Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?


Ni ya mbunge wa Kinondoni ABASS TARIMBA..mbona inafahamika sana hata bungen anaendaga nayo,mara nyingi ikiwa mjin anaendeshaga mwanae
 
Gari kama hii inapitaga msamvu Morogoro mara nyingi tu...
 
Starting price 173,000 USD roughly kama Million 400 TZS ikiwa 0 km lakini used TZS 150 Mln...mzigo bei ya T L/Cruiser latest
 
Sasa mbona 40 ndio nyembamba zaidi! Unatakiwa urudie kwenye 20 sasahivi. Jiandae na 20w50
5w40 ni nzito kidogo kulingana na 5w30 injini ikishafikisha joto linalotakiwa, ila kwenye cold start, zote ni sawa kwa sababu zote zinaanza na 5w..

Mkuu gari ndogo siwezi kuweka 20w 50....mpaka nifikie hiyo viscosity, nadhani nitakuwa sina hilo gari tena..😆😆
 
Mkuu suala la kubadili viscosity over time, ni technical issue mkuu .siyo myth kama wasemavyo watu...

SAE wanasema injini ikishafikisha mile age zaidi ya km laki 1, hiyo injini tayari imeanza kuzeeka,

Hivyo ndani inakuwa na parts ambazo zimeshaanza kulika.....haoa wanashauri ubadilisha viscosity, kutoka namba ndogo na kwenda kubwa mfano kutoka 5w30 kwenda 5w40 n.k..
Oil nzito inaleta ulinzi mzuri kwa injini zilizozeeka..tofauti na oil nyepesi.
 
Mkuu kwenye maelezo yako umefafanua vizuri..😀😀
Ila viscosity ya 20w50 kwa kweli siwezi kutumia kwenye gari ambalo nilianza kulitumia mwenyewe kwa mara ya kwanza lilipoingia nchini..
.ila ingekuwa ni gari nimenunua kwa mtu huko, na limechoka hapo sawa..coz siwezi kujua alikuwa analitunza vipi..😆😆

Mimi nimekuwa nikitumia 5w30 kama manual inavyosema, kwa sasa gari langu lina km 163k...nimehamia 5w40...

20w 50 ni nzito sana mkuu kwa injini ndogo .

Hizo tuwaachie watu wa Rav4 Massawe zenye 3s😆😆😆 au wenye GX 100....hizo tuwaachie wao....

5w30 au 5w50, injini ina run smoothly...
Kuna kipindi nilijichanganya mikaweka SAE40 monograde, nilijuta...asubuhi nikiwasha gari RPM inapanda sana na inakawiwa kushuka, wakati huo nasikia kelele ambayo si ya kawaida kwenye too cover kutoka kweny cam shaft..🙌🙌🙌
 
Maelezo mazuri.. Ila hapo W hiyo ni Winter..
Hapa TZ monograde oil inatosha kabisa.. Hii mambo ya multigrade ni marketing tuu..!
Hizo ni oil za kutumika nje ambapo kwenye mwaka kuna majira tofauti..!
Mkuu naheshimu msimamo wako...😊..

Multi grade oils zinasaidia kusambaa sehemu zote za injini within ten seconds, at most...unlike monograde..

Ndiyo maana gari nyingi za siku hizi hazina haja ya kuoasha injini sijui nusu saa kabla ya safari,....kama unatumia oil ambayo ni multi grade, ni kuwasha na kusepa...

Watengenezaji wa magari wamekadiria kuwa, ukiwasha gari, ufunge seat belt umalize, sekunde kumi zitakuwa zimetimia na oil itakuwa imefika kila eneo..

SAE 40 kavu inaua injini ndogo za petrol taratiibu....
Unakutana na Passo Camshaft zinagonga kama injini ya tractor, hayo ni madhara ya SAE 40 kwenye injini ambazo zilipendwkezwa kutumia multi grade oils
 
Sure.. Kwa scenario hiyo ya kuwasha na kuondoka hapo hapo multigrade ni bora..

Halafu kwenye mapendekezo hapo.. Unadhani manufacturers huwa wanatuconsider waswahili..!!? Nahisi zile ni recommendations za engine kwenye mazingira yao..!!
 
Hahahahahah mkuu kwa engine ambazo sio vvt-i kama family ya RZ, A, S,JZ hizo kitumia 5w 30 oil inaweza ika leak 😅 inakuwa kama maji kabisa na unaweza shangaa gari inakula oil! 20w 50 ndio engine oil nzuri kwao.

Ila kwa gari mpya hizi za VVT-i inakuwa freshi sana ukiweka namba 30 au 40 inakuwa poa zaidi.
 
Mabus yana mwendo mzuri, kwa upande wa private car nikiwa naenda field nakodiwa gari na kampuni so namcontrol dereva speed ninayotaka.
Bora vurugu za mabus au top speed za private?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…