira haya mapya na huru wanaweza kujifunza tabia mbalimbali nzuri na mbaya. Wengi wao bado wakiwa bado ni wadogo ki umri na kiakili wanaweza kujifunza mambo yasiyofaa ambayo yanaweza kufuta ndoto zao. Mtoto labda alikua akisoma shule ya bweni maisha yake yote au wazazi walikua wakimuangalia kwa ukaribu ila kumuacha mtoto kwenye mazingira haya yenye uhuru wa kila kila kitu unaweza kuchangia kumuaribu mtoto kitabia. Wawapo vyuoni wanakuatana na watu wenye tabia mbalimbali ila kibinadamu huwa wanavutiwa zaidi na mambo yasiyofaa kama ulevi, uzinifu na hata utumiaji wa madawa ya kulevya.
Watoto hawa wamekua rahisi kudanganyika na vitu vidogo, kama pesa, simu janja, nguo na kadhalika ambavyo vinaweza kuwashawishi kujiingiza kwenye ngono katika umri mdogo. Pia wanaweza kuashawishiwa na vijana wenzao au jamii inayowazunguka na kuwangiza katika tabia zisizofaa. Inauma sana kuona mtoto mdogo kabisa ametoka nyumbani huku wazazi wakiwa na matarajio makubwa na mtoto wao lakini anaporudi nyumbani anakua ameharibikiwa kabisa.
Wazazi na Serikali chukueni hatua mara moja kudhiti janga hili ili kudhibiti mmomonyoko wa maadili kwenye jamii, lakini pia kuwasadia wasije haribikiwa wakiwa wangali wadogo, nao wanamatarajio yao ya baadae. Kwa Serikali ningeshauri wangevifanya vyuo hivi kama shule ya sekondari nikimaanisha kuwe na sheria kali kama vile wapangiwe muda wa kuamka na kulala, wavae sare maalum, kurekodi mahudhurio na kadhalika.
Lakini pia kwa wazazi tuangalie maisha ya baadae ya watoto wetu, hautajisikia vizuri mwanao anarudi nyumbani ni mjamzito au mtumiaji wa madwa ya kulevya, ameathirika na magonjwa ya zinaa au amebadilika kabisa kitabia. Ningeshauri tusiwapeleke watoto wetu mbali ambapo hatuna njia ya kuwaangalia kwa ukaribu.
Nawasilisha.