Wazazi wapumzisheni watoto wenu. Ngoma hii ni ngumu, wapeni moyo

Wazazi wapumzisheni watoto wenu. Ngoma hii ni ngumu, wapeni moyo

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
WAZAZI WAPUMZISHENI WATOTO WENU; NGOMA BADO NGUMU. WAPENI MOYO.

Anaandika, Robert Heriel

Inawezekana wewe ni miongoni mwa Vijana mnaopitia kipindi kigumu Kutokana na shinikizo la wazazi wakikutaka Uajiriwe.
Licha ya kuwaambia upatikanaji wa kazi umekuwa ni mgumu lakini bado wazazi wamekuwa wagumu kuelewa.
Wanakuona mzembe,
Wanakuona haujishughulishi,
Na imefikia hatua wanakuona hauna Faida, ni kama walipata hasara kukuzaa na kukusomesha.

Wanakuambia mbona wenzako wanapata ajira lakini wewe wanakuona umebung'aa. Lawama na mateto yamekuwa sehemu ya Maisha yako kila wakupigiapo simu. Inafikia hatua ukiona simu ya wazazi unaogopa kupokea.

Wazazi wapumzisheni Watoto wenu. Wapeni Moyo. Hali ni ngumu mno. Kuwasomesha Watoto wenu isiwe fimbo ya kuwachapia Watoto wenu. Jueni mnawapa hali ngumu huko walipo.
Mazingira yamebadilika Sana.
Elimu pekee haitoshi kumfanya mtoto wako afanye vizuri. Ni unyanyasaji, utendaji, uonevu kumshinikiza mtoto wako kuhusu mambo ya Kazi bila kuangalia mazingira ya dunia Hii yamekaaje.

Taikon mpaka naandika, nimekutana na visa na mikasa, nimejiridhisha Vijana wengi wapo katika Depression kubwa inayotokana na mashinikizo mengi ukiwepo shinikizo kutoka Kwa wazazi.

Wazazi msitake Watoto wenu wajiingize kwenye mishe hatari ili nao waonekane wanawatumieni Pesa.

Mnawaambia Watoto warudi nyumbani, wakirudi nyumbani shida, mnawasema, mnawanyanyasa, wengine wanafikia hatua ya kujiua, kujiingiza kwenye madawa ya kulevya.
Huku wengine wakiamua kuolewa ilimradi nao waondoke katika Himaya yenu.
Sio ajabu wengine wanapanga njama kuwaua ili warithi Mali.

Wakiondoka nyumbani Napo Kero.
Mtoto hajui atakula nini atakuwaza wewe?
Mtoto hajui atalipaje Kodi atakufikiria wewe? ATI kisa ulimsomesha?

Vijana wa sasa wanapitia kipindi kigumu mno. Wanahitaji Faraja, upendo, kuwaombea na sio kuwasema kisa wanashindwa kuwatumia Pesa.

Maneno yenu ya kejeli kisa ni wazazi hayafurahishi. Na kama Watoto wanashindwa kuwaambia, Mimi Taikon nitawaambia Ukweli. Mkiumia Sawa kwani hampendi ukweli, mkiukubali Sawa Pia.

Wapeni Watoto wenu mitaji, alafu wakishindwa kuwasaidia ndio mlalame na kuwakejeli, na sio muwatie Vijana Stress za kijinga jinga kisa mliwazaa au kuwasomesha. Hiyo sio Haki.

Nawapongeza wazazi wote wenye uelewa, wanaojua dunia Ipo kipindi gani. Waelimisheni wazazi wengine kuwa dunia ya sasa ni yakibepari, sio Ile dunia ya kijima tena.
Na ninyi wazazi mnaowapa Stress Watoto wenu acheni hiyo Tabia ya hovyo. Vijana wa sasa hatutavumilia.

Mnasema Vijana wa sasa wanalaana, laana mliwapa nyie sio?
Ninyi msio na laana mbona mnawasumbua wenye Laana badala ya kuwabariki?

Wapeni Moyo Watoto wenu. Maneno yenu ya kijinga na vitisho ni upuuzi tuu, mnaharibu jamii na taifa Kwa sababu ya ubinafsi wenu. Hamuvai viatu vya Watoto wenu ndio maana wanawatesa.
Badilikeni!

Nafahamu hata Mimi ni mzazi. Hivyo ujumbe huu unamhusu MTU yeyote.

Nipumzike SASA!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Mimi ni mzazi na kazi sina, naanzaje kumlaumu mtoto kukosa kazi?

Nitamfundisha skills za kuishi bila kazi mpaka wenye kazi wakikwama wana kuja kukosa kwangu.
 
