Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Sisi wazee wa bro niazime gari nitaweka mafuta unatusagia kunguni. Tunaweka ya elfu Tano Ili taa isiwake tunaporudisha gari 😂😂😂
 
Sisi wazee wa bro niazime gari nitaweka mafuta unatusagia kunguni. Tunaweka ya elfu Tano Ili taa isiwake tunaporudisha gari [emoji23][emoji23][emoji23]
Hahah!
Sema huwa mnajua kujiongeza..mtu anakuja kuweka ya bei ndogo halafu anaomba risiti ya bei kubwa aende nayo kumpiga mtu cha juu.
Wa hivi hawanaga shida,akija ni stori mnacheka kwa kwenda mbele,huku mkimtafutia risiti ya hela kubwa kwenye kapu la taka.
 
Nitakuja mimi kukusalimia
 
Mjini mipango Dada, nipe location mwezi ujao nitakuwa napita kununua petrol ya elfu 5. Kwenye kidumu Cha Lita 5 ya boti.
 
Maana viongozi wanakaa wanawashangaa vijana ambao hatuna ajira..wanasema jiajirini ila mitaji hakuna na wanasema hakuna hela za kutosha kuwapa mitaji.
Kuna mdau[emoji23]akasema kama vipi watukusanye tu watupige mnada nchi za nje kama mbolea.
"Hii nchi bhana wanaowaambia vijana wajiajiri nao wameajiriwa hawataki kuachia ngazi na bado wanawachomeka watoto wao na ndugu zao kwenye system". Alisikika kijana mmoja jobless asiye na mtaji.
 
"Hii nchi bhana wanaowaambia vijana wajiajiri nao wameajiriwa hawataki kuachia ngazi na bado wanawachomeka watoto wao na ndugu zao kwenye system". Alisikika kijana mmoja jobless asiye na mtaji.
Wanapigana vijembe usiku na mchana wanatafutana kisa uongozi,ila wanasema vijana jiajirini.
"Ni maneno ya kajobless kamoja hivi baada ya kunyooshwa na kitaa😂😂😂"
 
Na nyie huwa mnauza risiti. Mara nyingi huwa wananiomba risiti zangu za full tank! Nawaambia gari ya Muhindi lazima niipeleke hii.
 
Pantoni hili hili na mateso yake yote?

Jana jioni nimetoka kugeuza pale chuo cha ustawi maana foleni ya pantoni ilifika kule, nikageuka mpaka darajani na nikafika muda sawa na aliyevuka kwa miguu

Mwezi uliopita nilispend 2 hours kuvuka pale na pantoni

Labda wewe unaliotea mida yake unavuka shwaap, ila mimi kwangu limelaanika lile dude
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…