Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Duuh hilo MV Kigamboni silioteagi kulipanda. Mara nyingi mie nayakutaga MV Magogoni na MV Kazi, hilo linaonekana bovu tayari lishachoka sema kuna siku wanalilazimisha tu, hayo mengine mawili mbona yanapiga kazi fresh tu.
Sasa hivi MV Kigamboni liko poa. MV Kazi imekuwa kimeo. Jembe MV Magogoni tu.
 
Sasa hivi MV Kigamboni liko poa. MV Kazi imekuwa kimeo. Jembe MV Magogoni tu.
Oohh bora kama wamelitengeneza maana kuna kipindi nilikuwaga silioni kila nikifika nakuta Magogoni na Kazi tu ndiyo zinapishana. Halafu mimi kila mara lazima nijikute natumbukia Magogoni hilo Kazi ni kama linanikwepa hivi haha.
 
Mbweni si ndo kule mvua ikinyesha wote mnahama kwa muda?

Au sio huko? Juzi nimeambiwa kiwanja sqm 1 = 15k.
Hahaa umenichekesha mkuu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Yeah kuna maeneo mvua zikinyesha hapatamaniki mfano kule kwa kina Halima Mdee wanakuita sijui Moga sema siku hizi wameanza kuchimba mitaro.

Ila kule kwingine Jeshini, Usalama, Kwa Mama Samia, Teta, hadi kule Stendi mwisho wa lami kuko vizuri na watu wanazidi kuporomosha mijengo tu
 
Tumeuanza mwaka Ila kuna mtu sioni ski comment siku hizi. Bwana Extrovert kimya mno. Ingekua ni bwana RRONDO angesha tafutwa Kwa udi na uvumbe na hizi pic Kali.

Mm nilipata mzinga mwaka Jana nikapotea muda mrefuuu hakuna ATA alie ulizia hehe. Tumshukuru mungu tuko hai. Binafsi nimeuona uwepo wa mungu. Tukumbukane thou hatufahamiani.
 
Extrovert yupo majukwaani huko tunakutana naye..ila hajaingia tu humu...ndiyo maana hajauliziwa.

Pole sana kwa ajali mkuu,,
Next time ukiadimika tunaahidi tutakutafuta kwa nguvu zote.

Mungu wa Mbinguni akulinde[emoji120]
 
Pole sana. Extrovert yupo anachangia nyuzi nyingine kama kawaida. Pole tena kwa ajali natumaini uko poa sasa hivi.
 
Duh mkuu pole sana kwa ajali mbaya...mie nipo mkuu, heri ya mwaka mpya mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…