Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Najitahidi sana mkuu kufuata sheria....Japo wakati mwingine tunajisahau tunavunja sheria..[emoji38]
 
Kwa mwaka napata vyeti kama vinne hivi. Hii ya juzi nilipata cheti kimoja nimeingia kwenye 50 nikahisi hawapo nikajiachia!
Hahaha...naona unachangia mapato ya nchi kwa kiasi chake..[emoji119][emoji119]

Cheti cha kwanza ilikuwa mwaka 2016..nilipigwa tochi..

Cheti cha pili Mwaka 2018 bima ilikuwa imeisha muda wake nikapuuzia..[emoji119][emoji119][emoji119]hatari sana..

Cheti cha tatu 2020 niliovateki darajani....

Cheti cha nne Mwaka huu 2022...niliovateki on the same area.
[emoji38][emoji38][emoji38]

Mimi kuandikiwa cheti ni kila baada ya miaka 2....ikitokea nikaandikiwa cheti kabla ya miaka 2 kupita, nitakileta hapa mchangie...maana kipo nje ya bajeti..[emoji38][emoji119][emoji119][emoji119][emoji2960]
 
Hongera sana
 
siwezi tembea km 2000 nikakoswaaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].km 2000 ni nyingi sana, kwa sisi vijana si rahisi kutoboa hizo km bila Cheti...
Kijana akipitwa hata na gari namba SU, DFP, STK...kijana anaaza nao ligi. [emoji38][emoji38]...wenzetu hawaandikiwi vyeti
 
Nilipata mkuu, wa kawaida tu, baba mmoja alikuwa na mtoto wake. Na huwa sichukui abiria wenye mizigo
Kuna siku nilikua natoka dar kwenda bara. Nikapita mbezi kulikua na watu wengi saaana na gari ndogo nyingi Mida ya saa Saba mchanna.

Nika park wakanikimbilai vijana wanasema wana abiria wa Moro nikawambia nahitaji wa moja Kwa moja mpaka dom waksema hakuna hapo hao abiria wote ni wa Moro wanangoja abood zitoke Moro zije ziwabebe.

Wakati natafakari akatokea mbaba mmoja kavaa nguo za kimasai akaniuliza naenda wapi nikamjibu Dom, akauliza nauli ya Dom ngapi nikamtaji. Akasema yeye analipa nauli ya Dom lakini atashuka Moro na yupo na mwanae. Nikasema hamna shida.

Tuka Anza safari Yule Mzee WA kimasai alikaa seat ya mbele na mwanae nyuma. Nilianza kuona kero baada ya Mzee kuingiza mkono wake kwenye shuka lake na kukuna P***bu Kama vile yupo peke Ake chooni hivi ili bidi nizime AC tule upepo maana Hali ilibadilika. Mpaka tuna fika Moro Ile pesa yake ikabidi ninunue manukato.
 
😂😂😂😂😂
 
Ha ha ha pole sana! Kuna watu ukiwapakia inabidi ufungue vioo!
 
Za kubrashi viatu huwa natoa..sometimes nasimamishwa, wananikagua wanakuta nipo safi...

Basi unakuta jamaa anaomba ya maji kistarabu...natoa chenchi yoyote iliyopo karibu..[emoji119][emoji119][emoji2960][emoji2960]
Hongera sidhani kama nishamaliza mwaka bila mikeka miwili mitatu, na hapo za kubrush viatu zinakuwepo sana tu.


Kama juzi hapo Makanya - Same watu walinunua kiwi mpya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…