Wasio na elimu ndiyo watafanya hivyo na humu hawamo humu ni Great thinkers only
 
Ni mda mwafaka wazazi kuwapa watoto mwelekeo mpya , aina ya elimu wanayopata kwa Sasa Haina faida Tena. Naona njia Bora ni kuwapa elimu kiasi na kuwapa mwelekeo WA kufanya ujasiriamali kwa kuwaftia mitaji
 
Ni mda mwafaka wazazi kuwapa watoto mwelekeo mpya , aina ya elimu wanayopata kwa Sasa Haina faida Tena. Naona njia Bora ni kuwapa elimu kiasi na kuwapa mwelekeo WA kufanya ujasiriamali kwa kuwaftia mitaji
Kwa Tanzania tumefungwa sana, hata ku invest katika masoko ya kimataifa ni mgogoro mkubwa sana wa kisheria.

Juzi nilikuwa naongea na dogo mmoja hapa kitaa (US). Huwa napenda kupiga nao stories, kuwafuatilia wanafundishwa nini shuleni.

Ana miaka 14 lakini anajua mambo ya stock trading, investments, etfs, indexes, economic calendar.

Anasema shuleni kwao wanafundishwa katika somo maalum la "Wealth Management" na wametengenezewa accounts za MarketWatch wanafuatilia Stock Markets (ingawa si kwa hela za kweli, ni hela za kufanyia practice).


Wanashindanishwa shuleni kwao kuona nani anaweza kutengeneza faida zaidi kwenye stock market.

Nikawa namuuliza maswali mengi, nilishangaa anajua mpaka mambo ya ETF zinazoenda na indexes, nikamuuliza kuhusu investment strategy, akasema ana diversified investment strategy kwenye phramaceuticals, tech na ETFs, akasema stock market iko chini na inaweza kushuka zaidi, lakini kwa long term investors itapanda tu, anafuatilia markets.

Nikasema natamani na mimi ningekulia nchi hii nilivyokuwa na miaka 14 ningekuwa naja haya.
 
Mimi ni mzazi na kazi sina, naanzaje kumlaumu mtoto kukosa kazi?

Nitamfundisha skills za kuishi bila kazi mpaka wenye kazi wakikwama wana kuja kukosa kwangu.

Wapo mabinti wengi wamejiingiza kwenye michezo migumu Kwa shinikizo
 
Kwa Tanzania tumefungwa sana, hata ku invest katika masoko ya kimataifa ni mgogoro mkubwa sana wa kisheria.

Juzi nilikuwa naongea na dogo mmoja hapa kitaa (US). Huwa napenda kupiga nao stories, kuwafuatilia wanafundishwa nini shuleni.

Ana miaka 14 lakini anajua mambo ya stock trading, investments, etfs, indexes, economic calendar.

Anasema shuleni kwao wanafundishwa katika somo maalum la "Wealth Management" na wametengenezewa accounts za MarketWatch wanafuatilia Stock Markets (ingawa si kwa hela za kweli, ni hela za kufanyia practice).


Wanashindanishwa shuleni kwao kuona nani anaweza kutengeneza faida zaidi kwenye stock market.

Nikawa namuuliza maswali mengi, nilishangaa anajua mpaka mambo ya ETF zinazoenda na indexes, nikamuuliza kuhusu investment strategy, akasema ana diversified investment strategy kwenye phramaceuticals, tech na ETFs, akasema stock market iko chini na inaweza kushuka zaidi, lakini kwa long term investors itapanda tu, anafuatilia markets.

Nikasema natamani na mimi ningekulia nchi hii nilivyokuwa na miaka 14 ningekuwa naja haya.

Jamii yetu mzazi akikusomesha anataka uajiriwe tuu. Hata kama hakun Ajira bado atakuona wewe ndio mzembe wa kutafuta
 
Taikon kwny moja na mbili,madini haya walengwa ujumbe uwafikie sisi ambao hatuna watoto na hatujaoa tunasubir nyuzi zetu
 
Taikon nakukubali sana nakura yangu nimekupa ww unandika vtu reality vya maisha. Ni kicompare treatment kipind jobless na saiv na kajira aisee nimeamin ukiwa una kaz/hela mzaz anakwa na hasira na ww.kingine wanajisifia san kwa wenzao mtt wang anasom degree anazn ukimlza unaingia kwenye kaz kumb kuna kipind cha mpito.
 
Taikon nakukubali sana nakura yangu nimekupa ww unandika vtu reality vya maisha. Ni kicompare treatment kipind jobless na saiv na kajira aisee nimeamin ukiwa una kaz/hela mzaz anakwa na hasira na ww.kingine wanajisifia san kwa wenzao mtt wang anasom degree anazn ukimlza unaingia kwenye kaz kumb kuna kipind cha mpito.


Mkuu nashukuru Sana Kwa Kura yako.
Pole Sana. Jipe moyo
 
Back
Top Bottom