Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Ukiwa na wewe uko na li Prado hivi huguswi ila kama una passo unaonekana kabisa Masai kaingia disko
 
Ni kwel mommah,
 
Hawa jamaa sio! Unaweza kuamua kufuata sheria zote halafu kuna mahali unakuta wameondoa kibao cha 50 limit, unashangaa unaoneshwa picha umepita na 100kph kwenye 50kph
Huo uhuni wao sasa ndiyo ambao hupelekea watu kuwa wakali! Kuna makosa mengine wanayatafuta na kuyakuza tu kwa lazima!

Nimekumbuka mzee wangu aliwahi kupita kwenye 50kph zone kufika mbele wakamsimamisha anaambiwa kazidisha eti speed inasoma 57kph!

Akawaambia gari yake speedometer iko katika mfumo wa miles per hour na siyo kms per hour! Yeye aliingia na 35mph akijua kwamba hiyo haichezi mbali na 50kph na haina shida sana!

Yule traffic akawa anakomaa tu oo umezidisha 7 sijui nini! Mzee ikabidi aanze kuwa mkali akamuambia "kwahiyo we mama umenisimamisha hapa barabarani muda wote huo tunabishana kisa hizo 7 tu" hahaaa alikomaa kweli ikabidi traffic amuachie tu!
 
Kuna jamaa alinunua i think inaitwa Land wind something like that, 2011 kufika 2014 kila kitu ndani ya gari kimeng'oka! Yaani vents,panels na vitu vidogo vidogo. Gari ina miaka mitatu tu!
Duuh hizi Land Wind si ndiyo zile mchina alitoa copy ukiiangalia hivi Range Rover hii hapa. Kasoro vitu vichache tu ndiyo walibadilisha.

Nilisikia hadi Land Rover waliwashitaki kwa kucopy bila makubaliano yoyote sasa sijui waliishia wapi. Daah Wachina ni copycats balaa.
 
Jamii hio hio za mwanzo kabla hajaamua kutoa photocopy ya LR Evoque
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…